TAKUKURU KATAVI WATOWA ONYO KWA MATAPELI WANAOJIFANYA MAAFISA WA TAKUKURU

 

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi,Faustine Maijo.

Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Taasisi ya Kuzuia  na Kupambana  na  (TAKUKURU)  Mkoa wa Katavi   imewaonya watu wanaojifanya watapeli  watu  wanaowapigia watu simu  na kujitambulisha  kwao kuwa wao ni   maafisa wa Takukuru  waache  tabia  hiyo mara moja  kabla  hawajatiwa nguvuni .


Onyo hilo  limetolewa na  Mkuu wa  TAKUKURU  Mkoa wa  Katavi Faustine   Maijo wakati alipokuwa akitowa  taarifa ya utekelezaji wa  kazi katika kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia  Aprili   hadi June 2023.

Amebanisha kuwa  bado  kumekuwepo  na wimbi  linalioendelea  la  watu  matapeli  wanaojifanya  ni  maafisa wa Takukuru  ambao huwapigia watu simu kwa lengo la kuwatapeli  kuwa wao ni  maafisa wa Takukuru  na kuwataka waweze kuonana nao  kwa madai wao ni wahusika wa Taasisi hiyo ,

 Maijo  amewaonya  matapeli kuacha tabia  hiyo mara moja  kwani watambue kuwa kufanya hivyo ni kosa la  jinai na watakao  thubutu kujifanya  maafisa  wa  Taasisi    hiyo  watambue kuwa watakamatwa mara moja kwani wameisha jipanga  kukomesha  kabisa  katika  Mkoa wa Katavi  wimbi hilo .

Mkuu  huyo wa Takukuru  Mkoa wa  Katavi  ametowa   wito  na rai  kwa jamii na watumishi wa Mkoa wa Katavi  ambao  ikitokea  wamepigiwa simu na matapeli hao  watowe taarifa  kwenye  osifi ya  Takukuru  iliyokaribu nae kwa kupiga simu namba  113.

Amewataka watu wasikubali kutapeliwa na watu hao  bali  watowe taarifa mapema  Takukuru  ili   mhalifu au wahalifu  aweze kuchukuliwa hatua  za kisheria  mapema   kwani ni kosa la kisheria kujifanya    mtumishi wa TAKUKURU .

 Adha  alisema  Takukuru  Mkoa wa Katavi  wameendelea  na utekelezaji  wa  majukumu  yake  katika robo mwaka  kwa kipindi cha mwezi     A prili  hadi June 2023 mkazo uliwekwa  katika   elimu  ya kuhamasisha  wananchi  ili washiriki  kikamilifu  kuzuia    rushwa na  ufatiliaji wa fedha za miradi ya maendeleo  zilizotolewa na serikali  ikiwa  ni pamoja  na kufanyia kazi  maelekezo mbalimbali  yaliyotolewa na viongozi wa  nchi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages