RC MRINDOKO KATAVI IPO TAYARI KUWAPOKEA WANAFUNZI WOTE WA KIDATO CHA TANO.

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake.

Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Mkoa wa Katavi  umewahakikishia   wazazi wa wanafunzi  na Wanzania kwa ujumla kuwa wako tayari kuwapokea wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu kutokana na kuwa  miundombinu ya kutosha  ambayo imeisha  andaliwa na Mkoa wa Katavi .

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko wakati alipokuwa  akiongea na wandishi wa  habari  jinsi ambavyo  Mkoa huu ulivyojipanga kuhakikisha  hakuna  changamoto yoyote    ambayo   inayoweza kufanya       mwanafunzi  asiweze kuripoti shuleni .

Mrindoko  amebainisha kuwa wanafunzi waliofanya  mtihani wa kidato cha   nne  matokeo yake yameisha patikana  na  kutangwa mwezi Januari 2023 na  tayari  mipango ya kuwapangia kujiunga na kidato cha tano imefanyika  na kwa  Mkoa wa Katavi wamepangiwa kupokea  wanafunzi 2587 kwa ajiri ya kujiunga na  elimu ya kidato cha tano kwa shule zilipo katika Mkoa wa Katavi  katika shule  nane zilizopo  katika Mkoa wa Katavi .

 Kati ya wanafunzi hao wavulana ni 940 na wasichana  1,647 na wameanza kuripoti  toka  tarehe 13  Agosti  na   mpaka   leo Agosti  14 wanafunzi   269 wameisha ripoti  shuleni  na wanaendelea kufatila kama Mkoa kuhakikisha wanafunzi wote wanalipori .

Mrindoko amewawahakikishia   wazazi  ,walezi na wanzania kwa ujumla  na wanafunzi  kuwa wapo  tayari kuwapokea  wanafunzi wote hao kwa kuwa miundo mbinu yoye  imekamilika na ipo ya kutosha  kupokea wanafunzi zaidi     y ahata   ya hao walichaguliwa .

Ametowa wito kwa  wazazi  na walezi    wa watoto     wanaowalea  ambao wamechaguliwa  kujiunga na masomo kwenye shule zote nane zilizopo katika Mkoa wa Katavi  wahakikishe wanafanya utaratibu  utakaowawezesha wale wanafunzi   ambao hawajaripoti  waweze kuripoti mapema ili waweze kuungana  na wenzao  ambao wameanza masomo .

Mkoa  umeisha weka   utaratibu  mzuri wa   walimu wa kuwapokea kwa  muda wote wanakuwepo  na  namba zao za simu  zinakuwa wazi ili kuweza kutowa  huduma    kwa haraka zaidi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages