RC: KATAVI ATAKA ONGEZEKO UZALISHAJI ZAO LA PAMBA.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwananvua Mrindoko akiongea na wadau wa Kilimo cha Zao la Pamba.

Na Walter Mguluchuma,Katavi

Wadau wakilimo cha zao la Pamba katika mkoa wa katavi wameobwa kwendakusimamia kwa vitendo uzalishaji wa Zao la Pamba kwa Msimu Ujao 2023/2024 ili kuendana na Uwezo wa Kiwanda cha kuchakata zao la Pamba cha NGS kilichopo mkoani katavi.

Wadau mbalimbali wa zao la Pamba wakiwa katika kikao cha wadau wa zao la Pamba mkoa wa Katavi

Wadau wakilimo cha zao la Pamba katika mkoa wa katavi wameobwa kwendakusimamia kwa vitendo uzalishaji wa zao la Pamba kwa Msimu Ujao 2023/2024 ili kuendana na Uwezo wa Kiwanda cha kuchakata zao la Pamba cha NGS kilichopo mkoani katavi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wakati akifungua kikao kazi cha Wadau wa Kilimo cha Pamba Mkoa wa Katavi.

Amesema kuwa  kiwanda hicho kinauwezo wa kuchakata Milioni 50 za Pamba kwa msimu mmoja huku uzalishaji wa Mkoa ukiwa ni Milioni 7 kwa Msimu 2022/2023 ameeleza kuwa pamoja na ongezeko lililopo bado uzalishaji huo hauna tija kutokana na mahitaji ya Kiwanda.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kwa msimu ujao wa 2023/2024 mkoa wa katavi unatalajia kuzalisha  Kilo milioni 20 ambazo zitagawiwa kunzia ngazi ya Halmshauri hadi kata ili kufikia malengo hayo.

Katika hatua nyingine amesisitiza  uzalishaji wa  pamba  kwa msimu uliopitahaulingani na mbegu ambazo walichukua wakulima  kilo 8,772,100 mbegu  hizo ukizichanganua zilikuwa na uwezo wa kupandwa kwenye ekari 43, 605,000 ambazo  zilikuwa na uwezo wa kuzalisha kilo  17,442 000 lakini uzalishaji umekuwa ni kilo  7,649,410hali ambayo inaonyesha kuna upunguzu wa kilo zilizozalishwa na idadi ya mbegu walizosambaziwa wakulima.

Mrindoko amesistiza kuwa kwa msimu huu Amcos na  wataalamu wa kilimo wahakikishe  idadi ya  kiko za mbegu ziendanane  na lengo la uzalishaji na wala si vinginevyo  kwani   Mkoa wa Katavi bado unapokea mvua   zuri zinazofanya mazao yaweze kusitawi bila shida  hivyo kila mmoja atambue kuwa malengo ya uzalishaji kwa msimu huu ni kilo milioni 20 kwa Mkoa wa Katavi na kwa msimu ujao uzalishaji uongezeke na kufikia kilo milioni 40.

Amewaagiza wakuu wa Wilaya wote wa  wilaya za Mkoa wa Katavi kuhakikisha wanafatilia kwa karibu  usambazaji wa mbegu za pamba ili kuweza kudhibiti upotevu  ili kuhakikisha mbegu zinazokuwa zimetolewa  zote  zina kwenda shambani .

Mkurugenzi wa  kIwanda  cha kuchakata pamba cha NGS  Njalu  Silanga  aliwatowa hofu wakulima kuwa NGS wataendelea  kuwalipa wakulima wa pamba kwa wakati  ili  kuweza kufikia  malengo  ya uzalishaji .

Aliomba tafiti ziendelee kufanyika  kwani yeye alivyozunguka kwenye  vijiji  mbalimbali vya Mkoa wa Katavi hajaona kama mkulima wa pamba anaitaji alime kwa kutumia mbole  ekumbukwe kila gharama inayoongezeka inapelekwa kwa  mkulima  hivyo wataalamu wetu waendelee kufanya tafiti  ili wajuwe ni maeneo yapi yanayohitaji mbolea .

Nae Katibu  Tawala  Msaidizi  Uchumi na Uzalishaji  Neemia  James  ameshukuru Bodi ya Pamba  namna ambavyoinashirikiana na Mkoa wa  Katavi katika kuzalisha tija ya uzalishaji wa zao  la Pamba   

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages