WATOTO 45 (DAMU CHAFU) WANAOJIHUSISHA NA UHALIFU WAKAMATWA KATAVI

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani.

Na Walter Mguluchuma, Katavi .

Jeshi  la Polisi  Mkoa wa Katavi limefanikiwa kuwakamata watoto 45(DAMU CHAFU) ambao wamekuwa wakijihusisha kufanya matendo mbalimbali ya uhalifu katika  maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Mpanda na kupelekea   kuwafanya wananchi wa  Manispaa ya Mpanda kuhofia hali ya usalama wao.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster  Ngonyani  amewaambia wandishi wa  Habari damu  chafu hao wamekamatwa kufatia msako   mkali ulifanywa na jeshi la Polisi kufatia kuwa kumejitokeza matukio mbalimbali ya uhalifu katika  Mji wa Manispaa ya Mpanda .

Alisema  jeshi hilo limekamata  Damu chao  45 wenye umri wa kuanzia  miaka kumi na moja   mpaka miaka 17 ambao waliweza kukamatwa na kushikiliwa na polisi  katika watoto hao waliowakamata waliweza kusaidia  jeshi hilo kuweza kuwapata  vijana wengine wahalifu  wenye umri kati ya miaka 18   hadi  miaka 24.

Amebainisha kuwa    vijana hao kumi na nane waliotajwa na damu chafu kushirikiana nao kufanya  vitendo vya  uhalifu wamekiri kujihusisha na vitendo hivyo vya yhalifu  kwamba ni kweli wanafanya vitendo hivyo   katika maeneo mbalimbali  yanayozunguka  mji wa  Mpanda .

Kamanda Ngonyani  alieleza  kuwa  katika hao vijana     kumi na nane waliokamatwa  wameweza nao kuwataja watu wengine  ambao  bado wanaendelea  kusakwa na jeshi la polisi  ambao ni wakubwa na wengine  kati yao wakiwa wametoka gerezani  hivi  karibuni  kwa  msahamu  uliotolewa  mwezi Aprili  mwaka huu.

Kati yao  wawili walikuwa wamemaliza  vifungo vyao na  mmoja wameweza kumkamata  na  mmoja  ambae amekuwa akihusika na matukio   bado wanaendelea kumtafuta kwani  yeye ndio  amekuwa akifanya matukio makubwa makubwa kwani wao damu  chafu wao wamekuwa wakijihusisha na matukio madogo  madogo .

Alisema  baada ya kukamatwa kwa  damu chafu 45  jeshi hilo  liliungana na ofisi ya  Ustawi wa Jamii   Manispaa ya Mpanda na waliweza kukaa na wazazi wa watoto hao  na wailiweza kuwapeleka Mahakamani na kupewa kibali na Mahakama  kwamba watoto hao watakuwa wanaripoti kituo cha polisi  baada  ya muda wao wa masomo kuwa umekwisha saa kumi na mbili jioni kila siku .

Amefafanua kuwa  wananchi wa  Manispaa ya  Mpanda waondokane  na hiyo taaruki ya kudhani matukio yote yanafanywa na damu chafu  matukio  makubwa yanafanywa na watu wazimu wao damu chafu ni watoto wadogo  na ndio wamewasaidia kuwapata hao walifu 18 wakubwa  na wameisha wapeleka Mahakamani kwa matukio  waliyokuwa wameyafanya .

Na  kwa kukamatwa kwa watu hao jeshi la polisi  limewezakufanikiwa  kukamata vitu vingi  kwa hao wahalifu wenye umri wa zaidi ya miaka 18 na  kuendelea    baadhi ya maeneo waliweza kufa wizi huo wa  viti ni kwenye eneo la Mtaa wa Ilembo  na  wameweza kuwakabidhi wahusika wa mali hizo  walizokuwa wakizipora kwa kuwakata watu kwa mapanga .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages