WADAU HALMASHAURI YA WILAYA YA MLELE WAOMBWA KUENDELEA KUWASAIDIA WALEMAVU

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga wa [wa kwanza kulia Mwenye kanzu] akikabidhi viti mwendo kwa watu wenye ulemavu vilivyotolewa na Tanzania Big Game Safari kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kushoto  ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Teresia Irafay.

Na Mwandishi wetu,Mlele

Wadau mbalimbali wa Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wameombwa kuendelea kujitokeza kuwasaidia watu wenye ulemavu ikiwa ni sehemu ya  kuhakikisha kundi hilo linaishi bila changamoto yeyote.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga akiwa katika picha ya Pamoja na watendaji wa Halmashauri ya  Wilaya ya Mlele na  watu wenye ulemavu waliopatiwa viti mwendo.

Wadau mbalimbali wa Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa katavi  wameombwa kuendelea kujitokeza kuwasaidia watu wenye ulemavu ikiwa ni sehemu ya  kuhakikisha kundi hilo linaishi bila changamoto yeyote.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga  wakati akikabidhi viti mwendo 18 vya watu wenye ulemavu  kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele vya walemavu vilivyotolewa na wadau wa Maendeleo Tanzania Big Game Safari.

Mwakilishi wa Tanzania Big Game Safari akitoa neno la shukrani kwa Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kwa kuendelea kuwa wadau mhimu katika masuala ya Maendeleo kwa wananchi

Mwanga amesema kuwa wadau wa maendeleo wamekuwa ni watu mhimu katika maendeleo ya Wilaya ya Mlele na kuwaomba wadau wengine kuiga mfano wa Tanzania Big Game Safari kwa kuona umuhimu wa kuwasaidia watu walemavu.

‘’tuwashukuru sana Tanzania Big Game safari kwa msaada huu wa vitimwendo kwa watu wenye ulemavu tuwaombe sana wadau wengine kuendelea kuwasaidia waleamavu’’amesema Dc Mwanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele Teresia Irafay amewapongeza Tanzania Big Safari kwa kuendelea kuona umuhimu wa kutoa viti hivyo kwa walemavu ili viwasaidie katika shughuli zao.

Mwakilishi wa Tanzania Big Safari yenye Makao makuu yake Jijini Arusha amesema kuwa wataendelea kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mlele katika Sekta ya Elimu na Maendeleo ya Jamii kama sehemu ya kuungana na serikali katika kuwatumukia wananchi kwa vitendo.

Nao baadhi ya walemavu waliopatiwa viti mwendo hivyo wamesema wameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Mlele kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kuendelea kufanya kazi na wadau mbalimbali ikiwemo Tanzania Big Game safari ambao wameonyesha mfano mzuri kwa kutoa msaada huo kwao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages