WAUGUZI WASIO WAADILIFU WAONYWA NSIMBO.


Anna Lupembe,Mbunge wa Jimbo la Nsimbo wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi akiwahutubia wananchi wa kata ya Uruwila.

Na George Mwigulu,Nsimbo.

Wauguzi wa afya katika halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wametakiwa kuzingatia maadili yao ya kazi wanapotoa huduma kwa wananchi pindi wanapokwenda katika  zahanati  kutafuta matibabu.

Wauguzi wa afya katika halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wametakiwa kuzingatia maadili yao ya kazi wanapotoa huduma kwa wananchi pindi wanapokwenda katika  zahanati  kutafuta matibabu.

Wito huo umetolewa leo na Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kata ya Uruwila ambapo amepokea malalamiko ya  baadhi ya wanawake wa kata hiyo kuwa wanachoteshwa ndoo za maji pindi pale wanapojifungua kwenye baadhi ya zahanati.

Baadhi ya wanawake wakitoa  kero zao kwa mbunge huyo wameeleza  kuwa wanapopata uchungu na kwenda kujifungua katika zahanati za serikali wanapomaliza kujifungua kabla hawajaruhusiwa wamekuwa wakitakiwa kuchota ndoo tano za maji wakati huo ni wazazi na hawana nguvu za kuchota maji.

Baada ya kupokea kero hiyo,Mbunge Anna Lupembe ametoa onyo  kwa wauguzi wa afya wanaojihusisha na vitendo hivyo kwani kipo kinyume na maadili ya kazi.

Lupembe amesema kuwa muuguzi ni kipaji ambacho wamepewa na Mungu na wanatakiwa kuwa na huruma kwa wananchi.

Revocatus Mapula Mtendaji wa Kata ya Uruwila amekiri kuwepo kwa vitendo hicho kwa kipindi cha zamani lakini kwa sasa walishapiga marufuku na hakipo tena.

“nilimwita inchaji wa zahanati hiyo nikamwambia ni marafuku mama yeyote akijifungua wewe umwagize akachote maji…huko nyuma kweli lilikuwepo na kwa bahati nzuri kwenye kikao cha Isagala juzi tuliliongelea na kulitolea ufafanuzi na Mh Diwani akakemea hilo.Sasa kama linaendelea tunaomba mtuletee ili tulishughulike” Amesema Mapula.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages