Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi Faustine Maijo akizungumza na wanahabari leo katika ofisi za Taasisi hiyo. |
Na Walter Mguluchuma, Katavi.
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)Mkoa wa Katavi katika kipindi cha miezi mitatu imefatilia utekelezaji wa Miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 2.8 katika kipindi cha miezi mitatu kwenye sekta za Barabara , elimu na Afya.
Hayo amesema Mkuu wa Faustine Maijo wakati aliokuwa akitowa taarifa ya utekelezaji kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia mwezi Aprili hadi June ambapo sehemu kubwa walimejikita katika kushughulikia wazabuni waliosababisha kuchelewa ukamilishaji wa miradi ya Maendeleo kwenye Mkoa huu.
Amesema Takukuru Mkoa wa Katavi
katika kipindi hicho cha miezi mitatu imefatilia utekelezaji
wa miradi 11 yenye thamani ya shilingi Bilioni 2,831,493,083
katika sekta za barabara ,elimu na afya .
Maijo amebainisha kuwa kati ya miradi
miwili mradi mmoja unaendelea vizuri na miradi
nane inaendelea kufatiliwa kwa ukaribu kutokana
na mapangufu mbalimbali ikiwemo ucheleweshaji na
ubora wa miradi hiyo
Aidha wameweza kufanya chambuzi za
mifumo ikiwa lengo la kutaka kubaini mianya
ya Rushwa ambayoinaweza kupelekea vitendo vya
Rushwa kutokea na kutowa ushauri kwa taasisi husika
namna bora ya kurekebisha mapungufu yaliyobainika kwenye
chambuzi hizo .
Amebainisha kuwa kwa kipindi cha Aprili
hadi june 2023 Takukuru Mkoa wa
Katavi imefanya chambuzi saba za
mifumo kwenye sekta mbalimbali ikiwa ni
pamoja na ulinzi , vipimo mistu , maji , maji miradi ya
maendeleo masoko na mazingira katika Halmashauri
za Mpanda ,Mlele na Tanganyika .
Kuhusu uchunguzi wa mashitaka Takukuru Mkoa wa
Katavi wameendelea kupokea malalamiko yanayohusiana na
vitendo vya Rushwa ambapo wameweza
kupokea malalamiko 62 kati ya malalamiko hayo
taarifa za Rushwa ni 45 na zisizo za Rushwa
ni 17.
Maijo amesema katika kipindi cha
Julai hadi Septemba 2023 wataendelea kufatilia
kwa karibu frdha zote zinazotolewa na Serikali
ili kuhakikisha zinatumika kama ambavyo ilivyokusudiwa na
upande wa miradi kuwa na ubora kama thamani ya
fedha zinazolingana na thamani ya mradi.