DC MLELE TOKOMEZENI UVAMIZI WA MISITU YA HIFADHI

 

Mkuu wa wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi,Majid Mwanga akiwa na baadhi ya maofisa wa TAWA kwenye ukaguzi wa mazingira.

Na. Kibada Ernest –Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino.

MKUU wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga  amewataka wananchi waliovamia misitu ya hifadhi na kukata miti hivyo kuacha mara moja na   kuondoka  na iwapo watakaidi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

MKUU wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga  amewataka wananchi waliovamia misitu ya hifadhi na kukata miti hivyo kuacha mara moja na   kuondoka  na iwapo watakaidi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kauli hiyo imetolewa   jana oktoba 20 na  Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga  baada ya kufanya ziara ya kushitukiza na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya kutembelea na kujionea halisi ya uharibifu uliofanyika katika maeneo hayo,

Hivyo  ikamlazimu kupiga marufuku  uharibifu unaofanywa wa kukata miti hovyo na kuwaagiza wakala wa huduma za mistu TFS kuhakikisha mistu inalindwa na mtu yeyote anayetaka kukata miti lazima awe na kibali na afuate utaratibu.

Aidha amewataka Wananchi wa Wilaya hiyo wakiwemo wageni kutoka maeneo mengine nchini kuwa mabalozi ili kutokomeza uvamizi wa misitu  ambayo iko hatarini kutoweka kutokana na   shughuli  za kilimo, ufugaji,kukata miti    na uchomaji wa moto kiholela hali ambayo inatishia   kuteketea kwa mistu huo.  

Mkuu wa wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi,Majid Mwanga akiendelea na ukaguzi wa mazingira yaliyoharibiwa baada ya kuvamiwa na baadhi ya wananchi.

Majid ameeleza kuwa uvamizi huo umesababisha baadhi ya  mistu kuteketea hali ambayo inatishia   kukauka  kwa vyanzo vya maji na  katika wilaya hiyo.

Katika hatua nyingine  ameiagiza Wakala wa  Huduma za Mistu,Tanzania TFS  Katika wilaya hiyo kuhakikisha wanashirikiana na Idara  vyombo vingine  pamoja na Idara ya Usimamizi wanyamapori TAWA    na wananchi ili kunusuru misitu hiyo ambayo iko hatarini kutoweka kutokana na uvamizi huo unaofanyika kutokana na shughuli za kibinadamu.

“Hii mistu inatakiwa ihifadhiwe,  hii mistu ndio uhai ikihifadhiwa vizuri inasaidia  vyanzo vyetu vya maji”alisema Mkuu wa Wilaya.

Baadhi ya nyumba za asili zilizojengwa kwenye maeneo mbalimbali ya uhifadhi na kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa mazingira.

Mkuu huyo wa Wilaya Mwanga amesema watu wanakata miti bila mpangilio na amejionea mwenyewe watu wanakata miti hovyo kwa shughuli zao kwa kujipatia kipato bila kuzingatia  utaratibu .

Kwa sasa Suala la uhifadhi lazima TFS  mhakikishe ninyi pamoja na vijiji vinavyozunguuka mistu ya hifadhi mzungumze lugha moja wote muwe kitu kimoja ili kuhifadhi mistu hii..

Amepiga marufuku wananchi wa wilaya hiyokukata miti  bila kuwa na kibali "Hakuna kukata miti bila kibali hata kama mti ni wa kwako uliupanda wewe au uko kwenye shamba lako, lazima hatua zote zifanyike kuanzia ngazi ya kijiji na hata ukikata mti mmoja lazima upate kibali".

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages