![]() |
Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Daud Lyamongo akitoa taarifa ya utendaji wa Takukuru kwa Kipindi cha Januari-Marchi |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)Mkoa wa Katavi
imebaini kukunuliwa kwa mabati yenye thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 220 yakiwa chini ya kiwango yaliyonuliwa kwa ajili
ya ujenzi wa Shule ya mpya ya sekondari ya Kitaifa ya Wavulana
ya Katavi.
Akitowa
taarifa ya ufuatiliaji wa utelelezaji wa miradi ya maendelo wa robo mwaka
kuanzia mwezi Januari hadi Machi mwaka huu kwa niamba ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa
wa Katavi; Afisa TAKUKURU, Daud Lyamongo amesema mabati hayo
wameyabaini baada ya ufatiliaji waliofanya wa kukagua miradi katika
sekta ya elimu.
Lyamongo
amebainisha kuwa katika kipindi hicho wameweza
kuokoa kiasi cha shilimgi 220,023,980 na wakiwezesha
kupanda kwa mapato ya stendi ya Mizengo Pinda Manispaa ya Mpanda
kutoka shilingi 500,000 kwa siku hadi 700,000.
Katika
utekelezaji wa jukumu hilo waliweza kukagua utekelezaji
wa miradi miwili ya elimu yenye thamani ya
Bilioni 4.3 na waliweza kubaini uwepo wa mapungufu
mbali mbali kwenye mradi wa shule ya sekondari ya Wavulana Katavi.
Afisa
hiyo wa TAKUKURU ameyataja mapungufu hayo kuwa ni mabati yaliyokuwa
yamenunuliwa kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo yenye
thamani ya shilingi 220,023,980 wameyabaini yakiwa chini ya
kiwango .
Ametaja
kasoro nyingine kwenye ununuzi wa bati ambapo walibaini yako chini ya kiwango
huku Mzabuni alilipwa fedha za kununulia mabati
hayo kabla hajayafikisha kwenye eneo la
ujenzi jambo ambalo n kinyume cha utaratibu za manunuzi .
Baada
ya kubaini hayo TAKUKURU Mkoa wa Katavi walifanya kikao
kilichowahusisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda, Mkuu wa Mkoa na
Mzabuni na kumtaka mzabuni abadilishe mabati na
kuleta mabati yanayokubalika kwa mujibu wa
muongozo wa Serikali .
TAKUKURU
wanaendelea na uchunguzi na watakao kuwa wamebainika kuhusiana na
ununuzi wa bati hizo pasipo kufuata utaratibu watachukuliwa hatua
za kisheria dhidi yao .
Kuhusu
uchambuzi wa mifumo amesema wamefanya uchambuzi wa
mfumo wa ukusanyaji wa mapato katika stendi kuu ya
Mizengo Pinda Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na kuwezesha
kupandisha mapato kutoka 500,000 hadi 700,000 ikiwa ni ingezeko la
shilingi 72,000,000 kwa mwaka .
Lyamongo amewakumbusha wagombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu wa 2025 kutojihusha na vitendo vya rushwa na kufuata taratibu kanuni na miongozo iliyotolewa na tume huru ya uchaguzi