WAKULIMA WA TUMBAKU WASAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA TUMBAKU.

 

Mwakilishi wa  Kampuni ya Ununuzi wa Tumbaku ya Premium Yusuph Mahundi  akisaini   mkataba wa ununuzi wa  Tumbaku na   kimoja wapo cha chama cha msingi  cha ushirika  ambacho wameingia nacho mkataba kwa msimu wa 2023/2024

 

 

Na Walter Mguluchuma,Katavi

Vyama vya  Msingi vya ushirika vya  wakulima wa Tumbaku   katika  Mkoa wa Katavi   vimesaini   mikataba na  makampuni ya ununuzi  wa  zao la Tumbaku kwa ajiri ya  msimu wa kilimo  2023/2024 kwa vyama  vya Msingi 21 huku  chama kimoja kikigoma kusaini   mkataba na Kampuni ya  Mkwawa  Leaf Tobaco .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akiongea na viongozi wa Vyama vya Ushirika na Makampuni yaliyoingia Mkataba wa ununuzi wa Tumbaku

Vyama vya  Msingi vya ushirika vya  wakulima wa Tumbaku   katika  Mkoa wa Katavi   vimesaini   mikataba na  makampuni ya ununuzi  wa  zao la Tumbaku kwa ajiri ya  msimu wa kilimo  2023/2024 kwa vyama  vya Msingi 21 huku  chama kimoja kikigoma kusaini   mkataba na Kampuni ya  Mkwawa  Leaf Tobaco 

Mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika  Mkoa wa Katavi Peter  Nyakunga  amesema  vyama hivyo vimesaini mikataba na makampuni  mawili yanayonunua tumbaku katika Mkoa wa Katavi  ambayo ni  Premium na  Mkawa kukiwa na lengo la uzalishaji wa kili  19,028, 462 ambazo zinatarajiwa kuzalishwa katika msimuujao wa kilimo .

Kktika mikataba hiyo   Kampuni ya Premium imeingia  mikataba yenye uzalishaji wa kilo  14 265 862 na  Kampuni ya  Mkwawa kili 4,762 600   utiaji huo saini mitakataba umeshudiwa na  Mkuu wa Mkoa wa Katavi   pamoja  na viongozi wa Chama Kikuu cha Ushirika  cha Mkoa wa Katavi Latcu  wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama,  Bodi ya Tumbaku na wadau mbalimbali wa kilimo .

Nyakunga amebainisha  kuwa   kanuni namba  36 ya Sheria ya zao la Tumbaku inazungumzia   habari  za  malipo ya wakulima  baada ya kuuza tumbaku yao malipo yanatakiwa kufanyika ndani ya siku 14 pamoja na mikataba hiyo iliyosainiwa  kwa ibara 25 ibara ya 9.1 inaeleza kuwa  mnunuzi  na  chama kikuu cha ushirika wanahakikisha malipo yanafanyika ndani ya siku 14 baada ya kufanyika kwa soko .

Utaratibu huo wa  kusaini  mitakaba ni  mpya kwa hapa nchini tofauti na ulivyokuwa  umezoweleka  katika misimu yote iliyopita huku lengo kuu ikiwa ni kuweka uwzi  na  kuaminiana na utaratibu huo utakwenda  kutatua changamoto  zilizikuwa zikijitokeza na kuleta malalamiko .

Meneja wa Bodi ya Tumbaku  Mkoa wa  Katavi  Genuin Swai  amesema zoezi hilo  ni la kihistoria kwani haijawahi kutokea hapa nchini mikataba ya ununuzi kwenye vyama vya ushirika vya msingi ikashuhudiwa na wadau wote hivyo ni historia kwa sekta ya tumbaku  .

Amesema mikataba hiyo imefanywa kufatia maelekezo yaliyokuwa yametolewa na waziri wa  Kilimo  Hussein Bashe alieagiza  mikataba ya msimu  huu  ufanyike  baina ya makampuni ya ununuzi wa  Tumbaku na vyama walivyonunua tumbaku ya msimu uliopita

Hivyo kila chama kinatakiwa kuendelea na kampuni yake ya msimu uliopita  kwa hali hiyo hata kama chama  kitakataa kuingia  mkataba na kampuni yake ya msimu uliopita  kampuni nyingine haiwezi kukichukua   ikiwa  ni   katika kulinda ushindani  ili kuondoa migogoro ya msimu uliopita  na kuongeza mahusiano kati ya hivyo vyama  na kampuni na kuendelea na ushindani wenye tija kuliko kubakia na kampuni moja .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko amesema  Mkoa umeweka utaratibu wa kusaini mikataba kwa njia ya ili kuondokana na malalamiko.

Ameyataka Makampuni  yaliyoingia  mkataba na vyama hivyo  kuhakikisha  wanawalipa wakulima fedha zao kwa asilimia mia moja kwa mwaka huu  utakuwa wa mwisho hawatakubali kuona kampuni ya ununuzi wa Tumbaku  inashindwa  kuwalipa wakulima kwa wakati .

‘’Mkoa  hauta vumilia kampuni ambayo inasusua kuwalipa wakulima  hivyo  agizo hilo walizingatie na walitilie maanani  kwani   malengo ya Rais na viongozi wa Mkoa wa Katavi  ni kuhakikisha wanasimia masilahi ya wakulima  ili walipwe malipo yao kwa asilimia  mia moja ‘’ amesema Rc Mrindoko

Aidha  katika  utiaji  saini huo  chama cha ushirika cha Msingi cha Magunga  kimekataa  kuingia  mkataba na Kampuni ya  ununuzi wa Tumbaku ya Mkwawa  katika hali ambayo wadau mbalimbali hawakutegemea kutokea.

Mwenyekiti wa  chama hicho  Hamza Makonyi amesema hawako Tayari hawako   tayari  kuingia  mkataba na Kampuni ya Tumbaku ya Mkwawa kwa kuwa  bado wanawadai malipo ya fedha ya ununuzi wa Tumbaku ya msimu uliopita na uamuzi wa kuikataa kampuni hiyo  ulitolewa na wakulima wa   chama hicho kwenye  mkutano mkku uliofanyika tarehe  29/7/2023na barua walisha mwandikia  mkurugenzi wa bodi ya Tumbaku Tanzania .

Meneja wa Bodi ya Tumbaku Mkoa wa Katavi amekili nakala ya barua hiyo ingawa hadi sasa  hajapokea  barua au maelekezo yoyote  juu ya majibu ya   barua yao hiyo .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages