MRADI WA SHULE BORA WAJA NA MAJIBU YA UGUMU WA SOMO LA HESABU

 

Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Mwalimu Upendo Rweyemamu akifunga Mafunzo ya Siku Nne kwa Walimu 50 wa Somo la Hesabu katika shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

Na Paul Mathias,Mlele

Walimu wa Masomo ya Hesabu katika shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya Mlele mkoa wa Katavi wameobwa kwenda kutumia ujuzi walioupata katika mafunzo maalumu kuhusu Somo la Hesabu Kupitia Mradi wa Shule Bora unaotekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na Serikali ya Uingreza kupitia Shirika la UK aid.

Walimu wa Shule za Msingi Mlele wa Masomo ya Hesabu wakiwa katika Majadiliano ya vikundi katika semina hiyo.

Walimu wa Masomo ya Hesabu katika shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya Mlele mkoa wa Katavi wameobwa kwenda kutumia ujuzi walioupata katika mafunzo maalumu kuhusu Somo la Hesabu Kupitia Mradi wa Shule Bora unaotekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na Serikali ya Uingreza kupitia Shirika la UK aid.

Akifunga mafunzo hayo ya Siku nne Kwa Walimu hao Afisa Elimu Mkoa wa Katavi Mwalimu Upendo Rweyemamu amesema kuwa ujuzi walioupata walimu hao kwa kipindi cha Siku nne ukatumike katika kuongeza ufaulu wa Somo la Hesabu ikiwa ni Msingi kwa somo hilo katika Masomo ya Sayansi.

‘’Mafunzo haya mliyoyapata yanalengo la kuwaongezea umahiri ninyi Walimu wa Hisabati katika kuchanganua Dhana Mbalimbali za kihisabati tumekuwa tukipata changamoto sababu ya kukosa Msingi mzuri kwenye Hesabu huku chini watoto hawa wanapanda huku wakijua Hesabu ni Ngumu Kupitia Mafunzo haya nendeni mkabadilishe Taswila hiyo kwa wanafunzi wetu’’amesema Rweyemamu

Ameeleza kuwa katika siku za hivi karibuni kumekuwa na tatizo la kwa somo la Hesabu kutofanya vizuri kwa wanafunzi Kutokana na Sababu mbalimbali hivyo serikali kwa kuliona hilo imeweza kuandaa Semina kwa walimu Hamsini kupitia Mradi wa Shule bora unaotekelezwa na serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Uingereza chini ya shirika la UKaid.

‘’Umahili mliojengewa leo unakwenda kufanya kitu cha tofauti kwenye Halmashauri yetu na ninyi mnaenda kuwa Chachu ya Mageuzi na Mabadiliko katika somo hili la Hisabati ukiangalia katika Takwimu za kitaifa bado Somo la Hisabati halifanyi Vizuri sana wanafunzi wetu wamekalili Somo hili ni gumu hapana ila ni namna ya wewe mwalimu unavyomwandaa Mwanafunzi kuhusu somo hilo ukimwambia Somo ni gumu ataendelea kuamini Somo la Hisabati ni gumu’’ amesema Rweyemamu

Awali akitoa taarifa juu ya Mradi wa Shule Bora Katika Mkoa wa Katavi Mratibu wa Mradi wa Shule Bora Mkoa wa Katavi George Mtawa amesema kuwa Mradi wa Shule bora unaofadhiliwa na serikali ya Uingereza Kupitia Shirika la UK aid kwa kushrikiana na serikali ya Tanzania katika mkoa wa Katavi wameweza kufanya Mafunzo kwa walimu katika Halmshauri zote za Mkoa wa Katavi.

‘’Mwezi wa nane tulikuwa na mafunzo ya Elimu Jumuishi katika Halmashauri ya Mpibwe na sasa hivi tunamafunzo hapa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kwaajili ya uboreshaji wa ufundishaji wa Somo la Hisabati kwa Walimu Hamsini kutoka kwenye Shule 25 ambapo kila shule imeleta walimu wawili ‘’anasema Mtawa

Walimu wa Shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wanaofundisha Masomo ya Hesabu wakiwa katika Mafunzo juu ya namna bora ya kuongeza ufaulu wa Somo la hesabu

Amina mwajumbe Mwalimu Kutoka shule ya Msingi Wachawaseme kuwa baada ya kupatiwa mafunzo hayo ya somo la Hesabu anaamini ufaulu wa Somo hilo kwa wanafunzi utakwenda kuongezeka kutokana na kile walichojifunza kuhusu mbinu bora za ufundishaji wa somo la Hesabu kwa wanafunzi.

Kwa upande wake Mwalimu Tom Mwakabanje Shule ya Msingi Kamsisi amiishuru Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na serikali ya Uingereza kupitia shirika la UK aid kuja na Mradi wa Shule bora ambao sasa walimu wasomo la Hesabu wanaongezewa ujuzi ili wanafunzi waendelee kufaulu somo hilo mara dufu zaidi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages