WAFANYABIASHARA KATAVI WAPATIWA ELIMU YA BIASHARA NA NMB

Kaimu Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Magharibi Gadiel Sawe akizungumnza na waandishi wa habari kando ya semina hiyo ya wafanyabiashara mkoa wa Katavi wanaotumia Benki ya NMB kwenye Biashara zao[Picha na Paul Mathias]


Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Benki ya NMB Mkoa wa Katavi imewakutanisha wafanyabiashara mbalimbali na kuwapatia Elimu juu ya Fursa mbalimbali za mikopo zinazotolewa na Benki hiyo    kupitia  NMB  BUSINESS  CLUB ambayo imekuwa kiunganishi kwa wafanya Biashara hao. 

Baadhi ya Wafanyabiashara Mkoa wa Katavi wakiwa katika Semina hiyo katika ukumbi wa Mikutano wa Mpanda Social Hall[Picha na Paul Mathias]

Benki ya NMB Mkoa wa Katavi imewakutanisha wafanyabiashara mbalimbali na kuwapatia Elimu juu ya Fursa mbalimbali za mikopo zinazotolewa na Benki hiyo    kupitia  NMB  BUSINESS  CLUB ambayo imekuwa kiunganishi kwa wafanya Biashara hao. 

Mafunzo hayo ya siku moja yaliowashirikisha  wafanya biashara   mbalimbali wakiwemo na wadau mbalimbali  kama vile Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Msajiri wa hati  Ofisi ya  biashara Manispaa ya Mpanda   na wadau wengine mbalimbali  yalifanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda .

Kaimu  Meneja  wa   Benki ya  NMB  Kanda ya   Magharibi  Gadiel  Sawe  amesema  lengo la kuwakutanisha wafanya  biashara hao ni kuwapatia  elimu  itakayowasaidia  kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi ili kuwawezesha  kujua  huduma  zinazotolewa kwenye ofisi mbalimbali   wanazofanya shughuli  zinazohusiana na biashara zao .

Mwenyekiti wa NMB BUSNES CLUB Mkoa wa Katavi Raymond Kamtoni[kushoto] akiongea Jambo na Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi Gadiel Sawe wakati wa Semina Hiyo. [Picha na Paul Mathias]

Lengo  jingine la  kikao hicho ni kuwataka wafanya biashara waweze  kutambuana  kwa kuweza kuuziana   bidhaa ambazo wanazalisha mfano mfanyabiashara aliyefika kwenye kikao hicho anauza   pembejeo   za kilimo  tayari mkulima   amejua kwenye kikao hicho zinapatikana wapi na mwingine mwenye nyumba ya kulala wageni  nae pia wafanya biashara  wamejua  mahali pa kufikia hivyo kikao hicho ni cha muhimu kwa kwa wafanyabiashara kuweza kufahamiana .

Sawe  amebainisha kuwa  watu waliowalenga kuwapatia elimu hiyo ni wafanya biashara wote  kuanzia wamachinga  wafanya biashara  waliwaacha ni wafanya biashara wale wakubwa  ambao wao nao   huwa wanautaratibu wa kuwapatia  elimu  bila kuwachanganya na wafanya biashara hao .

Makamu  Mwenyekiti wa   NMB   Business Club   wa   Mkoa wa Katavi Haidari  Sumry amesema  wao kamawafanya biashara wanaofanya  biashara na NMB kumekuwa na manufaa  makubwa sana   toka NMB  Business Club toka ilipoanzishwa katika Mkoa wa  Katavi .

Makamu Mwenyekiti wa NMB BUSNES CLUB Mkoa wa Katavi,Haidary Sumry akielezea namna Benki ya NMB ambavyo imekuwa ikiwasaidia kwenye Biashara.

Kwanza imesaidia  wafanyabiashara  wafanya biashara kukutana na wadau mbalimbali  wanaounganisha  biashara zao   kwa mfano TRA ,A rdhi na wawezeshaji mbalimbali yanayohusu  maswala ya biashara  wamesaidia sana wafanya biashara kujua namna ya kufanya biashara , kutunza kumbukumbu na kodi wanalipaje .

Hivyo kwa maana ya kufanikiwa wafanya biashara wamefanikiwa  pakubwa  na    NMB  nao wamefanikiwa  kwa kuweza kupanua wigo  kwa kuendelea kupata watu ambao wanajiunga kwenye  Benki yao  kwa kuendelea kupata watu wanaoendelea kupata mikopo NMB na benki hiyo kuendelea kuwa  benki inayochochea maendeleo ya Mkoa wa Katavi .

Sumry amesema  Nmb kwa sasa ni Benki  kubwa hapa nchini hivyo wajione kuwa wamekuwa wakubwa  wanachowaomba waangalie  ni vivutio gani ambavyo vinavyowasaidia wafanya biashara hivyo wanachoomba wafanya biashara kwa kuangalia  namna ya kupunguza liba .

Sasa hivi wafanya biashara wameisha elimika kwa kulipa madeni bila hata ya kupigiwa simu wanajua  kila mwisho wa mwezi kurejesha mikopo waone  kwa  kuwa kumekuwa na usalama huo wa marejesho  yao kwa hari      NMB  waone  nao namna  ya kupunguza  liba.

 Nae  mfanyabiashara  Issa  Idd Kapiligi duka la rejareja na wakala wa NMB   alisema wameudhuria  mafunzo hayo  ambayo hufanyika kila  mwaka  kwa wafanyabiashara wanao kopa NMB  yanayowasaidia  namna ya kufanya biashara  na kuendesha kwa ufanisi mkubwa ,

Kwenye mafunzo hayo wamejifuna mfumo mpya wa TAUSI wa kuomba leseni kwa njia ya  mtandao  elimu hiyo kwao imekuwa ni mpya na wameifahamu na pia wamefundishwa jinsi ya kupata hati za umiliki wa ardhimafunzo hayo yamewanufaisha .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages