Ni jiwe la msingi ambalo lilitumika kama ishara ya uzinduzi wa eneo la Maonesho ya Kilimo katika Kitongoji cha Ikulu Kijiji cha Kabungu Wilaya ya Tanganyika,Kibao cha maandishi kinadaiwa kuchukiliwa na wafungaji wa mifungo ambao hutumia eneo hilo kwa malisho-(Picha na George Mwigulu)
|
Na George Mwigulu,
Katavi.
Wazo la kupongezwa limeibuliwa mwaka 2019 na serikali ya Mkoa wa Katavi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa huo,Juma Zuberi Homera (Kwa sasa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya) ni kuanzisha eneo la maonesho ya kilimo (nane nane) ikiwa ni sehemu ya kutambua umuhimu wa historia ya kuanzishwa kwake nchini.
Hapa ni sehemu ya eneo la maonesho ya kilimo ya Mkoa wa Katavi ambapo limeota nyasi na miti mingi kwa sababu ya kutelekezwa kwa muda mrefu |
Maonesho ambayo yangebeba dhima kamili kwa wakulima wa Mkoa huo yanaoneka kutelekezwa licha ya faida yake ingekuwa kubwa
hasa wanawake na wasichana wangepata fursa ya kuona teknolojia mbalimbali za
uzalishaji,usindikaji na masoko pamoja na maarifa na taarifa za kilimo kutoka
ndani na nje ya nchi.
Mkoa wa Katavi ni wazi umeshindwa
kuzingatia hayo licha ya nia njema ya hapo awali walidhamilia kuanzisha eneo la maonesho ya kilimo licha ya kuwa
na maonesho ya kanda jijini Mbeya,Jambo ambalo wananchi wa Mkoa huo kwa muda
mrefu wamelipokea kwa furaha.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani kutoka ndani ya Halmashauri ya
Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi zinasema wananchi kuamua kutoa eneo la
hekari 240 katika kitongoji hicho ni sauti inayonesha uchungu wa kuhitaji
maendeleo na baadhi yao kuamua kutoa ardhi bure kwa serikali bila kudai fidia
licha ya kuwa watakosa eneo la uzalishaji kupitia kilimo.
Chanzo hicho kinasema njia
ya upatikanaji wa eneo hilo ni baada kupewa elimu na viongozi wa serikali ya
Mkoa naye kama kiongozi kwa kushirikiana na viongozi wengine wa ngazi ya kijiji
walifanya ushawishi kwa wananchi wote na kukubali.
“
wananchi baadhi yao walitoa bure ardhi na wengine findia ndogo ya Tsh 50.000/=,Tsh
100,000/=,Tsh 200,000/= na wachache ambao walilipwa kwa gharama kubwa kama Tsh
500,000/= kwa sababu walikuwa na nyumba za makazi” Kilibainisha chanzo hicho.
Kutelekezwa kwa mradi
huo umekuwa na athari kubwa kwa wananchi baada kuyaachia maeneo hayo na
kuhamishiwa kwenye maeneo mengine wakitengemea mradi utakapokamilika fursa ya
kukua kiuchumi kwao itapatikana.
“
Watu wamesubilia mradi huo kwa muda mrefu sasa na wamekata tamaa kiasi cha
kuuza ardhi zao na kuhama kwenda sehemu zingine ambako wanaweza kupata fursa za
kuongeza kipata chao”
Ameongeza hayo.
Madhara mengine wamepata
wananchi ni baada ya kuchimbwa mtalo mkubwa wa maji kutoka Kitongoji cha
Imalausinga hadi Ikulu ambako kutakuwa na eneo la maonesho ya kilimo.Mfereji
huo haujajengwa na kusababisha nyumba za makazi kuanguka kwa sababu ya kusambaa
maji kwa kasi wakati wa mvua.
“Tumepiga
kelele wee ule mtalo analeta maji kwa fosi,ukaleta mmomonyoko mkubwa wa udogo
hadi maji kuingia ndani ya nyumba za watu hata sasahivi tutakwenda kuona baadhi
maeno ya nyumba zilizoanguka”
Amesema bainisha hayo chanzo ambacho jina lake tunalo.
Baada ya kufika eneo hilo tumeonana na Anna Sukari,Mkazi wa
kitongoji cha Ikulu mama muhanga wa nyumba yake kuanguka kwa sababu ya mfereji
kuingiza maji kwa kasi ndani ya nyumba yake anasema “ maji yalikuwa ya kiingia hadi chumbani juu ya kitanda nikiwa nimelala
na watoto wangu”.
Mama huyo anaeleza
kuwa nyumba yake haikudumu kwa muda mrefu na kuaguka jambo ambalo lilimlazimu
kwenda kuomba hifadhi kwa majira zake huku taratibu baadaye alichukua hatua ya
kuanza kujenga nyumba nyingine mpya.
Amesema serikali ya
Mkoa wa Katavi inapaswa kuujenga mtalo kabla ya mvua za msimu wa kilimo ujao
kuanza kunyesha sambamba na kuhuwisha eneo la maonesho ya kilimo (nane nane)
kwani wanahisi uchugu kutoa maeneo yao bila kuendelezwa kwa lengo husika.
Mark Sylvester,Mkazi wa Kijiji cha Kabungu anasema serikali ya mkoa wazo lake ni jema na juhudi za awali zinaonyesha kwamba katika sekta ya kilimo wanakwenda kupiga hatua kwani maonesho ya kilimo ni fursa ya kujifunza.
Ni moja ya nyumba zilizoaguka kutokana na mtalo wa maji ambao haujajengwa katika kitongoji cha Ikulu Kijiji cha Kabungu. |
Anafafanua kuwa
juhudi zilioneka baada ya barabara kuchongwa mitaani,kupelekwa kwa huduma ya
umeme na maji safi na salama na baadhi ya taasisi kuanza kuchukua viwanja kwa
ajili ya uwekezaji kama vile Shirika la Kuwezesha Wakulima na
Wajasiliamali Katavi tangu mwaka 2021
wamejenga na kuendelea na kazi.
“Maeneo
mengine waliweka vibao vya kutambulisha taasisi hizo lakini vibao hivyo hakuna
hata kimoja kutokana na wafugaji wa mifungo kufanya eneo hilo la maonesho ya
kilimo kama sehemu ya marisho ya mifugo yao” Amesisitiza Mark.
Hata hivyo wananchi
wengi wa Mkoa wa Katavi wanauliza maswali “Je
mpango wa eneo la maonesho ya kilimo umesahaulika? Na je wazo hilo limebadilika
na kuachana nalo?” au kuhama kwa Mkuu wa Mkoa Juma Zuberi Homera na Mkuu wa
Wilaya ya Tanganyika Salehe Muhando kuondoka madarakani ndio wameondoka na
mawazo hayo?”.
Magreth Julius Mkazi wa Manispaa ya Mpanda, Mjasiliamali kutoka Umoja wa Wasindikaji mbogamboga na matunda. |
Magreth Julius,Mkazi
wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi na Mjasiliamali kutoka Umoja wa
Wasindikaji Mbogamboga na Matunda (UWAMBOKA) amesema kuanzishwa kwa eneo la maonesho ya kilimo katika
Mkoa wa Katavi kufanikwa kwake itakuwa sehemu ya mapinduzi makubwa ya kitakwimu
za kijinsia katika sekta ya kilimo. ili kuchangia katika sera bora na kuinua
kiwango cha mipango,ufuatiliaji na uwajibikaji katika sekta hiyo.
Salome
Mwasomola,Meneja wa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO)Mkoa wa Katavi
amesema shirika hilo linatoa huduma ya masoko hasa kuwasaidia wajasiliamali
kushiriki maonesho mbalimbali ambapi kwa mwaka 2022/23 wameweza kuhamasisha
wajasiliamali 23 ikiwa wanawake ni 17 na
wanaume 6 kwenda jijini Mbeya kwenye maonesho ya kikanda ya kilimo.
Meneja wa SIDO Mkoa wa Katavi,Salome Mwasomola. |
Meneja huyo
amefafanua faida za maonesho sio tu kukuza mtandao wa kibiashara na kuongeza
kipato cha wajasilimali kupitia kuuza bidhaa zao bali inajenga imani kwa
watumiaji wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi na kutangaza vivutio vya mkoa.
“
wajasiliamali wengi wanashindwa kwenda kwenye maonesho ya kilimo kutokana na
kuwa wanapaswa kujighalamia kwa kutumia fedha zao,Suala hilo linapunguza sana
ushiriki wa watu hasa wanawake ambao wanamajukumu ya kulea familia zao” Amesema Meneja huyo.
Chanzo cha ndani kinasema ni kweli mipango ya serikali ya Mkoa wa Katavi ni kuanzisha maonesho ya kilimo (nane nane) ambapo zaidi ya hekari 200 zimetengwa na tathimini ya awali ya ujenzi wa jengo maalumu umekamilika ambapo ujenzi wake ni thamani ya Mil 700 zitatumika.
Amesema fedha za ujenzi wa jengo hilo utatokana na michango ya halmashauri ya wilaya za Nsimbo,Mlele,Tanganyika,Mpimbwe,Manispaa ya Mpanda ikiwa kila halmashauri itatoa fedha kulingana na mapato yake ambapo hadi sasa jumla ya fedha Mil 100.1 zimekusanywa pamoja na fedha zingine kutegemea wadau.
Kutokana na fedha hizo kuwa zimetengwa na utekelezaji wa mradi huo kuchukua muda mrefu ni wazi pasipo na shaka fedha hizo kama sio kwamba ziko hatarini kupotea basi usalama wake wa kuwepo ni mdogo sana kulingana na mwenendo wa hivi karibu baada ya riporti ya CAG kuonesha madudu kwenye halmashauri nyingi hapa nchini.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko anatakiwa kuendeleza mpango wa maonesho ya kilimo ya mkoa huo kwani kupitia maelekezo ya rais Dkt Samia Suluhu Hassain anahitaji wananchi wengi kushiriki maonesho ya kilimo kwa ajili ya wakulima,wavuvi,wafugaji na wachakataji wa bidhaa mbalimbali waweze kujifunza na kubadilishana uzoefu wa teknolojia.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko |
Kwani kuanzisha
kwa maonesho ya mkoa utatoa nafasi ya wananchi wengi kushiriki tofauti na sasa
ambapo waliokwenda mkoani Mbeya tuliweza kuchukua wananchi takribani kama 225
kutoka halmashauri tano za mkoa wa Katavi.
Mkoa wa Katavi licha ya kufanya jitihada za kuwa na maonesho yake ya kilimo
lakini bado jitihada hazitoshi zinanzofanywa kwa wananchi katika sekta za uzalishaji ambapo mkoa umewahi kufanya maonesho ya siku nne ya bidhaa za kilimo,mifugo,uvuvi, bidhaa
za uchakataji na viwanda vidogo vidogo vya wanawake na wasichana.