WANANCHI WILAYA YA TANGANYIKA WACHANGISHANA FEDHA ILI KUWABAINI WACHAWI.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani 


Na Walter Mguluchuma,Katavi

Katika  hali isiyo ya   kawaida  wananchi wa  Tarafa ya Karema  mwambao mwa ziwa  Tanganyika  Wilaya ya Tanganyika  Mkoa wa Katavi wamechangishana fedha kwa ajiri ya  kumpeleka  mganga wa kienyeji(Kamchape] ili  afike  kijijini hapo kuweza kufanya kazi ya kuwabaini na kuwatambua watu wanao daiwa kuwa ni washirikina(wachawi)

Katika  hali isiyo ya   kawaida  wananchi wa  Tarafa ya Karema  mwambao mwa ziwa  Tanganyika  Wilaya ya Tanganyika  Mkoa wa Katavi wamechangishana fedha kwa ajiri ya  kumpeleka  mganga wa kienyeji(Kamchape]  ili  afike  kijijini hapo kuweza kufanya kazi ya kuwabaini na kuwatambua watu wanao daiwa kuwa ni washirikina(wachawi)

Baadhi ya wananchi  hao wamesema kuwa  ni  kweli wameamua kuchangishana  fedha za kumleta  mganga wa kienyeji  anaeitwa  Kamchape ili aweze kuwatambua watu ambae wamekuwa wakijihusisha na maswala ya  ushirikina  kwenye  kijiji cha  Karema .

Mmoja wa wakazi wa  Kijiji  hicho  aliyejitambulisha kwa jina moja la  Boki amesema swala hilo kwa hapo  kijiji la kuchanga fedha kwa ajiri ya  kumleta   kamchape  limeungwa mkono na watu wengi wa Kijiji hicho  licha ya kuwa anavyotambua yeye  swala hilo  Serikali  imeisha piga marufuku .

Amebainisha kuwa karibu  asilimia    tisini ya wananchi wa Kijiji cha Karema  husani   vijana wanaunga mkono kwa  asilimia mia  mganga huyo  kamchape  afike  kijijini hapo ili  aweze  kuwabaini watu wote kwenye   kijiji cha Karema  ambao wanajihusisha na  maswala ya   ushirikina .

Nae  mkazi mwingine wa  Kijiji  hicho ambae hataka jina  lake litajwe   alisema  wanalazimika kuchanga  mchango huo  ambao hadi sasa kuna zaidi ya shilingi laki tano  kwani  endapo  hutaonekana wewe hutaki  kuchangia jamii itakuchukulia kuwa na wewe ni  mshirikina ndio maana unaogopa kamchape  asifike  kijijini hapo .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani amesema hapo  siku za nyuma watu hao wanaojiita  kamchape wanaodai  kuwa wanatambua wachawi walikuwa  kwenye Kata ya  Ikola   Tarafa ya Karema  hata hivyo jeshi la  polisi kwa kushirikiana na jeshi la wananchi waliweza kuwafukuza  kundi hilo la kamchape  kabla  hawajaanza kufanya kazi yao hiyo .

Kamanda   Ngonyani   amewaonya  watu hao kutofanya  shughuli hiyo kwani matokeo ya kazi hiyo ni kusababisha mauaji kwa watu wasio na hatia hivyo    watahakikisha wanawazuia kabisa  kamchape kufanya kazi hiyo  ambayo haina tofauti na   lamli  chonganishi ambayo imekuwa  ikikazwa  na jeshi hilo kwa nguvu zote.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages