TAKUKURU KATAVI WAFANYA UFATILIAJI WA MIRADI YA ZAIDI YA BILIONI 3.2

Kaimu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stuart Kiondo akitoa taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi kwa Kipindi cha July na September.

Na walter Mguluchuma,Katavi

Taasisi ya  Kuzuia  na Kupambana na Rushwa  Takukuru Mkoa wa Katavi  kwa kipindi cha Mwezi wa Saba na Mwezi wa Tisa 2023 imeweza kufatilia  utekelezaji  wa Miradi  12 yenye  thamani ya   zaidi ya   Shilingi Bilioni  3.2 katika sekta ya elimu na kubaini uwepo wa  mapungufu mbalimbali .

Baadhi ya waandishi wa Habari mkoa wa Katavi wakitekeleza Majukumu yao wakati wa Kikao hicho.

Taasisi ya  Kuzuia  na Kupambana na Rushwa  Takukuru Mkoa wa Katavi  kwa kipindi cha Mwezi wa Saba na Mwezi wa Tisa  2023 imeweza kufatilia  utekelezaji  wa Miradi  12 yenye  thamani ya   zaidi ya   Shilingi Bilioni  3.2 katika sekta ya elimu na kubaini uwepo wa  mapungufu mbalimbali .

Kaimu  Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi  Stuart  Kiondo  amewaambia Wandishi wa Habari  wakati  akitowa taarifa ya utekelezaji wa kazi wa Taasisi hiyo  katika kipindi cha miezi mitatu ya Julai  hadi  September  mwaka huu.

Amesema katika kipindi hicho wameweza kusaidia  kufichua  ubadilifu  wa fedha  za Umma  Shilingi  Bilioni  1.23 ambazo  watumishi wa Halmashauri ya Mpimbwe  walifanya ubadilifu wa Fedha hizo

Watumishi hao  walikuwa wakifanya  malipo kwa mafundi  na miradi  hewa  kwa kutumia  mawakala  na watu  na watu mbalimbali  wanaotowa huduma za Kibenki kupitisha fedha hizo haramu na wanaendelea  kufanya uchunguzi  dhidi  ya  ubadilifu  huu wa fedha za umma.

Kiondo  ameeleza kuwa  katika  kipindi  cha Julai  hadi  Septemba  Takukuru  Mkoa wa Katavi  wamefatilia miradi 12 yenye thamani  ya Shilingi  Bilioni  3.25(3,250,750,000) iliyopo katka sekta ya elimu  na inaendelea kufatiliwa kwa karibu  kutokana na mapungufu mbalimbali ambayo walioibaini .

Katika kipindi hicho  Takukuru wameendelea  kupokea  malalamiko  na wameweza kupokea malalamiko  mbalimbali  na wameweza kupokea jumla ya malamiko  73 katika ya malalamiko hayo  54 yalihusu Rushwa na  19 hayakuhusu Rushwa .

Malalamiko yaliyohusu Rushwa yalihusu sekta za  Serikali za Mitaa 41,Mapato 2, Binafsi 1,Maji 1,Kilimo 2, Magereza  4, Elimu Msingi 2, kutokana na malalamiko hayo  majalada 5 yapo katika uchunguzi wa wazi  na yamefunguliwa majalada na  malamiko  9 uchunguzi wake umekamilika .

Katika kipindi hicho  mashauri  sita  yamefunguliwa  Mahakamani  na  kufanya kesi ambazo  zinaendelea  kufikia 13 ambapo kwenye kipindi hiki wameweza kushinda kesi mbalimbali za watu waliowafikisha Mahakamani .

Katika  hatua nyingine Kiondo amewaonya watu  wote ambao wamekuwa wakipita mitaani na kuwatapeli watu kuwa wao  ni maafisa wa Takukuru waache mara moja kwani  kwa wale watakao bainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages