BILIONI 22 KUTATUA TATIZO LA MAJI MANISPAA YA MPANDA.

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira [MUWSA] Manispaa ya Mpanda CPA Rehema Nelson akiwa katika eneo la Mlima wa Veta litakapojengwa Tanki la Maji  kwa wananchi wa Manispaa ya Mpanda kupitia Mradi wa Maji wa Miji 28 

 

Na Paul Mathias,Mpanda

Wananchi katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wanatalajia kuondokana na Adha ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama ifikapo 2025.
Muonekano wa Bwawa la Milala ambalo litakuwa chanzo kikuu cha Usambazaji wa Maji katika Mradi wa Maji Miji 28 utakaogharimu Bilioni 22 Katika Manispaa ya Mpanda

Wananchi katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda wanatalajia kuondokana na Adha ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama ifikapo 2025.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Mpanda [MUWASA [CPA Rehema Nelson alipotembelea eneo la Mlima Veta ambalo litajengwa Tanki la Maji kupitia Mradi wa Maji wa Miji 28.

Rehema amesema kuwa katika eneo hilo kutajengwa Tanki la Maji lenye uwezo wa kuhifadhi Maji Lita Milioni 2 ambalo chanzo chake kikubwa kitakuwa Bwawa la Milala.

‘’Hapa ni eneo ambalo tutajenga Tanki la Maji lenye ujazo wa Lita Milioni Mbili Maji haya yatashuka kwa wananchi kupitia Njia ya Mseleleko na kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Mpanda na mradi huu utakuwa umetatua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa Manispaa ya Mpanda ’’anasema Rehema.

Greda ikisafisha Eneo la Mlima Veta Mpanda Manispaa ambapo litajengwa Tanki la Maji kupitia mradi wa Maji wa miji 28 litakuwa na uwezo wa kuhifadhi Maji lita Milioni 2 
Ameeleza kuwa Mradi wa Maji wa Miji 28 kupitia Chanzo cha Bwawa la Milala utagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 22 mradi huo umeanza kutekelezwa tangu Mwezi wa Nne Mwaka huu  na unatalajia kukamilika October 2025 .

Ameeleza kuwa kazi zitakazofanyika katika mradi huo ni ujenzi wa chanzo cha Maji katika Bwawa la milala pamoja na kujenga chujio la maji katika Bwawa hilo litakalokuwa na uwezo wa kuchuja maji Lita Milioni 12 sambamba na ujenzi wa Tanki la Maji katika eneo la Mlima Veta ambalo litakuwa na uwezo wa kuhifadhi Maji lita Milioni 2 ambayo yatasambazwa kwa wananchi wa Manispaa ya Mpanda kwa njia ya Mseleleko kwa Kilomita 40.

Amebainisha kuwa kwa sasa Muwasa inahudumia Kata 11 za Manispaa ya Mpanda kati ya Kata 15 za Manispa ya Mpanda na uzalishaji wa Maji kwa sasa ni zaidi ya Lita Milioni 7 huku kukiwa na upungufu wa lita za Maji Milioni 4 kwenye kata 11 wanazozihudumia kwa sasa.

 Katika hatua nyingine amesema kuwa Mradi wa Maji wa Miji pindi utakapo kamilika utakuwa muarobaini kwa wananchi wa Manispaa ya Mpanda kwani watapata huduma ya Maji kwa asilimia Miamoja katika kata zote 15 za Manispaa ya Mpanda.

’jumla ya kata 15 zinauhitaji wa Maji zaidi ya Milioni 15 tunatalajia kwamba ukijumlisha na hizi Lita milioni 12 zitakazo zinazalishwa kupitia Bwawa la milala na hizi Lita zaidi ya Milioni 7 tutakuwa na jumla ya lita Milioni 19.3 tunaimani kwamba Kukamilika kwa mradi huu wa Maji wa Miji 28 tutawahudumia wananchi wa Manispaa ya Mpanda’Kwa asilimia Miamoja’ ameeleza Rehema.

Ameishuru serikali kwa kuja na Mpango huo wa Mradi wa Maji wa Miji 28 ambao utawasaidia wananchi wa Manispaa ya Mpanda kupata huduma ya Maji kwa ufasaha na kutoa wito kwa wananchi kuunga mkono juhudi za serikali kwa kuilinda miundombinu itakayojengwa na serikali kwa manufaa ya Wananchi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages