KAMCHAPE ASABABISHA WANAWAKE KUKIMBIWA NA WAUME ZAO.

 

Baadhi ya muonekana  wa maeneo ya  Kijiji cha Ikola   Tarafa ya Karema  W\ilaya ya Tanganyika ambako wanaume wamewatelekeza wake wao kwa kuhofia kukamatwa na polisi kwa tuhuma za kujihusisha na kumuunga mkono mtu anadai anauwezo wa kuagua na kuwabaini wachawi  (Kamchape)

Na Walter  Mguluchuma.Katavi .

KATIKA hali  isiyo ya  kawaida  idadi ya wanawake  walikuwa  wanaishi na waume zao katika Kata za Ikola na Karema mwambao mwa   Ziwa Tanganyika Wilayani Tanganyika Mkoa wa Katavi  wamebakia kuishi bila waume zao kwa sasa  kufatia  wame zao kuwakimbia kwa kuhofia kukamatwa na Polisi kutokana na tuhuma z a kumuunga  mkono  mtu  anaedaiwa  kuwa  na uwezo wa kuagua na kufichua wachawi (Kamchape)

Mmoja wa   wanawake wa Kijiji cha  Ikola  jina  tunalo  alisema  kwa karibu wiki mbili sasa anaishi  bila mwenza wake ambae  amemkimbia bila hata ya  kumuaga na kumwachia  familia ya watoto  watano kutoka na kuhofia kukamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kujiusisha na kundi lilikuwa linamuunga mkono  mganga wa kienyeji (kamchape ) aliyekuwa anadai  anao uwezo wa kubaini washirikina(wachawi)

Amebainisha kuwa  Kamchape  alipokuwa amefika kwenye  Kijiji chao cha Ikola mume wake alikuwa ni miongoni mwa watu  waliokuwa wanamuunga mkono  Kamchape afanye kazi ya  kuwabaini wachawi  lakini  mume wake alivyoona watu waliokuwa wanamuunga mkono  mganga huyo kuanza kukamatwa na Polisi nae pia alitokemea pasipo  kujulikana na wala  hata mawasiliano nae   kama familia hawana 

Huo ni  mwonekano wa baadhi ya  maeneo ya   Kijiji  cha Karema ambako wanawake wamekimbiwa na wame  wao baada ya kuhofia kukamatwa na polisi kwa tuhuma za  kumuunga mkono mtu anae daiwa kuwa ana uwezo wa kubaini wachawi (KAMCHAPE)

Nae   mama    mwingine wa    Kata ya Karema  ambae hakuta jina lake litajwe  alisema  mume wake amekimbia nyumbani kwa  kwa muda wa siku kumi sasa kwa kuhofia  kamata kamata inayoendelea   ya watu walikuwa wakiumuunga mkono  Kamchape  na kufanya uhalifu wa mali  mbali mbali za watu .

Alieleza mume wake aliwaaga nyumbani siku kumi zilizopita kuwa     anakwenda  kwenye shughuli zake za kila siku  za uvuvi wa kati akiwa ziwa alipata taarifa za kuwepo kwa msako wa watu waliojihusisha na uhalibifu wa mali za wafanya biashara  wakati wa Kamchape .

 Alieleza kuwa walioathirika na kukumbiwa na waume  zao ni wanawake wengi tuu kwenye maeneo ya Kata ya Karema  na pia wapo baadhi ya wanaume nao wamebaki bila  wake zao kufatia wanawake kukimbia kukamatwa  kwan kujihusisha na kumuunga mkono  mganga huyo wa kienyeji .

Nae Mkazi wa Kijiji cha Ikola  Emanual  Kibiriti alisema upatikana wa  samaki   katika   maeneo ya Kata za Ikola  na Karema umekuwa ni  washida kutokana na wavuvi wengi   ambao ndio walikuwa wakimuunga mkono  Kamchape kukimbia na kuacha  kufanya shyghuli yao ya uvuvi .

Amefafanua kuwa  idadi kubwa ya wanawake walikimbiwa na waume zao  kutoroka kwa kuhofia kukamatwa na jeshi la polisi ni wake wa wavuvi wa samaki  ingawa pia wapo na wanaume nao wamekimbiwa na wake zao na kuwaachia  watoto.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages