DC: JAMILA ATOA SIKU 60 UKARABATI WA HOSPITALI UKAMILIKE


Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiwa katika ziara ya kukagua Ukarabati wa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda wakati akitoa majumuisho ya ziara hiyo kwa waandishi wa habari hospitali hapo

Na Paul Mathias,Mpanda

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila yusuph amemwagiza mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda kuhakikisha ukarabati wa Majengo,na Ujenzi wa Majengo Mapya Katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda unakamilika ifikakapo 30/10/2023.


Moja ya jengo jipya lililojengwa katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda ambalo mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amefika na kufanya ukaguzi

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila yusuph amemwagiza mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda kuhakikisha ukarabati wa Majengo,na Ujenzi wa Majengo Mapya Katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda unakamilika ifikakapo 30/10/2023.

Maelekezo kezo hayo ameyatoa alipotembelea hospitalini hapo kukagua mwenendo wa baadhi ya majengo unaoendelea kwenye hospitali hiyo  ambapo serikali imeleta fedha shilingi milioni 900 ili kukarabati miundo mbinu hiyo ya majengo ya hospitali ya Manispaa ya Mpanda.

‘’Nimwagize mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda kuhakikisha ujenzi huu unakamilika ifikapo tarehe 30/10/2023 ujenzi uwe umekamilika wodi zote ambazo zinajengwa ziwe zimekamilika na majengo mapya amabayo yanajengwa yawe yamekamilika’’ amsema Jamila yusuph mkuu wa wilaya ya Mpanda

Jengo la mionzi katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda likiwa katika hatua za mwisho kukamilika tayari kwa kuanza kufanya kazi

Katika hatua nyingine ameipongeza Serikali ya kwa kuleta fedha zaidi Milioni 900 kwaajili ya ukarabati wa Majengo ya hospitali hiyo pamoja na ujenzi wa Majengo mapya hali ambayo itasaidia upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Mpanda ameridhishwa na ukarabati wa hospitali hiyo na kuwaomba wasimamizi kuendelea kufanya kazi hiyo ili kumaliza ujenzi huo kwa wakati naili  huduma zianze kutolewa kwenye majengo  hayo.

Mganga mkuu wa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda Dk Paul Lughata akitoa taarifa ya mwenendo wa ukarabati wa Majengo ya Hospitali hiyo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph alipotembelea hospitali hiyo 

‘’tumetembelea tumeridhika na kazi ambayo imefanywa hapa bado sehemu chache ambazo zinaendelea na ukamilishaji wa vitu kama milango na maeneo machache ambayo yamebaki kwaajili ya ukamilishaji’’amesema Jamila yusuph  

Mkuu wa wilaya ya Mpanda ametoa rai kwa wafanyakazi wa Hospitali hiyo kuendelea kuwahudumia Wagojwa kwa weledi kwakuwa serikali inaendelea kuboresha miundo mbinu ya sekta ya afya kwa Vitendo.

Mganga mkuu wa Hospitali ya Manispaa ya Mpanda Dk Paul Lugatha amesema majengo yaliyo kalabatiwa ni ukalabati wa jengo la wanawake [wodi ya upasuaji] ambalo limetengewa Milioni 54,ukarabati wa jengo la wanawake[Medical word ]iliyotengewa Milioni 56 ukarabati wa jengo la wanaume milioni 56 na jengo la wanaume la upasuaji lililotengewa  milioni 54

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph [kushoto]akiwa katika ukaguzi wa Majengo yanayokarabatiwa na kujengwa katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda

Dk Lugatha amesema kuwa majengo mengine yanayoendelea kukarabatiwa wa Wodi ya watoto iliyotengewa milioni 66 jingine ni ukarabati wa Jengo la Bima lilitengewa zaidi ya Milioni 5.

Onolata Mgawe mkazi wa Manispaa ya Mpanda ameishukuru serikali kwa kuona umuhimu wa kufanya ukarabati wa hospitali hiyo ili wananchi wapate huduma katika mazingira mazuri.

''kunamabadiliko Makubwa sana sasa hivi ukarabati huu wa Majengo haya hata kama unamgojwa ukimfikisha hapa anajihisi kupona amsema'' Onolata.

Ukarabati wa Baadhi ya Majengo katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda pamoja na majengo mengine mapya umeanza  Mwezi wa Pili mwaka huu na unaendelea vizuri majengo mengi yamesha kamilika na hatua zinazo endelea ni umaliziaji wa kawaida wa Majengo hayo katika ujenzi na ukarabati huo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages