MWENGE WA UHURU WARIDHISHWA NA MIRADI WILAYA YA TANGANYIKA

 

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Majid Mwanga[kushoto] ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mlele akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu tayari kwa mwenge huo kuanza kukimbizwa katika Wilaya ya Tanganyika 

Na Paul Mathias,Tanganyika

Mwenge wa uhuru katika Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi imezindua miradi Saba yenye Thamani ya Shilingi Billion 1.5

Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Shaib Abdalla Kaim Mwenyekombati Nyekundu [Katikati] akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika

Mwenge wa uhuru katika Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi imezindua miradi Saba yenye Thamani ya Shilingi Billion 1.5

Akizungumza Kwa nyakati tofauti akiwa katika uzinduzi wa miradi hiyo katika Wilaya ya Tanganyika  kiongozi wa mbio za Mwenge  Kitaifa  Abdalla shaib kaim amesema ameridhishwa na miradi hiyo.

Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Tanganyika Eng Alkam Sabuni akitoa maelezo ya Mradi wa Maji Vikonge  katika mchoro kwa Kiongozi wa Mbioza Mwenge Kitaifa Abdall Shaib Kaim.

Miradi iliyozinduliwa ni pamoja na Mradi wa maji katika Kijiji Cha vikonge wenye thamani ya Shilingi Zaidi ya million 608 Ambao utawanufaisha wa wakazi zaidi ya 8400 kutoka Kijiji Cha vikonge pamoja na maeneo jirani .

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Abdalla Shaib Kaim [Kulia] akiwa katika picha ya Pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu[Kushoto] muda mchache baada ya kuzindua Mradi wa Maji Vikonge

Mradi mwingine uliozinduliwa Jengo la wagojwa wa nje OPD katika Kituo Cha Afya Sibwesa kilicho gharimu kiasi Cha Shilingi Million zaidi ya milioni  500 ambao utawasidia Wananchi wa Kata ya Sibwesa kupata Huduma za Afya pamoja na Huduma ya mama na Mtoto .

Kiongozi huyo wa mbio hizo za Mwenge amezindua Shule ya awali na MsingiNtikimo iliyotokana na Fedha za Mradi wa Boost ambapo Serikali imeleta zaidi ya Milioni 600 Kwaajili ya kufanikisha ujenzi huo wa Shule.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim akiwa katika ukaguzi wa Majengo ya shule ya Awali na MsingiNtikimo  Kijiji cha Kasekese kabla ya kuzindua Mradi huo

Mwenge huo wa uhuru umeweza kuzindua Mradi wa Vijana wa ufundi selemala cha Cha vijana Twiga Planing Fuaniture kilichopo Majalila ambacho kimewezeshwa na halmashauri Kupitia Mikopo ya Asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri wenye Thamani ya shilingi Milioni 3.

Baadhi ya wananchi katika Kijiji cha Sibwesa Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi walijitokeza kuulaki Mwenge wa uhuru ulifika kijijini hapo.

Katika kukabiliana na Tatizo la Rushwa na utunzaji wa mazingira Mwenge wa uhuru katika Wilaya ya Tanganyika umezidua Club ya Kupinga Rushwa katika Shule ya Sekondari Majalila pamoja na kuzindua Mradi wa upandaji miti katika Shule ya Sekondari Majalila pamoja na kuzindua Mradi wa lishe katika Shule hiyo.

Mwenge wa uhuru Kwa mwaka 2023 unaenda sambamba na kauli mbiu inayo Sema Tunza Mazingira okoa vyanzo vya Maji Kwa usitawi wa viumbe hai na uchumi wa taifa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages