MWENGE WA UHURU NSIMBO MKANDARASI ALEKEBISHE DOSARI.

 

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023,Abdallah Shaib Kaim akishuhudia hivi karibuni upimaji wa upana wa barabara ya Isinde Halmashauri ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi.



Na George Mwigulu,Nsimbo.

MWENGE wa Uhuru mwaka 2023 umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa barabara ya kiwango cha lami mita 745 wenye thamani ya zaidi ya fedha Mil 491 katika kijiji cha Isinde kata ya Mtapenda halmashauri ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi utakao hudumia jamii.

Abdallah Shaib Kaim,Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2023 akizungumza na wakati wa kijiji cha Isinde Kata ya Mtapenda wakati wa kuweka jiwe la msingi wa barabara hiyo yenye urefu wa Mita 745.

Barabara hiyo ni sehemu ya mtandao wa barabara wenye jumla ya urefu wa Km 511.18 za halmashauri ya  Nsimbo ambapo kati ya hizo ni Km 2.14 ni lami,Km 111.308 ni changarawe na Km 397.622 ni za udongo.

Akiweka jiwe la msingi leo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2023.Abdalla Shaib Kaim katika kijiji cha Isinde Kata ya Mtapenda amesema serikali kwa kutambua umuhimu wa miundombinu ya barabara nchini  imekuwa ikitoa fedha nyingi za kujenga barabara zitakazo chochea ukuaji wa maendeleo ya wananchi.

Kiongozi huyo wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuwa na nyaraka zote za ujenzi wa mradi wa barabara  na miradi mingine yote kutokuwa  na dosari yoyote.

Licha ya kuwapongeza na kuweka jiwe la msingi ametoa siku tano kwa uongozi wa halmashauri hiyo kufanya marekebisho ya barabara hiyo ya Mita 745 baada ya mwenge wa uhuru kubaini kuna mapungufu.

”Katika sehemu ambazo mwenge wa uhuru umebaini kuna chanamoto tunaagiza ndani ya siku 5,Na kwa kutambua mkandarasi bado yupo site aitwe aelekezwe na sehemu hiyo ifanyiwe marekebisho na baada ya kufanya marekebisho tunahitaji taarifa ya utekelezaj wa marekebisho pamoja na picha za kabla na baada na video wakati mkandarasi akiwa site ili kuona agizo lililotolewa na mwenge wa uhuru limetekelezwa kwa wakati ” Amesisitiza  Kaim.

Vilevile amemwomba Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Jamila Yusuph kwa kushirikiana kamati ya ulizi na usalama ya wilaya kuona kwamba kwa sehemu hiyo na maelekezo hayo wanawasimamia TARURA sambamba na kuhakikisha ujenzi wote na muda wa matazamio ya  mradi kuwa ubora na viwango wa ujenzi wa barabara umezingatiwa.

“Msisite popote kuchukua hatua mtakapo ona kuna changamoto wakati wa kipindi cha matazamio mhakikishe mnatoa maelekezo kwa ajili ya kurekebishwa mpaka  muda wa matazamio utakapokamilika kwani rais Samia Suluhu Hassain anatmia fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo ili wananchi waweze kufaidika” Amesema Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa.

Awali Meneja wa TARURA Wilaya ya Mpanda,Mhadisi Hoza Joseph akisoma taarifa ya mradi wa barabara hiyo mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa,Abdalla Shaib Kaim amesema kuwa mradi wa barabara ya Isinde uliibuliwa na Wakala wa barabara Vijijini na Mjini (TARURA) mwaka wa fedha 2022/23,ukiwa na lengo la uboreshaji na uimarishaji wa barabara katika mji wa Nsimbo.

Mhadisi Joseph amesema ujenzi wa barabara ya lami ulianza kutelekezwa Septemba,2022 na kukamilika Feb,2023 kwa hatua ya ujenzi wa lami nyepesi na mifereji yam awe  na kazi zilizobaki ni uwekaji wa alama za barabarani na usimikaji wa taa ambapo gharama ya ujenzi wa lami  ni zaidi ya fedha Mil 491.

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Isinde Kata ya Mtapenda kabla ya kuweka kwa jiwe la msingi wa barabara hiyo.

 

Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Mkoa wa Katavi,Anna Lupembe amesema kuwa serikali inafanya kazi kubwa ya kuhakikisha miradi mbalimbali ya maendeleo inajengwa katika Jimbo la Nsimbo  kama sehemu ya kuwahudumia wananchi.

Lupembe ameipongeza serikali kwa kuimarisha miundombinu ya barabara ambapo kwa sasa mtandao wa barabara za lami unaendelea kuimarika.

Aidha katika halmashauri ya Nsimbo  umekimbizwa Km 198 na kupitia jumla ya miradi 10 yenye thamani ya Fedha zaidi ya Mil 897.

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages