Viongozi wa chama cha ACT wazalendo wakiwa katika mkutano huo
Na Jackson Gerald,Katavi
Chama cha ACT Wazalendo Jimbo la Mpanda Mjini
wamezidi kujiimarisha kwa kuweza kufanya uchaguzi wa kuwachagua
viongozi watakao kiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka
mitano ikiwa ni hatua ya kuendelea kujiimalisha
Chama cha ACT Wazalendo Jimbo la Mpanda Mjini wamezidi kujiimarisha kwa kuweza kufanya uchaguzi wa kuwachagua viongozi watakao kiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka mitano ikiwa ni hatua ya kuendelea kujimalisha
Uchaguzi huo wa kuwapata viongozi wa chama hicho katika
jimbo la Mpanda Mjini ulifanyika katika ukumbi wa Kanisa
Katoliki Jimbo la Mpanda na ulisimiwa na Amon
Simbabhaje kutoka ACT Wazalendo Taifa na na
uliwashirikisha wajumbe wa mkutano Mkuu kutoka Kata zote
zinazounda Jimbo la Mpanda Mjini .
Vingozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho ni
Anselimo Majani amechaguliwa kuwa Mwenyekiti , Cyril
Mshota Mshota Katibu , Juma Bileta Katibu Mwenezi
, Donatha Petro Mweka Hazina Feisal Hassan Mipango
na Uchaguzi , Juma Sanda Mwenyekiti Ngome ya Wazee ,
Anna Paulo Nyani Mwenyekiti Ngome wanawake
Abdalla Kang;ombe Mwenyekiti Ngome Vijana .
Wengine waliochaguliwa ni Habibu Bandya
Katibu Ngome Wazee, Specioza Kambulaya Katbu Ngome
Wanawake , John Mniko Katibu Ngome Vijana Idd
Mvano Mjumbe kamati ya uongozi Abdul Iddy
Nziguye Mjumbe kamati ya uongozi Fatuma Masoud
mjumbe kamati ya uongozi
A mewapongeza wajumbe wote wa kutoka kwenye Kata
zote ambao wameweza kujitokeza kwa wingi na kushiriki kwenye mkutano
huu mkuu muhimu wa kuwachagua viongozi watakao kiongoza
chama hicho .
Katibu wa ACT Wazalendo Joseph Mona amebainisha kuwa uchaguzi huu ni muendelezo wa chaguzi nyingine ambapo kwa mujibu wa tataribu za chama hicho uchaguzi kama huu utafanyika katika Majimbo yote yaliko katika Mkoa wa Katavi na kisha utafanyika uchaguzi wa kuwachagua viongozi wa ngazi ya Mkoa.