KATAVI YAPATA “CLEANSHEET” MWENGE WA UHURU.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2023,Abdallah Shaib Kaim akizungumza wakati wa makabidhiano ya Mwenge huo katika ya Mkoa wa Katavi na Rukwa yaliyofanyika leo katika Kijiji cha Kizi wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa.

Na George Mwigulu,Katavi.

MKOA wa Katavi baada ya kutembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2023 kwa siku 5 katika halmashauri za wilaya ya Tanganyika,Mpanda,Nsimbo,Mlele na Mpimbwe na kukimbizwa kwa zaidi ya Km 885 umeweza kufikia jumla ya miradi 40 yenye thamani ya fedha zaidi ya Bilioni Tano.

Kaimu  Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Majid Mwanga akimpatia zawadi mmoja wa kimbiza mwenge wa uhuru  Kitaifa baada ya kuimba mwimbo mzuri uliowafurahisha mamia ya watu waliohudhuria katika makabidhiano ya mwenge huo.

Mwenge huo ukiwa katika halmashauri hizo tano  umezindua miradi 22,umeweka mawe ya msingi katika miradi 8 na kukabidhi misaada,kutembelea miradi 10.ambapo baadhi ya miradi hiyo ni ujenzi wa barabara za kiwango cha lami,Zahanati na Vituo vya afya,Ujenzi wa miundombinu ya maji safi na salama na upandaji wa miti.

Akizungumza leo wakati wa makabidhiano kati ya Mkoa wa Katavi na Rukwa ya Mwenge wa Uhuru,Kiongozi wa Mbio za Mwege wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023,Abdallah Shaib Kaim amesema kuwa usimamizi bora wa ujenzi wa miradi hiyo unaonesha uimara na mshikamano na uwajibikaji wa viongozi wa wilaya ya Mkoa.

Kiongozi huyo ameeleza kuwa ujenzi wa miradi hiyo ni kichoche cha ukuaji wa shughuri mbalimbali za uchumi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Majid Mwanga akitoa taarifa ya mbio za mwenge wa uhuru zilizofanyika Mkoani hapa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Majid Mwanga akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sixtus Mapunda.

“Tunapongeza Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko kwa kuwa mama bingwa tunaamini kazi kubwa ambayo tumeiona ndani ya mkoa wake ni kwa sababu ya usimamizi shupavu wa weledi na umahili wake…tunaomba tufikishie salama zetu” Amesema Kaim.

Aidha,Atupokile Elia Mhalila Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa ameipongeza serikali ya mkoa wa Katavi kwa usimamizi bora wa ujenzi wa miradi ya maendeleo kwani wamejenga imani kubwa kwa rais Samia Suluhu Hassain kwamba hakukosea kuwateua kumsaidia kufanya kazi.

“Mkoa wa Katavi mmepata Cleansheet kwenye miradi yenu,haikuwa kazi rahisi hata kidogo ndani ya halmashauri tano kufanya vizuri kwenye ujenzi wa miradi ya maendeleo kwa kufanikiwa kuzinduliwa yote na kuwekewa mawe ya msingi bila hata mradi mmoja kukwama” Amesema Atupokile.

Baadhi ya watumishi wa Mkoa wa Katavi na wakimbiza mwenge wa uhuru wa Mkoa huo waliohudhuria wakati wa makabidhiano ya mwenge huo kati ya Mkoa wa Katavi na Rukwa.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Majid Mwanga akitoa taarifa kwa niamba ya Mkuu wa Mkoa huo Mwanamvua Mrindoko  wakati wa makabidhiano wa Mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Kizi Wilaya Nkasi Mkoani Rukwa amesema wanatambua falsafa ya  mwenge wa uhuru ni kuchochea maendeleo,umoja na amani katika taifa.

Mwaga amesema Mkoa wa Katavi kwa kuzingatia jitihada za kutekeleza ujumbe wa mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2023 ambao unasema Tunza Mazingira,Okoa Vyanzo vya Maji  kwa ustawi wa viumbe hai kwa uchumi wa taifa.

Ameeleza kuwa mkoa huo kupitia kupitia Halmashauri za Wilaya ya Tanganyika,Mpanda,Nsimbo,Mlele,Mpimbwe na kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo na uhifadhi wa mazingira wamefanikiwa kupand zaidi ya miche Mil 7 imepandwa kwenye maeneo mbalimbali ya mkoa.

Baadhi ya viongozi wa dini kutoka Mkoa wa Katavi waliohudhuria makabidhiano ya mwenge wa uhuru kati ya Mkoa wa Katavi na Rukwa. 

Baadhi ya asikali kutoka Mkoa wa Katavi waliohudhuria wakati wa makabidhiano ya mwenge wa uhuru kati ya Mkoa wa Katavi na Rukwa,

Aidha katika kuhakikisha vyanzo vya maji vinahifadhiwa,Mkoa wa Katavi umefanikiwa kutambua jumla ya vyanzo vya maji 102 ikiwamo mito na vijito ambapo serikali ya Mkoa kupitia halmashauri na wadau wa uhifadhi wa mazingira wamefanya juhudi za kuvilinda.

Katika kuhakikisha suala la upandaji miti na utunzaji wa mazingira linakuwa la kudumu,Mkoa mefanikiwa kuwa na mkakati wa upandaji miti na uhifadhi wa vyanzo vya maji ili kuweza kufanikisha lengo la kuongeza  kasi ya ushiriki wa jamii kwenye upandaji miti.

Kaimu Mkuu wa Mkoa huyo amesema baadhi ya malengo ni kuhifadhi vyanzo vya maji kwa kushirikiana na jamii,kuzuia uharibifu wa misitu,kuruhusu urejeshwaji wa uoto kwa njia asili,kuhamasisha upandaji miti na kuhamasisha jamii kwenye utunzaji na usafi wa mazingira.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages