MKOA WA KATAVI WAPATA MASHINE YA KUSAFISHA DAMU (DAYALISISI)

 

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akiongea na wajumbe wa Kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa wa Katavi[ RCC]

  

Na  Walter Mguluchuma,Katavi.

Wananchi katika Mkoa wa Katavi wameaondokana na adha kubwa iliyokuwa inawakabiri kwa muda mrefu  kuwafanya walazimike kuhamishia  makazi yao kwenye maeneo yenye Hospitali zinazotowa huduma ya kusafisha damu  kufatia  Hospitali ya Mkoa wa Katavi kupatiwa mashine tatu za kusafisha damu zitakazoanza kufanya kazi hivi karibuni .

Wajumbe mbali mbalimbali wa Kikao cha RCC Mkoa wa Katavi.

Wananchi katika Mkoa wa Katavi wameaondokana na adha kubwa iliyokuwa inawakabiri kwa muda mrefu  kuwafanya walazimike kuhamishia  makazi yao kwenye maeneo yenye Hospitali zinazotowa huduma ya kusafisha damu  kufatia  Hospitali ya Mkoa wa Katavi kupatiwa mashine tatu za kusafisha damu zitakazoanza kufanya kazi hivi karibuni

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt  Jonas Mollel  ameyabainisha hayo wakati wa kikao cha Kamati ya ushauri cha Mkoa wa Katavi  (RCC) kilichofanyika katika  ukumbi wa  ofisi ya Mkuu wa Mkoa   huu kilichoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko.

amesema kutokana na  umuhimu wa  mashine hizo  za kusafisha damu    Serikali  imeweza kuwatumia  fedha  Mkoa wa Katavi za  kununua  mashine tatu za kusafisha damu( DAYALISISI   kwa  ajiri ya  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huu)na tayari fedha hizo wameisha letewa na wameweza kununua kutoka MSD mashine tatu na tayari  zimeisha wasili  Katavi .

Mbunge wa Mpanda Mjini Sebastian Kapufi akichangio hoja mbalimbali katika kikao cha kamati ya ushauri Mkoa wa Katavi[RCC]

Dkt Molllel amesema lengo la Mkoa ni kuwa na mashine kumi ambazo walikuwa wameomba kuweza kupatiwa lakini kwa kuanzia wameanza na mashine hizo tatu ambazo zitakapoanza kazi  zitawasaidia sana wakazi wa Mkoa wa Katavi   kuweza kupatiwa huduma hiyo pasipo kusafiri kwenda katika  Mikoa mingine .

Amebainisha kuwa pamoja  na kuwepo kwa mashine hizo bado kuna changamoto ya  jengo  litakalotumika  kuwekea huduma hiyo kwani kwa sasa hospitali hiyo   haina jingo hilo maalumu ila wameisha anza kufanya utaratibu wa kujenga jengo hilo maalumu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi .

Mbunge wa Jimbo la Mpanda  Mjini Sebastiani  Kapufi  alikiambia  kikao hicho cha RCC   kuwa kuna watu wengi wamehama hapa Katavi wengine  wamehamia  Jijijini Mbeya  na  maeneo mengine kwa ajiri ya  kufata  huduma yam ashine  ya kusafisha damu kutokana   kutowepo  kwa mashine hizo katika  Mkoa huu .

Amesema kutoka na umuhimu wa mashine hizo yeye  binafsi kama hakutakuwa na mashariti mengine ya  kitaalamu yupo  tayari kutowa nyumba yake  nzima  iwezekutumika  kwa ajiri ya kuweka mashine hizo hili wananchi wasogezewe  huduma karibu .

Alisisitiza kuwa kutokana na mahitaji makubwa ya wananchi kwa huduma hiyo aliomba mashine hizo zifungwe mapema na zianze kutowa huduma kwa wananchi wa Mkoa huu ambao  wengine wanazimika kupanga   vyumba vya kuishi  huko Mbeya    na wapo waliopanga  vyumba  kwa kipindi cha  miezi sita kwa ajiri ya kuwa karibu na huduma hiyo .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mwanamvua Mrindoko  alisema    huduma ya  mashine za kusafisha damu ni muhimu sana   zianze kutolewa  kwa wananchi wa Mkoa huu kutokana na mahitaji yalipo kwa sasa kwa wananchi .

Amesema kama swala  la upatikanaji wa fedha za ujenzi wa   jingo hilo maalamu  litakalotumika    kwa ajiri ya utoaji wa huduma hiyo Mkoa utaangalia namna ya kuwashirikisha wadau mbalimbali   ili kuwezesha huduma  hizo  zianze kutolwa na mapema  kama ambavyo Serikali ilivyokusudiwa .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages