KATAVI KUADHIMISHA WIKI YA UTALII KWA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrimdoko akizungumnza na waandishi wa habari ofisini kwake

Na Walter Mguluchuma,Katavi

Mkoa wa Katavi  wameandaa maadhimisho ya wiki ya mwana Katavi  kwa muda wa  siku saba  zitakazomsaidia mwananchi  wa Mkoa wa Katavi  na Wanzania kwa ujumla  kuweza kujifunza  mbinu mbalimbali  za kisasa  za kuhusu sekta mbalimbali   na  kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Katavi .

Mkoa wa Katavi  wameandaa maadhimisho ya wiki ya mwana Katavi  kwa muda wa  siku saba  zitakazomsaidia mwananchi  wa Mkoa wa Katavi  na Wanzania kwa ujumla  kuweza kujifunza  mbinu mbalimbali  za kisasa  za kuhusu sekta mbalimbali   na  kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Katavi .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema Mkoa wa Katavi  umeaandaa wiki maarufu inayojulikana  mwana Katavi  ukiwa ni  utaratibu huo  ambao utumika kwenye siku ya wiki hiyo kumwelimisha  mwananchi wa Mkoa wa Katavi na Watanzania  kuhusiana na mambo mbalimbali .

Wiki hiyo itaanza  Oktoba 25 hadi Oktoba  utaaribibu huu ulionzishwa na Mkoa wa Katavi  ambayo  ndani ya wiki nzima  kutakuwa  na  shughuli mbalimbali  zitakazo kusaidia  wananchi kwenye mambo mbalimbali lengo  kwa kujifunza  maswala ya sekta mbalimbali  na kutangaza utalii.

Alizitaja baadhi ya sekta hizo kuwa ni kilimo ,ufugaji  uvuvi ,uwekezaji ,madini   michezo na sekta inayohusiana na utalii  wa vivutio vyote vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Katavi  baadhi ya vivutio  hivyo  ni  Hifadhi ya Taifa ya Katavi    maporoko ya maji Nkondwe, chem chem ya   maji moto ,Mto  mapacha  andaki  lililotumiwa na Wabeligiji wakati wa vita vya Dunia

Mrindoko alisema   kauli mbiu  ya wiki hiyo   ni  inasema  Katavi yetu  talii  wekeza imalisha uchumi kwa maendeleo endelevu  na wataendelee na kauli mbiu hiyo muda wote wa wiki hiyo  ili kuwahamasisha wananchi  kuendelea kujishughulisha na shughuli za kiuchumi  kwa kuleta maendeleo endelevu .

amefafanua kuwa kila siku kutakuwa na sekta kadhaa  zinazohusika na tukio la siku  ambapo  zitapewa  kipaumbele   katika kueleza shughuli zake  na kueleza tekinojia mbalimbali zinazotumika katika uzalishaji wa biashara ,ujasiliamali utalii  na   nyinginezo .

amesema  Halmashauri zote zimejiandaa  kushiriki  kwenye wiki  hiyo kwa kushiriki  kikamilifu na   zimepanga kuleta wananchi wengi zaidi kutokana na hamsa kubwa ambayo imefanywa hadi sasa.

Mwaka 2022 walifanya kwa mara ya kwanza na waliweza kupata mafanikio kwa  kushilikisha wananchi na wadau  pamoja na taasisi za kifedha .  na wananchi walishiriki kwa wingi na kuweza kujifunza kwa kupatiwa elimu mbalimbali .

Nae  Mkazi wa Manispaa ya Mpanda John Sanane amesema kufanyika kwa wiki hiyo ni furusa kubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi na Wanzania kwa ujumla kwa kuweza kufahamu  furusa zilizopo  katika Mkoa huu.

Pia ni nafasi kwa Mkoa kuweza kutangaza vivutio vyake kwani licha ya kuwa na vivutio vingi ndani ya Mkoa huu bado  havija fahamika vya kutosha  hivyo  wiki hiyo ndio wakati wa kutangaza zaidi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages