WANANCHI WALALAMIKIA CHANZO CHA MTO KUVAMIWA.

Muonekano wa bustani za mboga mboga kando ya mto kasimba hali ambayo inatishia usalama wa mto huo 

 Na Mwandishi wetu

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda katika Mkoa wa Katavi wamelalanikia uhalibifu wa  mto Kasimba ambao ni chanzo cha maji unavyoharibiwa  kwa kufanyiwa shughuli za kilimo huku mamlaka  zikishindwa kuchukua hatua zozote za haraka za kuunusuru mto huo.

Hali ilivyo kwa sasa kwenye mto kasimba ambao wananchi wameanza kufanya shughuli za kibinadamu hususani kilimo cha bustani za mboga mboga kwenye kingo za mto huo.

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda katika  Mkoa wa Katavi wamelalamikia uhalibifu wa  mto Kasimba ambao ni chanzo cha maji unavyoharibiwa  kwa kufanyiwa shughuli za kilimo huku mamlaka  zikishindwa kuchukua hatua zozote za haraka za kuunusuru mto huo.

Wananchi wamedai kuwa  endapo mamlaka  hazitachukua hatua za haraka upo uwezekano  mkubwa wa chanzo hicho cha mto Kasimba  unaounganisha barabara muhimu ya kutoka kati kati ya  Mji wa Mpanda na barabara ya kwenda Sumbawanga Mkoani Rukwa.

Selemani Tengeneza  mkazi wa  Mtaa wa Kasimba amesema eneo hilo limekuwa ni kawaida  wala si  jambo geni kwa wananchi kufanya shughuli za kilimo na za kibinadamu  kwani wamekuwa wakilima bustani za  mboga mboga  na kupanda mahindi kwenye chanzo cha mto huo

Ameiomba Serikali  kuchukua hatua sitahiki za haraka kunusuru chanzo hicho cha mto ambacho kimekuwepo kwa muda mrefu sasa kuliko kukiacha kikiendelea kuhalibiwa huku  uwezekano wa kukinusuru upo unawzekana .

Salome John ameeleza kuwa hapo zamani ilikuwa ni marufuku kabisa kwa wananchi  kufanya shughuli zozote za kilimo wala za kibinadamu lakini wanashangaa miaka  ya hivi karibuni watu kuachwa wakiendelea na shughuli za kilimo cha bustani.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages