DC :JAMILA ''HATUTA WAVUMILIA WANAO VAMIA VYANZO VYA MAJI''

 

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akizungumza na wananchi wa Kata ya kasokola katika mkutano wa hadhara.

Na Paul Mathias,Mpanda.

Serikali katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imesema haitasita kuchukua sheria kali kwa walewote watakaobainika kuavamia maeneo ya vyanzo vya maji na kuyafanyia shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo na ufugaji.

wananchi wa Kata ya Kasokola wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph kwenye mkutano wa hadhara kijijini hapo. 

Serikali katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imesema haitasita kuchukua sheria kali kwa walewote watakaobainika kuvamia maeneo ya vyanzo vya maji na kuyafanyia shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo na ufugaji.

Onyo hilo limetolewa na mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph wakati akizungumnza na wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kasokola Manispaa ya Mpanda mkoa wa Katavi.

Amesema kuwa kuna taarifa kwa baaddhi ya wananchi katika Kijiji hicho wameanza kufanya kazi za kilimo na ufugaji katika chanzo cha Maji Manga ambacho ni chanzo kikubwa cha maji katika Manispaa ya Mpanda na kuwataka kuondoka mara moja kwenye chanzo hicho cha maji.

Diwani wa Kata ya Kasokola Chrisant Mwanawima akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara baina ya mkuu wa Wilaya na wanachi wa Kasokola 

Jamila Yusuph anasema ‘’zilemita 60 zilizowekwa tuziheshimu tuzilinde kama maisha yetu sote tupo hapa tunakitunza na kukilinda chanzo hiki,ndugu zangu msilime ndani ya mita 60 walamsifanye shughuli yeyoteya kibinadamu ndani ya mita 60 kwenye mto au kwenye chanzo msifanye shughuli yeyote iwe kilimo au ufugaji eneo hilo limehifadhiwa kwa mujibu wa Sheria.

Amessitiza kuwa serikali haitakuwa na msaliamtume kwa yeyote atakae bainika kunfanya kazi katika chanzo cha Maji Manga kwakuwa chanzo hicho nitegemeo kubwa katika mradi wa maji wa Miji 28 ambao utakuwa muarobaini wa upatikanaji wa maji katika Manispaa ya Mpanda.

Waliovamia kwenye chanzo hiki cha Manga watupishe haraka kwani  chanzo hiki ni mhimu sana kwakuwa utasaidia upatikajaji wa Maji kuptia mradi wa Miji 28 kutokea bwawa la milala ambao unatekelezwa kwa zaidi ya Bilioni 22 amesema Jamila yusuph Mkuu wa Wilaya ya Mpanda.

Wananchi wa Kata ya Kasokola wakiwa katika utulivu wakati wa mkutano huo baina yao na mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya ameuagiza uongozi wa Bonde la ziwa Rukwa ndani ya siku saba aweamepata taarifa za uhalibifu wa cghanzo hicho cha Manga na hatua zichuliwe kwa wahusika kwa mujibu wa sheria.

‘’watu wa Bonde mnakisimamia hiki chanzo wananchi wamesema hapa chanzo kimevamiwa kuna watu wanakata mkaa mifugo inangia kule nanyie watu wa Bonde nawapa siku saba mnipe taarifa mmefanya nini juu ya uharibifu huu ulioelezwa wa chanzo hicho cha Maji amesema mkuu huyo wa Wilaya ya Mpanda Jamila yusuph.

Paul Ilesha mkazi wa Kijiji cha Kasokola amesema amemshuru mkuu wa wilaya kwa kuja na kutoa maagizo kwa wale waliovamia chanzo cha Maji Manga waondoke.

Thadeus Ndeseiyo afisa maendeleo ya Jamii kutoka Bodi ya Maji Bonde la Mto Ziwa Rukwa akitoa elimu kwa wananchi wa Kasokola juu ya umuhimu wa kutunza vyanzo vya Maji

’ujio huu wa mkuu wa Wilaya tunasubiria utekelezaji maagizo yake yatekelezwe ili kunusuru chanzo chetu cha maji watu wanaolima na kunyweshea mifugo yao waondolewe amesema Paul Ilesha mkazi wa Kasokola

Kwa upande wake Afisa maendeleo kutoka bonde Ziwa Thadeus Ndeseiyo amewaomba wananchi hao kuwa walinzi wa chanzo hicho cha Maji kwakuwa maji ni uhai.

Ndeseiyo anasema ‘’Ukikiingilia tu hiki kidaka maji cha Manga vilevisima tulivyo chimbiwa na serikali vinakauka kwahiyo tunapovamia chanzo hiki tutakosa maji lazima kila mtu awe mlinzi wa mwenzake kukilinda na kutoa taarifa za uhalibifu wa chanzo hiki.

wananchi wa Kasokola wakiwa katika mkutano wa hadhara baina yao na mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila yusuph 

Kikao hicho kupitia mkutano wa hadhara baina ya mkuu wa Wilaya ya Mpanda na wananachi wa Kata ya Kasokola kilikuwa na lengo la kusikiliza changamoto na kero mbalimbali za wananchi katika Kata yao. 

kwahabari zaidi endelea tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages