SERIKALI YASIKIA KILIO CHA WANANCHI WA KAKESE NA ITENKA

 

Baadhi ya Wananchi katika Kijiji cha Kakese wakipita kwenye Daraja hilo la watembea kwa Miguu linalounganisha Kata ya Kakese na Itenka.

Na Paul Mathias-Mpanda

Wananchi katika kata ya Kakese Halmashauri ya Manisaapaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameishukuru serikali kwa kuwajengea Daraja la Watembea kwa Miguu linalopita Mto Mpanda na Kuunganisha Kata za Kakese na Itenka Wilaya ya Mpanda.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph [Kushoto akiwa na Moja ya Mwananchi wakivuka kwa pamoja kwenye Daraja hilo.

Wananchi katika kata ya Kakese Halmashauri ya Manisaapaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameishukuru serikali kwa kuwajengea Daraja la Watembea kwa Miguu linalopita Mto Mpanda na Kuunganisha Kata ya Kakese na Itenka Wilaya ya Mpanda.

Wananchi hao wamesema hayo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph alipotembelea Daraja hilo kwa lengo la kujionea namna Serikali ilivyojenga Daraja hilo kwa manufaa ya Wananchi hao.

Sophia Shija mkazi wa Kijiji cha Kakese amaesema kuwa kipindi cha Nyuma kulikuwa na changamoto ya kuvuka kutoka Kakese kwenda Itenka kutokana na mto huo kufurika maji na kukwamisha shughuli za kiuchumi kwa wakazi wa Kata hizo.

Shija anasema ''Kipindi cha nyuma tulikuwa tunahangaika hapa palikuwa panajaa Maji tulikuwa hatupiti lakini kwa sasa tunapita kama kawaida tunaishukuru sana Serikali kwa kutuona sisi wanakakese’’ameeleza Shija

Amebainisha kuwa kukamilika kwa Daraja hilo litaimaimarisha shughuli za kiuchumi kwenye kata hizo Jirani.

Kwa upande wake Charles Madirisha amesema kuwa mwanzoni kabla ya kujengwa kwa Daraja hilo walikuwa wanapita kwenye Mabanzi watu walikuwa wanasobwa na Maji na kupoteza Maisha hasa wakati wa Masika.

‘’Watu wengi sana wameenda na Maji hapa tulikuwa tunapita kwenye Mabanzi kwahiyo tulikuwa tunateleza na mtu anaenda na maji anasema Madirisha’’

Anabainisha kuwa kabla ya kujengwa kwa Daraja hilo walikuwa wanavuka kwa kuvushwa na watu kwa kutoa kiasi cha Shilingi Elfu Moja ila kwa sasa wana ishukuru serikali  kwa ujenzi wa Kivuko hicho.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiwa katika Daraja hilo amesema kuwa serikali kwa kutambua umuhimu wa kujenga Daraja hilo pamoja na Kunyanyua barabara inayounganisha kata hizo kwa Gharama ya Shilingi Milioni 162.

‘’Tunamshukuru sana Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwakutuletea fedha kwaajili ya  ujenzi wa Daraja la hili la watembea kwa Miguu pamoja na kunyanyua barabara hii ambayo tumeiona hapo fedha zilizotumika hapa ni shilingi Milioni 262 ‘’anasema Jamila

Ameeleza kuwa eneo hilo lilikuwa na adha kubwa kwa wanananchi kuvuka kutoka kata ya Kakese na Kata ya Itenka hali ambayo iliwafanya wananchi kuchangishana wenyewe na kuweka Vivuko vya Miti ambayo havikuwa na uiamara kwa wakati huo.

Amewaagiza Tarura Wilaya ya Mpanda kujengelea maeneo ya Kingo kwenye daraja hilo ili kuepusha Mmomonyoko ambao unaonekana ili kuepusha Daraja hilo Kusobwa na Maji.

Saimon telephonesi mhandisi wa Tarura Wilaya ya Mpanda amesema pamoja na serikali kujenga Daraja hilo wao kama Tarura Wilaya ya Mpanda wameshaandika Barua kwa mtendaji mkuu wa Tarura kwaajili ya ujenzi wa Daraja la kudumu kwenye eneo hilo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages