WAZAZI ACHENI KUWATUMIKISHA WATOTO MIGODINI

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki akizungumza na wanawake wa UWT kata ya Machimboni ambapo amewaasa kusaimama imala katika malezi ya watoto wao.

Na Paul Mathias,Nsimbo

Baadhi ya Wazazi na walezi Katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wameonywa kutowatumikisha watoto katika Shuguli za uchimbaji wa Madini na badala yake wahakikishe watoto wao wanawapeleka Shule ili wapate Elimu.

Muonekano wa Shuhguli za uchimbaji wa Madini katika Kata  ya  Machimboni ambapo baadhi ya wazazi huwatukisha watoto katika kazi hizo 

Baadhi ya Wazazi na walezi Katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wameonywa kutowatumikisha watoto katika Shuguli za uchimbaji wa Madini na badala yake wahakikishe watoto wao wanawapeleka Shule ili wapate Elimu.

Wito huo umetolewa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki wakati wa ziara yake ya kutembelea Kata za Mkoa wa Katavi alipokuwa anazungumza na Umoja wa wanawake UWT kata ya Machimboni pamoja na wanachama wa chama cha Mapinduzi.

Amesema kuna tatizo la baadhi ya wazazi kuwatumikisha watoto wadogo katika shughuli za uchimbaji wa Madini kwa ujira mdogo kitu ambacho ni kinyume na sheria hali ambayo huwafanya baadhi ya watoto kuacha shule au kuwa watoro kwa kujiingiza katika kazi hizo.

Mbunge wa Viti maalumu Martha Mariki [Kulia] akisalimiana na Vikundi vya Ngoma ya Asili apofika katika Kata ya Stalike.

Mbunge huyo anasema ‘’ajira kwa watoto hairuhusiwi watoto hawa wanatakiwa waende Shuleni mfano wewe unamgodi wako unawatumikisha watoto katika eneo lako la Machimbo hiloharikubariki sheria inasema nikosa kwa mtoto kumwajili chini ya miaka 18 nilazima achukuliwe hatua kwani anamnyima haki ya kupata masomo ‘’amesema Mb Martha

Ameeleza kuwa kazi ya Machimbo huhitaji watu wenye umri mkubwa ambao wapo juu ya miaka 18 hivyo kuwa fanyisha kazi hizo nzito machimboni niku hatarisha usalama wao kwani hufanya kazi ambazo haziendani na umri wao.

‘’kwanza unamfanyisha kazi mtoto huyu ambazo si za umri wake sheria zinasema ili mtu aweze kufanya kazi lazima afikishe miaka 18 ili aweze kujitambua na kuingia mkataba wa kazi husika anayoifanya tatizo hili niliambiwa pia katika Kata ya Magamba wazazi tuwajibike katika hili ‘’amesisitiza Mb Martha

Diwani wa Kata ya Stalike Adam Chalamila[kushoto]akiteta jambo na Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Martha Mariki akiwa katika Kata ya Stalike

Katika hatua nyingine ameziomba Jumuiya za Wazazi na UWT ngazi ya Kata kuhakikisha wanatembelea Shule ili kujiridhisha mwenendo wa Mahudhurio ya Wanafunzi shule ili iwe rahisi kuchukua hatua kwa wazazi ambao watabainika kuwatumia watoto hao katika shughuli za uchimbaji wa Madini.

’jumuiya ya wazazi mpo hapa jumuiya ya wanawake mpo hapa nendeni shuleni mkafatilie mienendo ya watoto Shuleni huko wapi ni Watoro wapi ambao hawaendi shuleni wamekimbilia Shughuli za Machimbo’’ameeleza Mbunge huyo.

Awali akiwa katika Kata ya Stalike ameishukuru serikali kwa kuendelea kudumisha huduma za jamii katika Nyanja ya Elimu,Afya,Barabara na Maji kwa mkoa wa Katavi na katika Kata hiyo kwa lengo la kusogeza Huduma Karibu na wananchi.

Katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwakani Mbunge Martha ametoa hamasa kwa Vijana na wanawake katika Kata za Stalike na Machimboni kujitokeza kwa wingi kuwania nafazi hizo ili kuweka msingi mzuri katika kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025

Akiwa katika ziara hiyo katika Kata za Machimboni na Stalike amewazesha wanawake wa UWT Kila Kata kiasi cha Shilingi Laki Tano na Kadi za UWT ili kuendelea kuingiza wanachama wengi zaidi kwenye.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 
kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages