HIFADHI YA KATAVI KUNUFAIKA NA HOTELI MPYA YA HOME GROUND

Naibu waziri wa Mali asili na Utalii Mary Masanja akiizindua  Rasimi Hotel ya Home Ground iliyopo mkoa wa Katavi.

 Na Walter Mguluchuma,Katavi

Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambayo ni  moja ya Hifadhi tano kubwa hapa   nchini  itanufaika  na Hoteli   Mpya ya Kitalii na yakisasa yenye uwezo wa  vyumba vya kulala viongozi  inayoitwa Home Ground ambayoitasaidia  kukuza mtandao  wa utalii katika eneo la huduma  na  malazi kwa watalii wanaokuja  nchini .

Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii Mary Masanja katikati akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama serikali na wabunge baada ya kuzindua hotel ya Home Ground inayomilikiwa na Mzawa kutoka mkoa wa Katavi Kelvin Mbogo.

Hifadhi ya Taifa ya Katavi ambayo ni  moja ya Hifadhi tano kubwa hapa   nchini  itanufaika  na Hoteli   Mpya ya Kitalii na yakisasa yenye uwezo wa  vyumba vya kulala viongozi  inayoitwa Home Ground ambayoitasaidia  kukuza mtandao  wa utalii katika eneo la huduma  na  malazi kwa watalii wanaokuja  nchini .

Hoteli hiyo ya  nyota tatu ya kwanza katika  Mkoa wa  Katavi iliko  katika   Mtaa wa  Ilembo  Manispaa ya  Mpanda imefunguliwa na  Naibu  Waziri  Maliasili na  Utalii Mary  Masanja  aliyekuwa mgeni rasmi  kwenye  ufunguzi huo .

Katika hotuba yake ya ufunguzi Naibu  Waziri wa Maliasili na Utalii amesema  hoteli hiyo ya kitalii ya   Home  Ground  kufunguliwa kwake itasaidia  kukuza    mtandao wa watalii wanaokuja    nchini  kutembelea hifadhi ya Taifa ya Katavi katika  eneo la  huduma na malazi .

Naibu  Waziri wa Maliasili na Utalii  Mary  Masanja akisalimiana na  Mkurugenzi wa  hoteli ya kitalii ya nyota  tatu  Kevini  Mbogo muda  mfupi  kabla ya uzinduzi wa hoteli hiyo iliyoko katika   Mtaa wa Ilembo  Manispaa ya Mpanda

Amebainisha kuwa  uwekezaji wa hoteli hiyo  Hifadhi ya Taifa ya Katavi  ambayo ni moja ya hifadhi   kati ya hifadhi  kubwa tano  za hapa  nchini  ambayo  inaukubwa   wenye kilometa za mrada  4,471  kuwa na uhakika wa malazi  ambayo mtalii yoyote au viongozi wa kiserikali kuweza kupata huduma hapo .

Masanja  alisema kuwa  uzinduzi wa hoteli hiyo ni  mwendelezo wa  ushirikiano wa Sekta  binafusi na Serikali  katika utoaji wa huduma za maradhi hapa nchini  na  pia  linaunga mkono  juhudi za  dhati  za  Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan  kama alivyoelekeza  katika filamu ya   The  Royal Tour.

Ameipogeza  kampuni ya    Home  Ground   kwa uwekezaji huo mkubwa walioufanya  hali  ambayo  imefanya kuwepo na ongezeko  na huduma  za malazi  zikiwa zmeomgezeka katika Mkoa wa Katavi na hapa nchini .

Mwenyekiti wa  Bodi  ya  Hoteli ya  Hoteli ya Home  ya  Grrond  Williy  Mbongo akielezea kuwa  hoteli hiyo ilifunguliwa inanyumba 38 kati ya vyumba hivyo  vitano  ni   vya uwezo wa kulala viongozi wa Kiserikali

Amewahakikishia  wawekezaji hao na wawekezaji wengine kuwa  Serikali  itazidi kuweka mazingira mazuri  wezeshi  ili kudumisha  ushirikiano  katika kukuza  na kuongeza  idadi ya  watalii wanaofika katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi inayosifika kwa kuwa na wanyama wakubwa kuliko hifadhi nyingine  akiwepo na twiga mweupe .

Naibu  Waziri  Masanja ameisisitiza  bodi ya wakurugenzi wa Hoteli hiyo kuhakikisha wanatowa huduma  zuri kwa wateja kuanzia kwenye mapokezi pindi  mgeni  anapokuwa amefika hapo  ili waweze kuendelea kupata wageni zaidi .

Kwa  upande wake   Mwenyekiti wa Bodi ya  hoteli ya Home  Gground Willy  Mbogo  alisema kuwa ujenzi wa hoteli hiyo ya kitalii  ilianza kujengwa   toka mwaka 2019 na  mpaka sasa   imefikia  asilimia 95  na imegharimu kiasi cha  shilingi Bilioni  3.5 na ikikamilika sehemu ya ukumbi  itakuwa imegharimu kiasi cha  shilingi Bilioni 4.

Amesema  hoteli hiyo  inavyumba  38  ambapo  katika  ya vyumba hivyo   vyumba  vitano   vinahadhi ya kulala viongozi wa Kiserikali  amewaomba  wadau mbalimbali kutowa ushirikiano  kwenye hoteli hiyo  yenye   hadhi ya nyota tano .

Aidha  Mbogo  ameiomba  Serikali  kuboresha  mazingira  ya miundo mbinu   ndani ya  Hifadhi ya Taifa ya Katavi  pamoja na kuweka mazingira   rafiki  ya wawekezaji ndani ya hifadhi nan je ya hifadhi ya Taifa ya Katavi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages