Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko [wapili kulia] aliposhiriki zoezi la uzinduzi wa Masoko ya Tumbaku Mwezi wa Tano Mwaka huu Katika chama cha Nsimbo AMCOS
Na Walter Mguluchuma,Katavi
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewahakikishia wakulima wa zao la Tumbaku katika msimu wa kilimo 2022/2023 ambao hawaja lipwa fedha zao zaidi ya Dola Milioni 2.5 kwenye Amcos 6 zilizoingia Mkataba wa ununuzi wa Tumbaku na Kampuni ya Mkwawa Leaf LTD zinatarajiwa kulipwa hivi karibuni na kampuni hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akisaini mfano wa Bello Tiketi ya Tumbaku wakati wa uzinduzi wa Masoko ya Tumbaku mkoa wa Katavi mnamo Mwezi May Mwakaa huu |
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo
vya habari RC mrindoko amesema anawahakikishia wakulima wa Amcos
sita ambazo hazijalipwa Fedha ya mauzo ya Tumbaku tayari serikali imefanya jitihada Kupitia Rais Dkt Samia Saluhu Hassan amefanya
jitihada kubwa za kuhakikisha wakulima hao wanalipwa fedha
zao hivi karibuni kuanzia tarehe 4 septemba na kuendelea wataanza
kulipwa .
Amebainisha kuwa Serikali ya Mkoa wa Katavi
inafahamu kuna wakulima wa Tumbaku
hawajalipwa fedha zao kwa wakati walizouza Tumbaku yao
kwa msimu wa mauzo ya tumbaku ya mwaka huu.
Amezitaja Amcos sita ambazo hazijalipwa fedha
zao na Kampuni ya Mkwawa kuwa ni Nsimbo , Bulamata ,Magunga ,Kasekese , Muungano na IlundeMkurugenzi wa Kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya Mkwawa Leaf LTD Ahmed Mansoor Huwel akiwa katika uzinduzi wa Msimu wa Masoko Mapema Mwezi May,2023 Katika Halmashauri ya Nsimbo
Mrindoko amesema Jumla ya fedha ambazo
wakulima wa Amcos hizo wanazodai Kampuni ya Mkwawa ni Dola za
Kimarekani Milioni 2.582 tatizo la wakulima kutolipwa fedha zao kwa
wakati si Mkoa wa Katavi peke yake na limetokana na matatizo
ya kiuchumi duniani ulisababishwa na uhaba
wa Dola .
Hivyo amewaelekeza wakuu wa Wilaya wote wa
Wilaya zilizopo katika Mkoa wa Katavi kusimamia fedha hizo
mara baada ya kuwa zimeingia kwenye Akaunti za
Amcos wahakikishe wakulima wanalipwa malipo yao kwa haraka
pasipokuwa na kucheleshwa hata kidogo .
Mrindoko ameeleza kuwa Rais
Dkt Samia amefanya kazi kubwa hivyo anawahakikishia
wakulima wa Mkoa wa Katavi malipo wanayodai wakulima watalipwa hivi
karubuni kwani wakulima watambue kuwa Serikali ipo pamoja nao
siku zote kuhakikisha haki ya kila mkulima inapatikana .
Aidha amewataka wakulima wa zao hilo kuendelea kulima kwa bidi
kwani hawatarajii tena kuona tatizo hilo linaendelea tena
kwenye msimu ujao wamejipanga kuondoa tatizo hilo kwa
kuyasimamia kikamilifu makampuni ya ununuzi wa Tumbaku .
Katika Mkoa wa Katavi kuna
makampuni mawili ambayo yanayonunua Tumbaku ambayo ni
Premium ambayo imeisha lipo kiasi cha Dola milioni 19.598
na wao hawadaiwi hata
senti moja na wakulima wao kampuni ya pili ni ya Mkwawa ambao wao
wanadaiwa na wakulima kiasi cha Dola milioni 2.582. .