UKOSEFU WA MAJI CHANZO WANAWAKE WAJAWAZITO KUPEWA KAZI YA KUTEKA MAJI.

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe ambapo alitoa wito kwa wauguzi kuacha tabia ya kuwapa majukumu wanawake ya kuchota maji pindi wanapokwenda katika vituo afya na zahanati za serikali  kujifungua.

George Mwigulu,Nsimbo.

Ukosefu wa maji safi salama kwa baadhi ya vituo vya afya na zahanati katika halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoa wa Katavi ni chanzo cha wanawake wajawazito wanaokwenda kujifungua kupewa jukuma la kuchota maji.

Baadhi ya wanawake wakitoa kero zao hivi karibuni kwa mbunge wa Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe wameeleza kuwa wanapopata uchungu na kwenda katika zahanati za serikali baada ya kujifungua na kabla hawajaruhusiwa kurudi nyumbani wanatakiwa kuchota ndoo tano za maji ikiwa kwa wakati huo hawajapata nguvu.

Mariam Sayi,Mkazi wa kijiji cha Uruwila amesema kuwa kitendo cha ukosefu wa miundombinu ya maji kwa baadhi ya zahanati za serikali kumekuwa kero kwao na kuwa adhabu.

“Sasa suala la kuzaa linaonekana kama adhabu kwetu,tunapitia mateso ambayo ni vigumu kwa kiongozi wa ngazi ya wilaya kufahamu hilo kwa kuwa wao wanaishi kwenye mazingira mazuri yenye maji ya kutosha” Amesema Mariam.

Hawa Lazaro anasema kuwa usubufu wanaoupata wa kuchota maji unawafanya baadhi ya wanawake kutokwenda kwenye vituo vya afya na zahati za serikali hivyo wanalazimika kusafiri umbali mrefu kwenda Manispaa ya Mpanda kujifungua na kusabisha gharama kubwa ya kifedha ambapo hawawezi kumudu.

Ameiomba serikali ya halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kuwaonea huruma kwani wanaoteseka zaidi ni wanawake wanao kwenda kwenye vituo vya afya na zahanati kujifungua.

Mtendaji wa Kata ya Uruwila,Revocatus Mapula amekiri kuwepo kwa kitendo cha wanawake kupewa majukumu ya kuchota maji lakini kwa sasa hakipo kutokana na kupiga marufuku Wauguzi wa afya kufanya hivyo.

“Nilimwita inchaji wa zahanati hiyo nikamwambia ni marafuku mama yeyote akijifungua wewe umwagize akachote maji…huko nyuma kweli lilikuwepo na kwa bahati nzuri kwenye kikao cha Isagala juzi tuliliongelea na kulitolea ufafanuzi na Mh Diwani akakemea hilo,sasa kama linaendelea tunaomba mtuletee ili tulishughulike Amesema Mapula.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Nsimbo,Mohamed  Ntandu anasema serikali inaendelea kufanya jitihada za kuhakikisha maji yanafika kwenye maeneo ya zahanati kwa kutumia mtandao wa RUWASA.

Anna Lupembe,Mbunge wa Jimbo la Nsimbo ametos wito kwa wauguzi wa afya kuzingatia maadili yao ya kazi wanapotoa huduma kwa wananchi pindi wanapokwenda katika  zahanati  kutafuta matibabu.

Lupembe amesema kuwa muuguzi ni karama ambayo wamepewa na Mungu na wanatakiwa kuwa na huruma kwa wananchi.

Vilevile amewaomba wananchi kuwa watulivu kwani serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya maji nchini na kama mbunge anaendelea kufanya juhudi za kuhakikisha maji safi yanapatikana.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages