DC : ''JAMILA UJENZI WA SEKONDARI YA WASICHANA UKAMILIKE KWA WAKATI''

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akitoa maelekezo ya kiutendaji kwa Wasimamizi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana  Maalumu inayojengwa katika Kata ya Kapalala Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi alipotembelea mradi huo.

Na Paul Mathias,Mpanda

Mkuu wa Wikaya ya Mpanda Jamila Yusuph amesema Wilaya ya Mpanda itahakikisha Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Maalumu ya Wasichana inayojegwa  Katika Kata ya Kapalala Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi inakamilika kwa wakati ilia ianze kupokea wanafunzi Mnamoa January 2024.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph [katikati] akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana  maalumu katika halamashauri ya Nsimbo

Mkuu wa Wilaya ya ya Mpanda Jamila Yusuph amesema Wilaya ya Mpanda itahakikisha Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maalumu ya Wasichana inayojegwa  Katika Kata ya Kapalala Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi inakamilika kwa wakati ilia ianze kupokea wanafunzi Mnamo January 2024

Ameyasema hayo wakati alipotembelea na kujionea Mwenendo wa Ujenzi wa Shule hiyo ya Wasichana Maalumu  ambapo serikali imeleta Shilingi Bilioni Tatu kwaajili ya ujenzi wa Shule hiyo ya Sekondari  ya Wasichana  maalumu  kwa Wasichana.

‘’tunamshukuru sana Rais Dk Samia Suluhu Hassan Mradi huu niwakimkoa macho yote ya mkoa yapo hapa kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati na thamani ya Fedha inaonekana Sisi kama Wilaya ya Mpanda tutahakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati ili ifikapo January 2024 wanafunzi waanze kutumia Miundombinu hii’’ anasema Jamila

Baadhi ya Muonekano wa Majengo ya Madarasa ya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maalumu inajengwa katika Kata ya Kapalala Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya ametaka kasi ya ujenzi iongezeka kwa kutambua umuhimu wa Shule hiyo kwa manufaa ya Halmashauri ya Nsimbo  na Wilaya ya Mpanda kwa ujumla.

‘’tumefika hapa tumetembelea na kukagua Majengo ya haya kwa macho tumeona Mradi huu unaviwango vinavyotakiwa nimwagize Mkurugenzi kupitia watalamu wake kuhakikisha mradi huu unaendana na thamani ya fedha mradi ukamilike kwa wakati ili ifikapo January 2024 Majengo haya  yaanze kutumiwa na wanafunzi’’amesisitiza Mkuu huyo wa Wilaya.

Katika kuhakikisha upatikanaji wa Maji unakuwa wa Uhakika shuleni hapo Mkuu huyo wa Wilaya ya Mpanda amewaagiza Ruwasa kuhakikisha wanakamilisha Uchimbaji wa Kisima ili huduma ya Maji iwe ya uhakika baada ya mradi kuanza kutumika.

''Niwaagize Ruwasa kuhakikisha hawa DCCA wanakamilisha kazi ya uchimbaji wa Kisima ambao wameanza kuchimba Halmashauri tayari wameshatoa fedha na tume ona kutokana na maji kutokuwa ya uhakika kuna baadhi ya maeneo mradi upo chini kutokana na ukosefu wa Maji nimtake meneja wa Ruwasa Mkoa kuhakikisha kazi ya kuchimba kisima kwenye eneo hili unakamilika fedha zote walishapewa ''amesema Dc Jamila

Mohamed Ramadhani Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Nsimbo amesema kuwa watahakisha kuwa mradi huo wa unakamilika kulingana na muda wa waliopewa na wizara ya Tamisemi ya kuhakisha ujenzi unakamilika ifikapo 31/12/2023 unakamilika .

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Nsimbo Mohamed Ramadhani akielezea Maendeleo ya Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana inayojegwa kwenye Halmashauri hiyo.

Ramadhani amesema kuwa tayari wameanza mpango mkakati wa kuhakikisha Vitanda kwaajili ya Mabweni na Madawati vinapatika ili wanafunzi wanapoanza masomo wakute miundombinu hiyo imekamilika.

‘’mkakati wetu sasa ni kupata Madawati pamoja na Vitanda kwaajili ya Mabweni maana bila madawati na Vitanda kwenye Mabweni hatuwezi kuanza kutumia hii Shule hilo tayari tumeshanza kulifanyia kazi’’ anasema Mohamed

Pamoja na hayo ameeleza kuwa tayari wamesha chimba kisima kwaajili ya kuhakikisha huduma ya maji inapatikana wakati wa Ujenzi lakini pia badaa ya ujenzi utakamilika ambapo wanafunzi watamia maji hayo kwaajili ya Matumizi yao ya kila siku.

Katika zaiara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ametemmbelea Shule ya Sekondari Lupembe ambayo ilipatiwa fedha za Serikali kiasi cha Shilingi Milioni 603 kwaajili ya kuongeza miundo mbinu ya Madarasa pamoja na Majengo mengine.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages