|
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi,Kaster Ngonyani akiwa katika mdahalo na waandishi wa habari na jeshi la polisi mkoa wa Katavi ulikuwa unajadili masuala ya ulinzi kwa waandishi wa habari wakati wakitekeleza majukumu yao kwenye mazingira ya hatari. |
Na Paul Mathias,Katavi
Jeshi la Polisi katika mkoa wa
Katavi limesema kuwalitaendelea kushirikiana na waandishi wa habari katika utekelezaji wa amajukumu yake ya kuhakikisha usalama wa Raia na
mali zao unaimalishwa kwa wananchi.
|
Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzania [UTPC] Deogratius Nsokolo akielezea namna UTPC ilivyo jipanga kuhakikisha Waandishi wa Habari na Jeshi la polisi hapa nchini wanashirikiana kwa pamoja katika kazi kwa lengo la kuimarisha usalama. |
Jeshi la Polisi katika mkoa wa Katavi limesema kuwalitaendelea kushirikiana na waandishi wa katika utekelezaji wa amajukumu yake ya kuhakikisha usalama wa Raia na mali zao unaimalishwa kwa wananchi.
Hayo yamebaimishwa na kamanda wa
Polisi mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani wakati akifungua mudahalo maalumu kati ya
jeshi la polisi na waandishi wa Habari mkoa wa Katavi ulioandaliwa na Umoja wa
klabu za waandishi wa habari Tanzania [UTPC ]pamoja na Klabu ya waandishi wa
Habari mkoa wa Katavi[KTPC]
|
Waandishi wa Habari mkoa wa Katavi wakiwa na maafisa wa Polisi mkoa wa Katavi kwenye Mdahalo huo.
|
Ngonyani amesema kuwa waandishi
wa Habari katika mkoa wa Katavi wamekuwa chachu kwa jeshi la polisi kwa
kuupasha umma habari mbalimbali zinazoiasa jamii kujiepusha na vitendo vya
uharifu katika Shughuli zao za kila siku.
Ameeleza kuwa waandishi wa Habari
wanamchango mkubwa wa kuisaidia jamii katika kukemea vitendo vya ukatili wa
kijinsia ambavyo vimekuwa vikijitokeza pamoja na mmomonyoko wa maadili katika
jamii ambao umekuwa chanzo cha kuibuka kwa Makundi ya watoto watukutu ambao
wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya kiharifu.
|
Waandishi wa habari mkoa wa Katavi na Jeshi la polisi mkoa wa Katavi wakiwa katika picha ya Pamoja baada ya Mdahalo.
|
Katika hatua nyingine ameushukuru
Umoja wa Klabu za uandishi wa Habari Tanzania [UTPC] na umoja wa klabu ya
waandishi wa habari mkoa wa Katavi[ KTPC] kwa kuandaa mhadalo kuhusu Ulinzi na
usalama kwa mwandishi wa habari katika maeneo ya hatari hatua ambayo itasaidia
kupunguza migongano ya kiutendaji baina ya jeshi la polisi na waandishi wa
Habari kwenye matukio ya hatari.
‘’Niishukuru sana UTPC kwa kutukutanisha hapa leo baina yetu jeshi la
polisi na waandishi wa habari naimani tutatoka hapa tukiwa tunaimba wimbo mmoja
ambao ni kuzuia uharifu na vitendo vya kiharifu sisi kama polisi na waandishi
wa habari kupitia kalamu zao wataandika na kuiambia jamii kutokuwa sehemu ya
uharifu ‘’anasema Ngonyani.
Kwa upande wake Rais wa Klabu za
waandishi wa Habari Tanzania [UTPC] Deogratius Nsonkolo amewaasa waandishi wa habari kufanya kazi yao kwa weledi kwa kuzingatia Miiko ya kazi yao pasipo
kuathiari kundi lolote kwenye jamii ili kuepuka kuzua taharuki kwenye jamii.
‘’Sisi waandishi wa habari tunamaadili yetu tuyafate na kuyatimiza
tukienda kinyume tutaharibu kila kitu kwenye taifa letu tunapotengeneza
uwajibikaji kwa viongozi tumejenga mahusiano ya kufanyakazi na Jeshi la Polisi basi tusifichue maovu
ambayo yanafanyika kwenye maeneo ya kazi kitu cha masingi ni kuzingatia maadili ’’
anasema Nsonkolo.
|
Alinanuswe Edward Mwandishi wa Habari mkoa wa Katavi akichangia hoja mbalimbali kwenye mdahalo
Katika hatua nyingine Nsokolo ameeleza kuwa waandishi wa habari wataemdelea kuwa wadau wa usalama kwa kuandika habari zinazolenga kuzuia uharifu kwenye jamii ili jeshi la polisi kuchukua hatua kwa uharaka kupitia taarifa za waandishi wa habari
|
Amesema kuwa Umoja wa
klabu za waandishi wa Habari Tanzania zinalengo la kuhakikisha zinachochea
maendeleo kwenye mikoa kupitia waandishi wa Habari kwa kuandika na kutangaza
changamoto na suluhu ya matataizo hayo kwa lengo la kuhakikisha maendeleo
yanapatikana kwa wananachi na taifa zima kwa ujumla.