Makamu Mwenyekiti wa Halamshauri ya Wilaya ya Mlele Alphonce Kiyungi akiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani |
Na Paul Mathias,Mlele.
Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamemuomba mkandarasi anaesambaza umeme Vijijini kufikisha huduma ya umeme katika Kituo cha afya Ilunde ili wananchi wapate huduma kwa wakati.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani |
Baraza la Madiwani katika halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamemuomba mkandarasi anaesambaza umeme Vijijini kufikisha kwa haraka huduma ya umeme katika Kituo cha afya Ilunde ili wananchi wapate huduma kwa wakati.
Madiwani hao wameyabainisha
hayo wakati wakichangia taarifa za taasisi katika kikao cha Baraza la Madiwani
kilichofanyika Katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri hiyo.
Diwani wa Kata ya Ilunde Maltin
Mgoloka amesema serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan imelefedha na kujengwa
kwa Kituo cha Afya Ilunde lakini huduma ya umeme bado haujafika kwenye Kituo
hicho.
Watumishi na wakuu wa Idara Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani. |
‘’tunaendelea kupoteza wananchi Ilunde
serikali ya Dk Samia imetupa fedha tukajenga kituo
kikubwa cha Afya na sasa tunapokea vifaa ikiwemo Jokofu la Damu Salama
tunachumba cha upasuaji lakini vyote hivi havifanyi kazi sababu hatuna umeme na
juzi kuna mama amefariki dunia kwa ukosefu wa damu lakini umeme ungekuepo
asinge poteza maisha mama Yule amesema ‘’Mgoloka
Kwa upande wake Diwani wa Kata
ya Nsekwa Eligius Malando amesema kuwa kituo cha afya Ilunde kimekamilika kwa muda
sasa lakini kukosekana kwa huduma ya umeme ni tatizo kwani kuna vifaa
vinahitaji nishati ya umeme ili vifanye kazi.
‘’tuombe sasa umeme huu ufike
pale kituo cha afya Ilunde haraka kwani kuna vifaa tiba vinahitaji umeme ili
kufanya kazi kuchelewa kufika kwa umeme kuna fanya utoaji wa huduma kutokuwa ya
ufanisi’’ amesema Diwani Malando.
Kaimu Meneja wa Shrikala la Umeme Tanesco Wilaya ya Mlele Hussein Mzanva akijibu hoja mbalimbali zinazohusu umeme zilizoibuka kwenye kikao hicho. |
‘’mradi wa Grid ya taifa
nimradi mkubwa wenye gharama kubwa lakini katika taarifa hii inaonekana mradi
huu utakamilika lakini sioni kama kuna dalili ya kukamilika kwa mradi huu
kutoka Tabora hadi hapa mkoa wetu wa Katavi ameeleza ‘’Diwani Bundala
Hussein Mzanva Kaimu meneja wa
Shirika la umenme Wilaya ya Mlele amesema hadi kufikia mwezi wa kumi na moja wanatarajia
kuwasha umeme katika Kata ya Ilunde na kijiji cha Isegenezya.
Diwani wa Kata ya Utende Deus Bundala akitoa hoja katika kikoa hicho. |
Kuhusu ujenzi wa Mradi wa umeme
Grid ya Taifa kutoka Tabora amesema kuwa katika siku za hivi karibuni kulikuwa
na tatizo la kibajeti na fedha ilikuwa inatoka kwa awamu kwaajili ya kuendelea
na mradi huo na tayari wameongezewa muda wa miezi nane ili kukamilisha Ujenzi
huo.
Baadhi ya Viongozi wa Vijiji na Kata Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wakisaini Sheria ndogo za Vijiji zilizopitishwa na Baraza hilo kutumika katika Vijiji vya Halmashauri hiyo. |