Kampuni ya ununuzi
wa Tumbaku ya PREMIUM ACTIVE Tanzania inayofanya kazi ya kununua
Tumbaku katika maeneo yanayolima Tumbaku katika Mkoa wa Katavi imetoa msaaada wa zaidi ya shilingi milioni 50 kwa ajiri ya sekta
ya elimu zitakazotumika katika kutengenezea madawati kwa shule za Msingi
na Sekondari .
Kampuni ya ununuzi wa Tumbaku ya PREMIUM ACTIVE Tanzania inayofanya kazi ya kununua Tumbaku katika maeneo yanayolima Tumbaku katika Mkoa wa Katavi imetoa msaaada wa zaidi ya shilingi milioni 50 kwa ajiri ya sekta ya elimu zitakazotumika katika kutengenezea madawati kwa shule za Msingi na SekondariMeneja Shughuli wa Kampuni ya Premium Tanzania Nico Roussos akielezea namna Kampuni hiyo imekuwa mdau wa Maendeleo katika mkoa wa Katavi.
Mfano wa hundi wa
fedha hizo imekabidhiwa n kwa mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi
Onesmo Busweru ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika na
imekabidhiwa kwa niaba ya kampuni ya Premium na Meneja shughuli
wa Kampuni hiyo Nico Rousss kwenye hafla ya makabidhiano
iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika .
Akikabidhi mfano wa
hundi hiyo Meneja shughuli wa Kampuni ya PREMIUM Nico Rousss
alisema kampuni hiyo imetowa kiasi hicho cha fedha
ambazo zitagawiwa kwenye maeneo ya Kata zote zinazolima Tumbaku ikiwa ni
katika sehemu ya kuchangia maendeleo katika maeneo yote yanayolima
Tumbaku katika Mkoa wa Katavi .
Amebainisha kuwa Kampuni hiyo licha ya kununua tumbaku wao ni sehemu kubwa sana ya wadau wa kuleta maendeleo katika Mkoa wa Katavi na ndio maana wameamua kutoa kiasi cha Tshs 50 300,000 katika sekta ya elumu kwa ajiri ya kutengeneza madawati ya shule za Msingi na Sekondari .
Katika
kufanikisha mchango huu kwenye jamii Kampuni hiyo
ilipokea maombi ya miradi ya kipaumbele kwenye kila Kata yenye
vyama vya ushirika vya Msingi vinavyofanya kazi na Kampuni ya
PREMIUM kwa hari hiyo sio rahisi kwa sasa kutimiza
miradi hiyo kwa wakati mmoja .
Amefafanua kuwa kwa sasa
Kampuni ya PREMIUM imweza kutowa kiasi hicho cha fedha kiasi cha
Tshs 50,3000,000 ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi tshs
31,800,000 ni kwa ajiri ya Wilaya ya Tanganyika Tshs Wilaya ya
Mpanda tshs 11 ,250,000 na Wilaya ya Mlele Tshs 7,220,000
hivyo kampuni hiyo wanayofuraha kubwa wa kuwa wadau waliorudisha faida
yao kwenye maendeleo ya Jamii
Meneja
Uhusiano na Usimamizi wa Kampuni ya Premium A ctive Yusuph
Mahundi amesema kampuni hiyo inafanya kazi katika
maeneo yote ya Mkoa wa Katavi kwa Wilaya ya Tanganyika ndiko
wanakofanya kazi katika sehemu kubwa na katika msimu wa kilimo
uliopita wamefanya kazi katika vyama vya msingi 14 na katika vyama hivyo
walitowa malengo ya uzalishaji kili 11.6 lakini ilipofika mwisho wa msimu
waliweza kununua kilo milioni 8.3 ambazo ndio zilikuwa zimezalishwa .Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Onesmo Buswelu akiishukuru Kampuni ya Premium kwa Mchango ilioutoa kwa Mkoa wa Katavi.
Ambazo kwa ujumla
wake zilkuwa na thamani ya dola 19.7 kwa fedha za kitanzania ni sawa na
shilingi Bilioni 47.4 ambapo kwenye fedha hizo kiasi cha Dola
500,000 waliweza kulipa ushuru kwenye Halmashauri za maeneo
yanayolima Tumbaku ambazo ni sawa na fedha za Kitanzania zaidi ya Bilioni
1.4 ,
Mahundi alieleza kuwa
wanaamini kiwango hicho cha fedha ni kikubwa ambacho kinaweza kuleta
maendeleo ya chachu kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi na pia kwa
Halmashauri za Mkoa wa Katavi .
Ameeleza kuwa msimu ujao
wa kilimo Kampuni hiyo inatarajia kununua kilo za Tumbaku milioni
11. 7 ambapo wameweza kuingia mikataba ba vyama 16 vya
ushirika vya msingi kwa ajiri ya kununua tumbaku kwenye vyama hivyo na
wanaendelea kuvishukuru vyama hivyo kwa kuendelea kuwaamini na kufanya
nao biashara na Premium .Baadhi ya watumishi Katika mkoa wa Katavi waliohudhuria hafla hiyo iliyofanyika Wilaya ya Tanganyika.
Mbunge wa
Jimbo la Mpanda Vijijini Moshi Kakoso alisema
kiasi hicho cha fedha kilichopokelewa kitatumiwa vizuri kwenye
maeneo yoye ya Halmashauri za Mkoa wa Katavi .
Ameiomba kampuni hiyo isiwachoke pindi watakapokuwa wamewaomba tena
msaada kama huu kwa ajiri ya huduma kwenye sekta nyingine
kwani yeye anatambua kuwa kampuni hiyo ya Premium ni kubwa hapa Duniani
kwani inashika nafasi ya tatu kwa ukubwa wa makampuni yanayo nunua Tumbaku .
Mwakilishi wa Mkuu wa
Mkoa ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo
Buswelu ameishukuru Kampuni hiyo kwa kuguswa na kile
walichoweza kupata kama faida yao na kisha sehemu kuirudisha kwa wananchi
kwenye kufanya shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu .Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini Mh Moshi Sulemani Kakoso akizungumzia namna Kampuni ya Premium imekuwa na mchango katika Halmashauri za mkoa wa Katavi kupitia Ushuru.
Amesisitiza
kuwa Halmashauri zote zilizopata fedha hizo kwa ajiri ya
kutengeneza madawati zihakikishe ifikapo Desemba 31 ziwe zimekamilisha
utengenezaji wa madawati hayo na wazingatie yawe na ubora ili watoto wa
wakulima wa Tumbaku na wasio wakulima kuweza kuyatumia .
Amesema Kampuni hiyo ni miongoni mwa makampuni yanayo nunua Tumbaku katika Mkoa wa Katavi na ni kampuni ambayo imekuwa ikifanya vizuri sana kwa kuwalipa wakulima wake kwa wakati malipo yao pasipo kuchelewa hivyo anaipongeza kampuni hiyo kwa hilo .