MADIWANI TANGANYIKA WACHARUKA FEDHA ZA MIRADI KUCHELEWA KUTOLEWA

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.

Na Paul Mathias,Tangayika 

Baadhi ya Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameiomba halmashauri hiyo kujenga choo cha Kudumu katika Mnada wa Kata ya Mnyagala ambao hukutanisha watu wengi na kusaidia halmashauri hiyo kupata Mapato.

Halima Kitumba kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika akitoa ufafanuzi wa Hoja mbalimbali zilizoibuliwa na Madiwani katika kikao hicho

Baadhi ya Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameiomba halmashauri hiyo kujenga choo cha Kudumu katika Mnada wa Kata ya Mnyagala ambao hukutanisha watu wengi na kusaidia halmashauri hiyo kupata Mapato.

Wakizungumnza katika kikao cha Baraza la madiwani Madiwani hao wamesema kuwa halmashauri imekuwa ikikusanya Mapato kupitia Mnada huo hivyo ni wakati sasa wa kuona umuhimu wa Kujenga miundombinu ya Choo katika mnada huo.

Watumishi na wakuu wa Idara Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani

Diwani wa Kata hiyo Mathias Nyanda amesema ''choo mnategemea bajeti na huku manaendelea kukusanya Mapato kama ni hivyo tusitishe au tuufunge kabisa  mnada huu mpaka pale halmashauri itakapo pata fedha kwaajili ya kujenga mradi wa choo kwenye mnada huu'' amsema Diwani Nyanda.

Pamoja na hayo diwani huyo amasema kuwa kutokana na Msongamano wa wawatu katika mnada huo kutokuwa na huduma ya choo kunaweza kusabisha Magojwa ya Mripuko kwa wananchi.

Amina Lubwe Diwani wa Viti maalumu katika Kata ya Mnyagala amesema kuwa halmashauri imekuwa ikikusanya ushuru katika mnada huo ambao hufanyika mara mbili kwa mwezi hivyo ni mhimu halmashauri kuchukua jitihada za haraka kujenga miundo mbinu hiyo ya choo.

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika pamoja na wakuu wa idara na watumishi wakiwa katika kikao hicho

‘’mnada huu upo katikati ya wananchi na kuna visima vya mikono vya kutekea maji tunaomba halmashauri angalau iangalie fungu lolote linaloweza kupeleka miundo mbunu ya choo kwenye mnada huu'' amesema Diwani huyo Amina Lubwe.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Halima Kitumba amesema kuwa halmashauri itafanya kila linalowezekana na kuchukua hatua za kujenga Miundombinu ya choo katika mnada huo ili wananchi waendelee kufanya kazi zao vizuri na halmashauri iendelee kupata Mapato.

’Niwaahidi watoa hoja ofisi ya Mkurugenzi itakwenda kujenga miundombinu hii kwa haraka iwezekenavyo ili wananchi wapate huduma katika mazingira salama na sisi halmashauri tuendelee kukusanya mapato’’ amesema Kaimu Mkurugenzi huyo Halima Kitumba.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Philmoni Molo [katikati]akiongoza kikao hicho

Philimon  molo makamu mwenyekiti wa Halmashauri na mwenyekiti wa Kikao hicho ameiomba ofisi ya mkurugenzi kutafuta fedha ya Dhalula ili kufanikisha ujenzi wa miundombinu hiyo kwakiuwa maeneo yenye mikusanyiko kama minada hujumuisha watu wengi.

’Mkurugenzi hamwezi kukushidwa kutafuta fedha ya dhalula kwaajili ya ujenzi wa matundu mawili ya vyoo kwenye mnada huuamesema ‘’Makamu mwenyekiti huyo wa Halmshauri hiyo.

Diwani wa Kata ya Tongwe Frank Kibigas amehoji kuwa kuna kigugumizi gani kwa halamsahuri kutopeleka fedha za miradi katika kijiji cha Ngoma Lusambo ambapo tangu 2017 kunaboma la zahanati ambalo wananchi wamejitolea kulijenga.

’Mh mweyekiti hivi shida ni nini kutopeleka fedha kwa wananchi hawa wa Kijiji cha Ngoma lusambo wananchi hawa wanapata shida tuwaonee huruma’’ alisema Diwani huyo

Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Tanganyika Yasin Kibiriti wakati akitoa neno kwa niaba ya chama katika Baraza hilo amesema halmashauri nivyema kutafuta fedha ya dhalula ili kuhakikisha miradi ambayo haijapatiwa fedha ipelekewe fedha.

‘’Sisi kama chama kazi yetu ni kushauri niishauri ofisi ya mkurugenzi kutafuta fedha ya dharula ili miradi iliyolalamikiwa na waheshimiwa madiwani ipelekewe fedha huko ndipo walipo wapiga kura wetu wa CCM’’ amesema kibiriti

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages