WANAWAKE 481 WAPATA HATI MILKI ZA KIMILA TANGANYIKA.


Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na maendeleo ya makazi,Geofrey Pinda akikabidhiwa hati Milki za kimila na Mkurugenzi wa Taasisi ya Jane Goodall ,Dkt  Kasukura Nyamaka leo katika kijiji cha Vikonge kata ya Tongwe wilaya ya Tangantika Mkoa wa Katavi.

Na George Mwigulu, Tanganyika.

Baadhi ya wanawake katika  wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wamepewa usawa wa kijisia kwenye  utekelezaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kukuza hali ya upatikanaji sawa wa rasilimali na fursa bila kujali jinsia.

Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na maendeleo ya makazi,Geofrey Pinda akikabidhi hati milki ya kimila kwa moja ya wanawake 1337 waliokabidhiwa leo katika kijiji cha Vikonge Kata ya Tongwe Wilaya ya Tanganyika mkoani humo.

Afisa ardhi wilaya ya Tanganyika,Mussa Yohana amesema hayo leo wakati wa kukabidhi hati Milki za kimila katika kijiji cha  Vikonge kata ya Tongwe ambapo utekelezaji wa mradi huo umefanikiwa kuboresha milki za ardhi bure  kwa kupima mashamba na viwanja 3460 na kutoa hatimilki 1337 kwa wananchi.

Yohana ameeleza juhudi za kuhakikisha usawa wa kijisia kwenye upatikanaji sawa wa rasilimali wameweza kutoa  fursa sawa kwa jinsia zote kushiriki ambapo kati ya hati 1337,hati 481 sawa na asilimia 36 zimesajiliwa kwa majina ya njinsi ya kike.

Wanawake kushiriki katika zoezi la umilikishaji kulikuwa na changamoto mkubwa kwa kuwa na mfumo dume ambao jamii inaamini kuwa kwenye haki ya kumiliki ardhi ni mwanaume lakini kwa kutumia sheria namba 4 na 5 ya mwaka 1999 imetoa fursa kwa mwanamke nafasi sawa na mwanaume ya kumiliki ardhi.

Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi,Mussa Yohana akizungumzia jitihada ambazo zimewafanya kufanikiwa kutoa hati Milki za kimila kwa wanawake wa wilaya hiyo.

“sheria hii imetoa fursa ambayo tumeitumia katika utekelezaji wa mradi huu ambapo tumetoa hamasa kwa wanawake kushiriki na kutafasiri  sheria ili wapate fursa ya kumiliki ardhi sawa na wanaume” amesema Afisa wa ardhi huyo.

Kutokana na wanawake kutengwa kwenye umilki wa mali kwenye ngazi ya familia wamefanikiwa kuhamasisha umilki wa pamoja  baba na mama kwa umoja wao kushiriki katika zoezi la upimaji wa vipande vyao vya ardhi kwa kupigwa picha pamoja na hati kutoka kwa majina ya mawili ya mume na mke.

“tumetoa pia fursa kwa mwanamke ambaye kimsingi ametafuta ardhi kwa nguvu yake naye amehamasishwa bila kuingiliwa na mtu mwingine kwenye maamuzi naye ameweza kushiriki kwenye upimaji na kupewa hati milki kwa jina lake”.amesema Yohana.


Aidha ambao wamepata ardhi ya mirathi au kwa waume zao waliofariki kwa mujibu wa sheria wametoa hamasa kwa wananchi kwamba wasiingiliwe na ndugu na jamaa wa marehemu kwa sababu ni mali waliyoipata pamoja na wanahaki ya kumilki ardhi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Jane Goodall,Dkt Kasukura Nyamaka amesema  taasisi inashirikiana na halmashauri ya wilaya ya Tanganyika,Uvinza na Kigoma kuandaa matumizi ya ardhi ya vijiji na mipango ya matumizi ya ardhi ya wilaya.

Mradi wa LCWT umeziwezesha serikali za vijiji kwa kushirikiana na halmashauri za wilaya kuandaa,kutathimini na kurejea mipango ya matumizi ya ardhi kwa vijiji 53 kata 74 imetekelezwa na taasisi miradi mingine ya miaka ya nyuma kati ya mipango ya ardhi ya matumizi ya ardhi ya vijiji 53 imerejewa,mipango 46 imewasilishwa tume ya taifa ya mipango ya matumizi ya ardhi.

Dkt Nyamaka amesema kuwa lengo la Jane Goodall la kufadhili upimaji wa vipande vya ardhi na utoaji wa hati Milki za kimila ni kuongeza ushirikishwaji wa wanawake na vijana kwenye masuala ya umiliki na usimamizi wa rasilimali ardhi ili kuongeza chachu ya uhifadhi wa maliasili za misitu na wanyamapori hasa Sokwemtu.

Naibu waziri wa Ardhi,Nyumba na maendeleo ya makazi,Geofrey Pinda akikabidhi hati Milki ya kilima kwa mume na mke ambapo hati hiyo inaumilki wa pamoja.

“taasisi ya Jane Goodall kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya ya Tanganyika,Uvinza na Kigoma tumefanikiwa kupima na kukusanya taarifa za vipande 13,105 katika vijiji 12 ambapo tunatarajia  watu 13,749 watanufaika na upimaji huo ikiwa vijana wa kike 1,218 na wanawake watu wazima 4,092” Amesema Dkt Nyamaka.

Eliata Korinalio,Mkazi wa Kijiji cha Vikonge Wilaya ya Tanganyika ambaye ni mnufaika wa kuwepa hati milki ya kimila ameishukuru serikali kwa kushitikiana na taasisi ya Jane Goodall kwa kufanikisha adhima yao ya kumiliki ardhi.

Amesema hati hizo zitawasaidia kama dhamana ya kupewa mikopo ya fedha ambazo zitaboresha mitaji kupitia biashara wanazofanya.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages