Na Alex Ngereza-Pwani
Madiwami
katika halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wamesema kuwa halmashauri ya Nsimbo
itakuwa miongoni mwa halmsahauri zinazokusanya mapato kwa wingi katika mkoa wa
Katavi ili kuisaidia halmashauri
kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo.
Madiwami katika halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wamesema kuwa halmashauri ya Nsimbo itakuwa miongoni mwa halmsahauri zinazokusanya mapato kwa wingi katika mkoa wa Katavi ili kuisaidia halmashauri kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo.Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe akitoa neno kwa Uongozi wa Halmashauri ya Chalinze katika ziara ya Madiwani wa Halmashauri ya Nsimbo kwenye Halmashauri ya Chalinze
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Nsimbo Halawa Malendeja amesema Ziara hiyo inaenda kuleta mafanikio makubwa kwenye halmashauri kutokana na kufika eneo sahihi la kujifunza na hitaji lao la namna ya ukusanyaji wa mapato pamoja na shughuli za kiutawala
Madiwani kutoka halmashauri ya Nsimbo mkoa wa Katavi walipotembelea Soko la Kisasa la Chalinze kwenye ziara hiyo |
Diwani wa Viti maalumu kutoka Kata ya Itenka Nesta Masebo amesema kupitia ziara hiyo ya kutembelea Halmashauri ya Chalizwe wameongezewa maarifa na ujuzi juu ya kubuni vyanzo vingi vya Mapato ambavyo vitaisadia halmashauri ya Nsimbo kuwa katika ukusanyaji wa Mapato.
Mbunge wa Jimbo la Nsimbo,Anna Lupembe akiwa na Madiwani wa Halmashauri ya Nsimbo walipotembelea Kituo cha Redio Chalinze |
Lupembe amesema halmashauri ya Chalinze Muundo wa Kiutawala inafanana nayo kwa maana hiyo wameona ni vyema kwenda halmashauri ambayo wanaendana nayo kiutawala pamoja na halmashauri hiyo kuwa na ukusanyaji Mkubwa wa makusanyo ambayo yanafikia zaidi ya bilioni 15 hii ni sababu iliyowafanya kwenda kwenye Halmashauri hiyo.
Diwani wa Kata ya Nsimbo Michael Kasanga,akiwa katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashari ya Chalinze wakati wa ziara hiyo. |
Katika ziara hiyo Madiwani wametembelea Mradi wa radio Halmashauri ya Chalinze wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 102, Mradi wa soko la kisasa wenye thamani ya shilingi milioni 705, Ujenzi wa shule ya Msingi wa shilingi milioni 400, pamoja na kupatiwa Elimu bora ya ukusanyaji wa Mapato katika halmashauri ya Chalinze.