NAIBU WAZIRI WA UJENZI AWAONYA WANAO HARIBU MIUNDO MBINU YA BARABARA


Naibu  Waziri wa Ujenzi  Godfrey Kasekenya  akipokea  maelezo   Eng  Albert  Raizer Meneja  msimamizi    mkazi wa  mradi wa  barabara ya    Vikonge  hadi Luhafwe ya   maendeleo ya ujenzi wa  Barabara inayojengwa kwa kiwango cha  lami yenye urefu wa kilometa  25 kutoka  Vikonge  kwenda Luhafwe kuelekea   Mkoani  Kigoma inayounganisha Mikoa ya Katavi na Rukwa ujezi unaofanywa na Kampuni ya Kichina ya  CHICO  ambapo Naibu Waziri amewaagiza TANROADS Mkoa wa Katavi wahakikishe wanasimamia mradi huo kwa karibu .


Na Walter Mguluchuma,Katavi

Naibu  Waziri wa Ujenzi  Godfrey  Kasekenya amewaonya watu wenye tabia ya kuhalibu miundo mbinu ya  barabara  kwa kulima kando ya barabara kupitisha  wanyama  barabarani  na wanaoiba alama za barabaran waache tabia hiyo mara  moja  kwani wanaofanya hivyo watambue kuwa wanaihujumu Serikali

Naibu  Waziri wa Ujenzi God frey  Kasekenya  akitowa maelekezo  kwa uongozi wa TANROADS   Mkoa wa Katavi kuhakikisha   ujenzi wa  daraja la  mto Kavuu linalounganisha  mji mdogo wa  Maji Moto naI  inyonga ambalo ndio tegemeo kubwa kwa wasafiri wanaosafiri kutoka katika Mikoa ya  Songe      na  Rukwa kwa ajiri ya kwenda Kanda ya Ziwa  wahakikishe linakamilika kabla ya mvua kuanza kunyesha ili barabara hiyo isiweze kufungwa na watu kushindwa  kusafirisha mazao yao  ujenzi  wa daraja hilo unagharimu zaidi ya bilioni moja ambapo hapo awali daraja hilo  lilikuwa la vyuma

Naibu  Waziri wa Ujenzi  Godfrey  Kasekenya amewaonya watu wenye tabia ya kuhalibu miundo mbinu ya  barabara  kwa kulima kando ya barabara kupitisha  wanyama  barabarani  na wanaoiba alama za barabaran waache tabia hiyo mara  moja  kwani wanaofanya hivyo watambue kuwa wanaihujumu Serikali

Agizo hilo amelitoa  wakati wa ziara  yake   ya siku mbili aliyoifanya Mkoani Katavi ya kukagua maendeleo Miundo  mbinu  ya barabara zinazoendelea kutekelezwa kayika  Mkoa wa Katavi inayosimamiwana  Wizara ya  Ujenzi    alipokuwa akikagua  ujenzi wa barabara inayojengwa kwa kiwango cha  yenye urefu wa kilomita 25 kutoka Vikonge Mkoani Katavi kuelekea Uvinza Kigoma .

Kasekenya amebainisha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiharibu  miundo mbinu ya barabara  kwenye maeneo wanayolima mipunga kwa kufungulia  maji kwenye majaruba  ya mpinga na kuyaekekezea barabarani  na kupitisha  mifugo barabarani   na kusabisha  uharibifu wa barabara i .

amesema kumekuwepo pia na uharibifu wa  alama za barabarani na wizi wa   alama za barabara  jambo ambalo  ni hatari  kwa watumiaji wa vyombo  vya moto na watembea kwa miguu kwani kunaweza kusababisha ajari na watu kupoteza maisha .

 Naibu Waziri wa Ujenzi  Godfrey Kasekenya  akikagua ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 50 kutoka  Kibaoni hadi sitalike  wakati wa ziara yake Mkoani Katavi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara zinazoendelea kujengwa Mkoani Katavi

amewataka watu wanye tabia hiyo waache mara moja kwani Serikali  imefanya kazi kubwa ya kutengeneza miundo mbinu hiyo  na Wizara ya ujenzi haiku  tayari kuona uhalibifu huu unaendela  kwa kuwa kufanya uhalibifu wa miundo mbinu  ni  kuhujumu nchi.

Akizungumzia barabara ya Luhafwe  kwenda  Kigoma inayoendelea kujengwa kwa kiwango cha lami  alisema kuwa yatari wameisha anza kujenga na zipo kilometa 39 kuanzia Mpanda  hadi Vikonge zipo tayari  na sasa ni  Vikonge  hadi Luhafwe lakini   mkandarasi huyo  wa Kampuni ya Kichina  ya CHICO ameisha saini  mkataba mwingine wa kilometa 37 zitakazofika hadi Mishamo  akiwa  anaelekea Kigoma .

amefafanu kuwa  zimebaki kilometa 101 barabara hiyo itakuwa imekamilika kabisa hadi Uvinza  hata hivyo  Rais    Samia  Suluhu  Hassan  ameisha fanya mazungumzo na Benki ya Afrika za kumalizia hizo kilomeata 101 na mazungumzo yapo katika hatua za mwisho .

Kesekenya  amemusisitiza Mkandarasi  na  msimamizi  mshauri wa mradi huo  kuwa watambue kuwa   hiyo ni barabara kubwa  na inapitisha magari mengi makubwa  na mizigo  na tukijua kuwa  moja ya mikoa inayozalisha mazao mengi ni Mkoa wa Katavi  na hata Kigoma  hivyo wakati   matengenezo hayo ya kiwa yanaendelea wahakikishe  barabara hiyo inaendelea kupitika katika kipindi chote cha masika.

amewataka   TANROADS  Mkoa wa  Katavi kuhakikisha wanamsimamia  mkandara huyo kwa karibu   ili barabara ijengwe kama ambavyo ilivyo sanifiwa  ili tusitegemee barabara kuweza kufaei kabla ya muda wake  ikitokea hivyo TANROADS watakuwa  wameiangusha  Serikali kwa kushirikiana na  mkandarasi .

Meneja Msimamizi wa  Mradi wa Barabara  hiyo  Mhandisi Albert  Raizer alisema  Ujenzi wa   barabara ya  vikonge     hadi  Luhafwe  yenye urefu wa kilomeata 25 ni  utekelezaji wa moja ya ahadi  za Rais  Mkoani Katavi  kwakuwa barabara hiyo ni   kiunganishi kati ya  makao  makuu ya  Mkoa wa Katavi na Kigoma .

Ujenzi wa barabara hiyo unagharamiwa na  fedha za Serikali ya Tanzania  kwa asilimia mia moja  na itagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 35,638,514,918.00 zikijumlisha na kodi zote  na ushuru isipo kuwa VAT  na tarehe  awali  ya  kumaliza   mradi ni  22 Desemba 2023.

Mhandisi  Raizer  alisema  mpaka sasa  hakuna changamoto  kubwa   kuhusiana na mradi huo  ukiondoa changamoto ya mvua ambayo inafahamika wakati wa kipindi cha masika .

Mkazi wa Kijiji cha  Luhafwe  John Masanja  ameishukuru  Serikali kwa kuona umuhimu wa kutengeneza barabara hiyo ambayo ni mkombozi kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi na Kigoma na kwa  nchi za Burundi DRC  na Rwanda .

Kwa   wananchi itasaidia pia kuwapunguzia gharama za usafiri wanapokuwa wanahitaji kwenda sehemu nyingine kwa kupitia barabara na alitowa mfano  kutoka kwenye kijiji chao hadi makao makuu ya Mkoa wanatozwa nauli ya Tshs 7000 kwa umbali huo wa kilometa 70.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages