Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Kagwira wakiwa katika mshangao kufuatia watu wawili kuuawa kwa Kuchijwa kwenye Kijiji hicho |
Na Paul Mathias,Tanganyika.
Watu wawili wakazi Kitongoji cha Imbambe Kijiji Cha Kagwira Kata ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wamekutwa wamefariki Dunia kwa Kuchijwa na kutupwa Pembezoni mwa Barabara.
Shira benedictor Mwenyekiti wa Kijiji cha Kagwira akielezea tukio hilo. |
Watu wawili wakazi Kitongoji cha Imbambe Kijiji Cha Kagwira Kata ya Kabungu Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wamekutwa wamefariki Dunia kwa Kuchijwa na kutupwa Pembezoni mwa Barabara.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea usiku wa
Kuamkia leo Kijijini hapo huku wananchi hao wakilaani kitendo hicho cha unyama
kilichofanywa na wauaji hao.
Waliouawa kwa Kuchijwa katika
tukio hilo ni Atanas Allyen Miaka 23 mkazi wa Kijiji cha Kabungu pamoja na
Katalina Yuna Mkazi wa Kabungu miaka 21.
Wakazi wa Kijiji cha Kagwira wakiwa katika eneo la tukio |
‘’Nimtu na jirani yake
waliouawa wanaishi kitongoji cha Ibambe
tumepata taarifa hii kwa mshtuko sana tunaomba Jeshi la Polisi lifanye
uchunguzi’’ anasema mwenyekiti huyo
Ziada mnayahe afisa Mtendaji wa
Kijiji cha Kabungu amesema kuwa alipata taarifa ya tukio hilo kwa njia ya simu
majira ya usiku ambayo alipigiwa na wananchi juu ya tukio hilo la watu kuuawa
kwa Kuchijwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa
Kaster Ngonyani amekili kuwepo kwa tukio hilo na tayari jeshi hilo linawashikilia
watu
wawili kwaajili ya mahojiano juu ya Tukio hilo.
Ngonyani ameeleza kuwa tukio
hilo linasura ya Wivu wa Kimapenzi kwani wamebaini mmoja ya marehemu alikuwa
nawasiliana na watu ambao walikuwa ni wapenzi wake.
Katika hatua nyingine amesema
jeshi hilo limeanza kufanya upelelezi wa kina juu ya tukio hilo.