DC : MWANGA AWAAGIZA WENYEVITI WA VITONGOJI KUHAMASISHA CHANJO YA POLIO

 

Mkuu wa Wilaya ya Mlele  - ALHAJ.MAJID MWANGA  akiongea na wajumbe wa kamati ya Afya ya Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Kwenye ukumbi wa mikutano Jengo la utawala Halmashauri ya WILAYA

Na  Kibada Ernest-MLELE

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Alhaj Majid Mwanga amewaagiza Wenyeviti wote wa Vitongoji,na watendaji wa Vijiji kufanya   mikutano ya hamasa kuhamasisha wananchi  ili waweze kuwa na uelewa pamoja na  watoa ushirikiano wa karibu  wakati wa zoezi la kutoa chanjo ya polio litakalofanyika tarehe 21 hadi 24 mwezi Septemba mwaka 2023 kwa Mkoa wa Katavi na mikoa mingine hapa nchini

Wajumbe wa kamati ya Afya ya Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Mlele Kwenye kikao hicho.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Alhaj Majid Mwanga amewaagiza Wenyeviti wote wa Vitongoji,na watendaji wa Vijiji kufanya   mikutano ya hamasa kuhamasisha wananchi  ili waweze kuwa na uelewa pamoja na  watoa ushirikiano wa karibu  wakati wa zoezi la kutoa chanjo ya polio litakalofanyika tarehe 21 hadi 24 mwezi Septemba mwaka 2023 kwa Mkoa wa Katavi na mikoa mingine hapa nchini

Mwanga ametoa maelekezo hayo wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya Msingi cha Wilaya ya Mlele kilichoketi kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya  ya Mlele leo

Aidha Alhaji Mwanga ametoa ombi kwa Viongozi wa dini  kuwa  siku za Ibada  na baada ya kukamilika Ibada hiyo kwa madhehebu yote  kuwatangazia waumini wao   kuwa tarehe ya chanjo ya polio  kuwa itakuwa siku ya Alhamisi  tarehe 21-24 mwezi Septemba kuwa itakuwa ni siku ya chanjo,na walengwa ambao ni  watoto wenye umri chini ya miaka minane 8 na kuendelea, hivyo waweze watu watoe ushirikiano wa kutosha,  ili tuvuka lengo tulilojiwekea.

Amesisitiza  kuwa Viongozi  wa kisiasa  watoe ushirikiano wa kutosha  kwa kushiriki nasi ili tuwe na uelewa wa pamoja ,viongozi waendelee  kutoa hamasa kwa jamii ili wote wawe na uelewa wa pamoja kuhusu chanjo ya polio.

Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii Bahati Mwailafu akiwa hutubia wajumbe kikao cha Kamati ya Afya Msingi Halmashauri ya Wialaya ya Mlele.

Mwakilishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii   Bahati Mwailafu ameipongeza timu ya Uendeshaji wa huduma za Afya ngazi ya Wilaya (CHMT} ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kwa maandalizi na hatua za haraka zilizochukuliwa baada ya kisa  kimoja cha polio kuripotiwa hapo mei 26 mwaka huu.

Mwakilishi huyo wa wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Mwailafu  amesisitiza kuwa watoto wote waliolengwa wapatiwe  chanjo  ili kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Polio,ugonjwa huo ambao unaathiri watoto  chini ya miaka 05 hadi 15, ambapo watoto wote wenye umri chini ya miaka 8 watapatiwa chanjo ya polio.

Kwa upande wake Mwakilishi wa TAMISEMI Monica Julias amesisitiza watumishi kufanya kazi kwa moyo wa upendo na kujituma hasa kwa wahudumu wa afya wawe na moyo wa kuwapenda wagonjwa maana mapokezi wakati wakija kuoata uhuduma tiba inawafanya wagonjwa wajione wamepona kutokana na mapekezi jinsi wanavyokirimiwa kwa maneno mazuri ya kutia moyo na kufariji

Teresia Irafay ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya alishukuru kwa yote yaliyoelezwa na kuahidi kuwa maelekezo yote yaliyotolewa wataenda kuyafanya kazi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Soud Mbogo akitoa neno kwenye kikao hicho 

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Dkt Thadeus Makwanda  ameeleza kuwa lengo la halmashauri ya Wilaya ni kuwapatia chanjo ya polio watoto wapatao 13,658 katika vijiji vyote 18 vilivyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele.

Mratibu wa Chanjo Halmashauri ya wilaya ya Mlele Haldy  Lushats akiwasilisha majukumu ya Kmati ya Afya ya Msingi ya Wilaya ameeleza kuwa ni kutoa elimu kwa Jamii.kutoa Taarifa ya Utekelezaji wa chanjo, kumsaidia Mganga Mkuu wa Mkoa na Wilaya namna ya kutekeleza chanjo,kwa mantiki hiyo kamati ya Afya ya ngazi ya wilaya ipo kwa mjibu wa sheria na ipo kusaidia upotoshaji wa baadhi ya watu kuwa chanjo zina madhara.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Teresia Irafay akielezea namana Halmashauri hiyo ilivyojipanga kutoa chanjo ya Polio kwa watoto kwenye halmashauri hiyo

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Mlele Mhe.Soud Mbogo amewasisitiza  kutoa ushirikiano kuhakikisha zoezi la chanjo ya polio linafanikiwa kwa halmashauri yote ya Mlele akawataka waendelee kuelimisha jamii kuhakiksha watoto wote lengwa wanapatiwa chanjo.

“Twende tukahamasishane huko majumbani kwetu ili kufanikisha zoezi hili la chanjo ya polio kila mtoto anayesitali aweze kupata chanjo ya polio.”amesema Mbogo .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages