MKOA WA KATAVI UMEFANIKIWA KULINDA MAENEO YALIYOHIFADHIWA KISHERIA

Afisa Wanyama  Pori wa Mkoa wa Katavi  Josephina  Rupia  ya  utunzaji wa  mazingira  na uhifadhi  wa maliasili  pamoja na  vyanzo vya maji     na  mkakati  wa upandaji miti wakati wa kikao cha  kamati ya ushauri ya Mkoa wa Katavi (RCC)  kwa  niaba ya Katibu  Tawala  msaidi Mkoa wa Katavi wa  Uchumi na uzalishaji

 Na Walter Mguluchuma,Katavi.

Serikari ya Mkoa wa  Katavi  imejikita katika  kuhakikisha  maliasili  zote na  maeneo yaliyohifadhiwa  yanalindwa  kwa mujibu wa  sheria  za uhifadhi  juhudi  hizo  zinadhihirishwa  kutokana na kuwepo  kwa ongezeko  la wanyama pori  kwenye maeneo ya Mkoa wa Katavi yaliyohifadhiwa  tofauti na hapo awali .


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko[Katikati]akiongoza kikao cha Kamati ya ushauri Mkoa wa Katavi,RCC

Serikari ya Mkoa wa  Katavi  imejikita katika  kuhakikisha  maliasili  zote na  maeneo yaliyohifadhiwa  yanalindwa  kwa mujibu wa  sheria  za uhifadhi  juhudi  hizo  zinadhihirishwa  kutokana na kuwepo  kwa ongezeko  la wanyama pori  kwenye maeneo ya Mkoa wa Katavi yaliyohifadhiwa  tofauti na hapo awali .

Hayo yamesemwa na  Afisa wanyama pori wa Mkoa wa Katavi   Josephina Rupia  wakati akisoma taarifa   ya utunzaji  wa mazingira  na uhifadhi wa  maliasili  kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Kataci (RCC) kilichofanyika  katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa huu taarifa hiyo aliyoisoma kwa niaba ya Katibi Tawala  msaidizi   wa Mkoa wa Mkoa wa Katavi  wa uchumi  na uzalishaji .

Amebainisha kuwa katika  kuhakikisha  maliasili  na maeneo yote  yaliyohifadhiwa  yanalindwa  kwa mujibu wa sheria  jitihada hizi  zimeanza kuonekana  kwa kuwepo kwa ongezeko  la wanyama pori  katika maeneo yaliyohifadhiwa katika Mkoa huu ammbapo  makundi   makubwa  ya wanyama kama  Tembo , Mbwa  mwitu , Tandala   , Twiga , Simba  na wengineo  wanaonekana wazi katika barabara ya Mpanda kwenda Tabora wakati hapo nyuma ilikuwa  ni hadimu kuwaona kwenye barabara hiyo.

Juhudi hizi zinakwenda  sambamba  na ongezeko  la wawindaji  wa kitalii waliotembelea  mapori ya akiba  ya Rukwa , Inyinga na Ugala ambapo kwa kipindi cha miaka   miwili iliyopita  jumla ya wawindaji  80 na watalii  92 walifika kwenye mapori hayo .

 Rupia alisema  Serikali ya Mkoa wa Katavi  imeendelea  kujiimarisha  katika suala  zima la utalii  kwa kuhakikisha  vivutio  vya utalii vinapatikana  ndani ya Mkoa  vinatangazwa ndani a nje   ya nchi  kwani hadi sasa kwa kipindi cha miaka mitano  watalii waliotembelea  Hifadhi ya Taifa  ya Katavi ni watalii  watalii  wa  nje   4,809 watalii wandani  14,281wageni wakazi  732.


Utunzaji wa  mazingira  na uhifadhi  wa maliasili  na vyanzo vya maji  ni shughuli  mtambuka  ambazo zinafanywa  na sekta  mtambuka  katika Mkoa huu na mamlaka za Serikali za mitaa,Hifdhi ya Taifa ya Katavi , TAWA ,TFS  ambapo  katika wilaya  za Mlele  Mpanda na Tanganyika wamekasimiwa    shughuli hizi  za uhifadhi  wa maliasili ,mazingira na   vyanzo vya maji .

Amefafanua kuwa  katika kuhakikisha  shughuli hizi  zinakuwa shirikishi  zaidi  Mkoa umehakikisha  jamii,taasisi  za umma  na binafsi   zinashiriki  kikamilifu  katika utunzaji wa mazingira ,uhifadhi  wa vyanzo vya maji  na upandaji miti  katika maeneo  yaliyopoteza uoto wa asili  na  katika vyanzo vya maji  inaendelea kutolewa .

Na juhudi hizi  za Mkoa wa Katavi  zimeleta matunda  kwa kufanikisha  upandaji wa miti  7,051,000 kwa kipindi  cha    mwaka  2022/2023 jambo ambalo linaloonyesha   namna  mkoa unavyojari  utunzaji wa mazingira .

Mbunge wa Jimbo la  Mpanda  Vjijini  Moshi   Kakoso  ameiomba Serikali ya Mkoa wa Katavi kuhakikisha inashughulikia  mgogoro ulipo wa  eneo la  mstu wa  Ntongwe Mashariki ulipo  baina ya Halmashauri ya  Wilaya ya Tanganyika na  Mamlaka ya  wanyama pori (TAWA)

Amesema pia kumekuwepo na upotevu wa mapato ya  fedha  za  vitalu vya  uwindaji katika  msti wa  Nkamba ambao unapakana na Wilaya ya  Nkasi  kitalu hicho kipo   katika maeneo mawili ya Tanganyika na Nkasi hivyo wanaonufaika na kitalu hicho ni Nkasi peke yao  .

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua   Mrindoko  amezitaka taasisi zote zinazosimamia   maliasili na mazingira kuhakikisha zinaendelea kusimamia sheria   ili  kuweza  kulinda maliasili za  nchi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages