George Mwigulu na Paul Mathias,Katavi
Wananchi wa mkoa wa Katavi
wameombwa kuacha kuwapa nguvu na fursa watu wanaodhaniwa kuwa na uwezo wa kufichua wachawi maarufu kwa
jina la Kamchape au lambalamba kwani wanafanya mambo yanayokiuka sheria za
nchi.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi [CCM] Taifa Daniel Chongolo akivishwa Sikafu ya ukaribisho alipofika katika viunga vya Ofisi ya Chama cha Mapinduzi [CCM] Mkoa wa Katavi |
Wananchi wa mkoa wa Katavi wameobwa kuacha kuwapa nguvu na fursa watu wanaodhaniwa kuwa na uwezo wa kufichua wachawi maarufu kwa jina la Kamchape au lambalamba kwani wanafanya mambo yanayokiuka sheria za nchi.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu
Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Daniel Chongolo baada ya kupokea
taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katika ofisi ya Mkoa ya
Chama hicho ambapo Mrindoko alisema kuwa kitendo hicho kiliweza kuhatarisha
amani na usalama wa mkoa hususani katika mwambao wa ziwa Tanganyika.
Chongolo alisema kuwa imani za
kishirikina ni umasikini na kama jamii inapaswa kujifunza ni kuagalia kwa watu
wengi wanaoamini katika ushirikina kwani wanaami kwenye ndoto ambazo kutekelezeka
kwake ni ngumu “Achaneni kuendekeza
mambo yanayoweza kutoa taswira ya umasikini kwa mkoa wetu” amesisitiza.
Katibu Mkuu huyo amesema ni
lazima mkoa utoke kwenye kufikiri mambo kwa njia rahisi kwa sababu maendeleo
hayapatikani nduba,kupuliza,kupiga lamli na kutengeneza mambo lahisi kwenye
mambo yanayohitaji kufuata utaratibu.
“Ukiona watu wa namna hiyo wala usipate shida angalia wanaishi kwa
masharti mtu anaweza kuwa nang”mbe 1000 lakini kwake haruhusiwi kula nyama nusu
kilo kwa wiki sababu masharti yanayotolewa na watu wanaopenda
kupulizapuliza…achaneni na maisha hayo kwani niafadhari uwe na ng’ombe 10 uwe
na uhuru wa kula nyama” Amesema Katibu Mkuu huyo.
Aidha katika hatua nyingine
Chongolo amewaletea salama za rais Samia Suhulu Hassain ambapo alisema atanabua
matatizo ya watu wa Mkoa wa Katavi na kama chama wanakazi kubwa ya kusimamia
ilani ya chama hicho ili kuweza kuondoa changamoto hizo.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa,Daniel
Chongolo yupo kwenye ziara ya siku 5 katika Mkoa wa Katavi ambapo atakangua
utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo sambamba na kuangalia
uhai wa chama hicho.
Zuena Rashidi,Mwananchi na mkazi
wa mtaa wa Kawajese ameshukuru ujio wa katibu mkuu huyo kwani anaamini kuwa
utakuwa sehemu ya kusikiliza kero za wananchi na kufanyiwa kazi kwa muda
muafaka.
Amesema kuwa CCM ilipewa dhamana
ya kuongoza serikali hivyo wanapaswa kuwajibika kwa kutatua kero ambazo
zimekuwa kikwazo kwa usitawi wa uchumi.
Jumanne Magaga anasema kuwa mkoa
wa Katavi unachangamoto nyingi hususani ya migogoro ya mashaba,mipaka kati ya
wananchi na hifadhi mbalimbali zilizopo mkoani Katavi ambapo kama Katibu Mkuu
huyo ataweza kuzishughulikia wataweza kuishi kwa amani.
Mwananchi huyo ameeleza kuwa Katibu
Mkuu anapaswa kuwaonya watendaji wa serikali ambao wamekuwa kikwazo cha wananchi
kwenye kufanikisha maendeleo yao kwa kuwa wabadhirifu na wapenda rushwa.