RC KATAVI AIAGIZA TANESCO KUWALIPA FIDIA WANANCHI KWA WAKATI

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizumgumnza na Wananchi wa Manispaa ya Mpanda Eneo la Mpanda Hoteli


Na Jackson Gerald,Katavi 

Serikali katika Mkoa wa Katavi imeliomba Shirika la Umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa Katavi kuwalipa fidia Wananchi waliopisha Maeneo yao kwaajili ya Kupisha Mradi wa Umeme wa Grid ya Taifa Katika Mkoa wa Katavi.

Serikali katika Mkoa wa Katavi imeliomba Shirika la Umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa Katavi kuwalipa fidia Wananchi waliopisha Maeneo yao kwaajili ya Kupisha Mradi wa Umeme wa Grid ya Taifa Katika Mkoa wa Katavi.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko wakati akizungumnza na wananchi wa Mkoa wa Katavi Eneo la Mpanda Hotel wakati akisikiliza na kutatua Kero za wananchi kupitia Mkutano wa Hadhara.

Mrindoko amesema kuwa zoezi la kuwalipawa Fidia wananchi hao nilamuhimu kwakwuwa wananchi hao wameonyesha uzalendo kwa kupisha maeneo yao ili mradi huo uweze kufika katika Mkoa wa Katavi.

‘’kuna baadhi ya wananchi walibomolewa nyumba zao na miongoni mwao kutofanya uendelezaji wa maeneo hayo kwa kupisha mradi huo Tanesco fatilieni Malipo hayo ili wananchi hawa wapate haki yao ‘’amesema Mrindoko.

Hatua hiyo inakuja baada ya Mwananchi Mmoja aliejulikana kwa Jina la Athumani Jummanne Mkazi wa Mpanda hotel kupata kufahamu kuwa changamoto ya kutokulipwa kwa Wakati inasabishwa na nini kwakuwa walibomolewa nyumba zao na kupelekea kuishi kwenye Nyumba za Kupanga.

‘’Mkuu wa mkoa mimi ni mwaka mmoja umepita sina sehemu ya kukaa nipo kwenye nyumba za kupanga naomba msaada wako mimi ninawatoto 6 na wake wawili niwaweka wapi ‘’amesema Jummanne

Kutokana na Changamoto hiyo Meneja wa Shirika la umeme Tanzania Tanesco Mkoa wa Katavi Mhandisi Seraphine Lyimo amekili kuwepo kwa changamoto hiyo nakubainisha kuwa kulikuwa na changamoto ya kimfumo wa Malipo na kuwaomba wananchi hao kufika ofisi za Tanesco mkoa ili kuhakiki majina yao na taratibu zingine kuendelea.

‘’Malipo ya fidia kwa wananchi waliopitiwa na Mradi wa Umeme wa Grid ya Taifa tayari yameshafanyika kwa baadhi ya Wananchi katika Wilaya za Mkoa wa Katavi ingawa kuna baadhi yao hawajalipwa kutokana na mchakato wa kufanya Tathimini ya Mali zilizopitiwa na Mradi huo amesema Lylimo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages