MBUNGE VITI MAALUMU ATUMIA MILIONI 249 KWENYE JAMII

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi Taska Mbogo akizungumnza wakati wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji ya mwaka 2020/2025

 Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa KataviTaska Mbogo  ametoa zaidi ya shilingi Milioni 249 kwa kipindi cha miaka mitano ikiwa ni sehemu ya  mchango wake kwenye jamii na kwenye Chama cha Mapinduzi kwa Mkoa wa Katavi .


Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa KataviTaska Mbogo  ametoa zaidi ya shilingi Milioni 249 kwa kipindi cha miaka mitano ikiwa ni sehemu ya  mchango wake kwenye jamii na kwenye Chama cha Mapinduzi kwa Mkoa wa Katavi .

Hayo ameyasema wakati wa kikao cha Baraza la  jumuia ya wanawake CCM(UWT)Mkoa wa Katavi kilichofanyika katika ukumbi wa idara ya maji uliopo katika Manispaa ya Mpanda .

Amebainisha kuwa michango hiyo ameitowa kwa moyo wake na  wala  kakulazimishwa na mtu yeyote yule bali ni kutokana na mapenzi aliyonayo ya kuwatumikia wananchi na chama chake cha CCM.


Amesema    hayo ameyafanya  kama   sehemu yake ya kuwa mbunge wa viti  maalumu Mkoa wa Katavi (ccm) miongoni mwa michango aliyoitowa kwenye jumuia za  chama  na chama  ni  uwezesha wa kiuchumi na kwenye jamii amechangia miundo mbinu mbalimbali ya afya na elimu.

Mbunge Taska Mbogo   amesema  katika kipindi hicho ameweza  kutembelea jumla ya Kata ya  53  kati ya Kata  58  zilizopo katika Mkoa wa Katavi na aliweza kufanya kazi pia ya  kuimalisha chama na kuwaeleza wananchi  yale   mambo  mazuri yaliofanywa na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Amesema ameweza kufanikiwa  kuwaeleza wanawake  wajiunge   kwenye vikundi  ili  waweze  kukopesheka   kwani  mikopo kwa ajiri ya akina  mama     vijana na watu wenye ulemavu ni swala la kisheria kwa kila Halmashauri  zote nchini kutenga asilimia  kumi  kwa ajiri ya makundi hayo kutoka kwenye mapato yao ya ndani .

Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Katavi Idd Kimanta amewapongeza wabunge    Taska  Mbogo na  Matha Mariki kwa kazi yao kubwa  ya kuwatumikia wananchi .

Alisema wabunge hao wa viti maalumu wamefanya kazi kubwa ya kutoa michango kwenye jumuia yao na kwenye jumuia nyingine za chama na kwenye jamii.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages