WAIOMBA SERIKALI KUREJESHA KWA WAKATI MIKOPO YA ASIMILIA KUMI.

 

Stella  Paul,Mkazi wa mtaa wa Misukumilo akiendelea na kazi yake ambayo humpatia kipato cha fedha za kujikimu.


Na George Mwigulu, Katavi.

BAADHI ya wanawake wajasiliamali wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameiomba serikali kuharakisha mchakato wa mfumo mpya wa utoaji wa mikopo  kwa wanawake,vijana na watu wenye ulemavu ili waweze kuendelea kukuza biashara zao zitakazo chochea ukuaji wa uchumi na maendeleo.

Marry Daniel akiendelea na majukumu yake ya kazi .

Serikali kwa muda wa mrefu sasa imesitisha zoezi la utoaji wa mikopo hiyo kupitia halmashauri zote nchini ambazo hutenga asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili kukopesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu baada ya kubaini ubadhirifu na wizi wa fedha hizo huku baadhi ya wakopaji wengine kushindwa kurejesha mikopo hivyo serikali kuwa kwenye mchakato wa kutumia mfumo mpya unaotajwa kuwa ni kibenki.

Wakizungumza kwa wakati tofauti 8, October 2023 baadhi ya wanawake hao katika mitaa ya Misukumilo, Kawajense na Tulieni Manispaa ya Mpanda wamesema wamekuwa wahanga wa kukosa mikopo ambayo iliwasaidia kukuza biashara zao na kuinua uchumi wa familia.

Christina Michael, Mjasiliamali na mkazi wa mtaa wa Tuleni Manispaa ya Mpanda anasema kuwa  serikali kupitia ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa fedha za serikali wahusika wote wa wizi wa fedha za mikopo walitajwa hivyo anashangaa kuona bado wanamaisha mazuri ili hali wao bado wanahangaika na umasikini.

Mjasiliamali huyo ameeleza kuwa fedha za mkopo walizokuwa wakipata ziliinua zaidi pato la kila siku na kuinua maisha yao kwa ujumla “Tuliweza kusomesha watoto wetu, kugharamia matibabu, mavazi na kuboresha makazi yetu” amesema Christina.

Nyumba ya Marry Daniel Mkazi wa Mtaa wa Misukumilo ambayo ameijenga kutokana na  kazi yake ni kutengeneza kokoto ambazo zinatumika kwenye ujenzi.

Suzana Paul, Mkazi wa mtaa wa Kawajese anasema licha ya nia ya serikali kuwa ni njema ya kusitisha mikopo lakini imegeuka kuwa kero kwa sababu hawana sehemu nyingine ya kukopa fedha kwa riba nafuu.

Amesema uendeshaji wa biashara zao umekuwa mgumu huku hali ya maisha ikiendelea kudidimia hivyo kuiomba serikali kuharakisha mchakato wa kurudisha huduma ya utoaji wa mikopo.

Marry Daniel, Mkazi wa mtaa wa Misukumilo mjasiliamali na mama wa watoto wanne amesema kuwa wanawake wengi wegeukia shughuli za kugonga mawe ya kutengeza kokoto zinazotumiwa kwenye ujenzi mbalimbali ili mradi waweze kuongeza kipato chao.

Ameeleza kuwa baada ya kutelekezwa na mume wake hakuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kujinga na wanawake wengine ambao kazi yao ni kutengeneza kokoto.

“Ndoo moja ya lita 10 yenye ujazo wa kokoto ni Tshs 500 tuko hapa na kikundi chetu kinaitwa HAPA KAZI TU hali sio nzuri kwa sababu wengi wetu hapa hatuna waume ambao tunaweza kusaidizana kufanya majukumu ya kuhudumia familia” Amesema Marry ambapo amesisitiza kama mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu itarejeshwa kwa wakati itawasaidia.

Stella Paul, Mwanakikundi wa HAPA KAZI TU amesema kuwa licha ya changamoto za kifedha na kuhudumia familia anazopata lakini kazi yake ya kutengeneza kokoto kwa kushirikiana na mume wake ameweza kujenga nyumba na kuvuta umeme.

Ameeleza kuwa ili kufikia usawa wa kijisia kwenye uchumi serikali ameiomba kuendelea kuwasaidia wananchi hususani wanawake kwa kuandaa warsha za kuwakomboa kiuchumi sambamba na kuwawezesha kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumzia suala la mikapo wakati wa ziara ya kikazi ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Daniel Chongolo katika kikao cha ndani amesema kuwa serikali bado inampango wa kuendelea kutoa mikopo hiyo bali bado wanasubiria utaratibu mpya wa utoaji wa mikopo hiyo.

Mrindoko amewaomba wajasiliamali mbalimbali kuwa na uvumilivu wakati utaribu mpya unatengenezwa kwani serikali inatambua umuhimu mkubwa mikopo hiyo ambayo ni chachu kubwa ya maendeleo kwa makundi hayo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages