Barabara ya Ilangu Busondo ikiwa katika muonekano |
Na Paul Mathias,Tanganyika.
Wananchi katika Kata ya Ilangu Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameipomgeza Serikali kupitia Viongozi wa Kata pamoja na Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini Tarula Wilaya ya Tanganyika kwa kuanza kuifungua Barabara ya Ilangu Busondo kwa Kiwango cha Changalawe ili kuchochea ukuaji wa Uchumi kwa wananchi hao.
Diwani wa Kata ya Ilangu Sadiki Agustino alipotembelea Barabara hiyo ambayo inaendelea kutengenezwa |
Wananchi katika Kata ya Ilangu Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wameipomgeza Serikali kupitia Viongozi wa Kata pamoja na Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini Tarula Wilaya ya Tanganyika kwa kuanza kuifungua Barabara ya Ilangu Busondo kwa Kiwango cha Changalawe ili kuchochea ukuaji wa Uchumi kwa wananchi hao.
Wananchi
hao wamebainisha hayo wakati wakizungumza kwa nyakati tofauti kuhusu kuanza
kufanyiwa Matengenezo barabara hiyo yenye urefu wa Km 31 ambayo itaunganisha
Kata hiyo na Wilaya ya Uvinza.
Mradi
huo uliiibuliwa na wananchi wa Kata hiyo Mwaka 2018 kwa Kwa kushirikiana na
Diwani wa Kata hiyo Sadiki Agustino kujitolea kusafisha eneo hilo la barabara
kwa lengo kufanikisha shughuli za uchukuzi kwa wananchi hao.
Mbazo
mtima ameishukuru Serikali kwa kuanza Matengenezo kwa kiwango cha Kifusi ikiwa
ni ishara ya kuifungua barabara hiyo ambayo wananchi wa Kata ya Ilangu
wanaihitaji kwaajili ya shughuli za kiuchumi.
Amina
Joel Mkazi wa Kijiji cha Ilangu amesema kuwa ili kuwa inawalazimu kuzunguka KM
68 Kufika uvinza lakini kuanza kufunguliwa kwa Barabara hiyo watatumia Muda
mfupi kufika uvinza ambapo ni Jirani kutoka eneo hilo.
Diwani
wa Kata ya Ilangu Sadiki Agustino ameeleza kuwa Mwaka 2018 kwa kushirikiana na
wanachi walianza kwa Pamoja kuibua mradi huo kwa kufyeka na kusafisha huku
wakiwa na imani ya kwamba Serikali itaona jitihada zao.
Katika
hatua nyingine diwani huyo ameishukuru serikali kupitia Wakala wa barabara za
Mjini na vijijini Tarura Wilaya ya Tanganyika kuanza kuitengeneza
Brabara hiyo kwa Kiwango cha Kifusi.
‘’Mwaka
jana serikali ilileta Shilingi Milioni 90
za kufungua Kilomita 9 na mwaka huu wamepatiwa shilingi milioni 200
kwaajili ya kumalizia ufunguzi wa barabara hiyo ya Ilangu Busondo ambapo
Wakandarasi wanaendelea na kazi kwa usimamizi wa Tarura anasema Diwani Sadiki
Agustino.
Meneja
wakala wa barabara za Mjini na Vijijini Tarura wilaya ya Tanganyika Mhandisi
Noalsco Kamasha amesema kuwa hadi sasa wamepokea Kiasi cha shilingi miloni 400
na tayari wapo katika mchakato wa kuanza kutengeneza Madaraja na
Makalavati kwa Mwaka huu wa
fedha.
Amesema
kuwa barabara hiyo imeanza kufunguliwa mwaka jana na mwaka huu wameanza
kumalizia kufungua barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 31.