RC KATAVI AWASHUKIA VIONGOZI WAZEMBE SERIKALI ZA MITAA NA VIJIJI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akizungumnza na wananchi katika Shule ya Msingi Kasisiwe Kata ya Ilembo juu ya umuhimu wa viongozi wa serikali za mitaa na Vijji kufanya mikutamo ya hadhara kwenye Maeneo yao.


Na Paul Mathias,Mpanda.

Viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji katika Mkoa wa Katavi wameagizwa kuitisha Mikutano ya hadhara kwa Wananchi ili kusikiliza kero zao ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji kwa nafasi walizonazo.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwananvua Mrindoko ,akikagua baadhi ya Majengo ya Madarasa katika Shule ya Msingi Kasisiwe kata ya Ilembo kwenye ziara hiyo.

Viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji katika Mkoa wa Katavi wameagizwa kuitisha Mikutano ya hadhara kwa Wananchi ili kusikiliza kero zao ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji kwa nafasi walizonazo.

Maagizo hayo yametolewa na mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko katika ziara yake ya Kutembelea Miradi ya Elimu na aliyoifanya Katika Manispaa ya Mpanda kwa lengo la kujioonea Mwenendo wa Miradi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akikagua Nyumba ya Walimu katika shule ya Sekondari Kawalyowa.

Akiwa katika Mradi wa Shule ya Msingi Kasisiwe Kata ya Ilembo Mkoa wa Katavi amewaagiza viongozi wa serikali za Mitaa na wenyeviti wa Vijiji kuzungumnza na wananchi na kutatua kero zao kwa vitendo ikiwemo kusoma mapato na Matumizi.

‘’Agizo hili nikwa wenyeviti wote wa Serikali za Mitaa na Vijiji mkoa mzima wa Katavi itisheni Mikutano ya hadhara someni mapato na Matumizi lakini pia sikilizeni wananchi wanakero gani zitatueni kero hizo’’amesema Mkuu huyo wa Mkoa

Amebainisha kuwa katika mikutano hiyo wananchi waelezwe umuhimu wa kuwaandikisha watoto wao Darasa la Awali na Darasa la Kwanza pamoja na kujiandaa kuwapeleka watoto wao Shule kujiunga na kidato cha Kwanza mwaka 2024.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli akielezea namna Halmashauri hiyo inavyosimamia fedha za miradi ya maendeleo kwenye Manispaa ya Mpanda.

‘’Mtakuwa na walimu wakuu au wataluma kwenye Mikutano hiyo wawaeleze wananchi utaratibu mwepesi kabisa wa kuandikisha watoto wa awali darasa la kwanza na kuwahamanasisha wazazi kujiandaa kuwapeleka watoto wao Kidato cha kwanza ‘’amesema Mrindoko

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewaonya vikali wazazi na walezi ambao hawato waandikisha   watoto wao shule ngazi ya awali na darasa la Kwanza pamoja na kidato cha kwanza mwaka 2024 na kuongeza kuwa serikali haiatawavumulia na hawatosita kuchukua sheria kali dhidi yao.

‘’Hatuta mvumilia mazazi au mlezi yeyote ambae hata mwandikisha mtoto wake shule wakati mtoto huyo anastahili kuandikishwa,hatuta mvumilia mazazi au mlezi ambae mtoto wake hato lipoti shule na kuanza kidato cha kwanza kwenye shule aliyopangiwa’’anasema Mrindoko.

Akiwa katika Shule hiyo ya Msingi Kasisiwe mkuu huyo wa Mkoa amesema kuwa Mradi wa shule hiyo unalidhisha na kuagiza miundombinu ya Madawati pamoja na miundo mbinu mingine ikamilishwe kwa Haraka ili watoto waanze kutumia Shule hiyo ambayo selikali imeleza zaidi ya Milioni 600 kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kundelea fedha za Maendeleo katika Wilaya ya Mpanda ikiwemo Manispaa ya Mpanda

Amewaomba watumishi wa umma katika mkoa wa Katavi kufanya kazi kwa uadilifu kwa kusimamia fedha za serikali zinazoletwa katika miradi mbalimbali ili wananchi wanufaike na serikali yao ya awamu ya Sita kupitia miradi hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia kumbuli amemhakikishia mkuu wa Mkoa wa Katavi kuwa Fedha zinazoletwa na serikali kwaajili ya kutekeleza miradi mbalimbali katika Manispaa ya Mpanda watazisimamia kwa uadilifu.

‘’Niku hakikishie Mkuu wa Mkoa sisi Manispaa ya Mpanda tunahakikisha feddha zinazoletwa na serikali kwaajili ya miradi ya maendeleo tunaisimamia na kuhakikisha Miradi hiyo inajengwa ili wananchi wapate huduma’’ anasema Kumbuli


Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi ametembelea miradi mbalimbali ikiwemo Ujenzi wa Shule ya Msingi Kasisiwe,Ujenzi wa Sekondari Kapalangawe,Ujenzi wa Shule ya Msingi Kawajense,Kutembelea shule ya Msingi Kivukoni Kata ya  Shanwe,Kutembelea ujenzi wa Nyumba ya Walimu katika Shule ya Sekondari Kawalyowa pamoja na Miradi mingine kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati ili iwanifaishe wananchi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages