Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,ACP August Urio |
Na George Mwigulu,Katavi.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja akiwa na vifaa vya Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi ambapo lengo lake ni kuvitumia kwenye matukio ya kiharifu.
Kaimu kamada wa Jeshi la Polisi
wa Mkoa huo, ACP August Urio akitoa taarifa leo kwa Waandishi wa Habari katika
mahabusu ya wilaya Mpanda amesema kuwa mtuhumiwa huyo ni miongoni mwa watu 83
waliokamatwa kwa makosa mbalimbali kwa kipindi cha mwenzi Desemba mwaka
uliopita.
Urio amefafanua kukamatwa kwa
mtuhumiwa huyo akiwa na vifaa vya Jeshi kama vile sare za Jeshi la Wananchi na
Polisi,Pingu zikiwa na funguo zake pamoja na mkanda ni matokeo bora ya
doria na misako wanayoifanya
kubaini,kuzuia na kutanzua uhalifu.
Kaimu kamanda huyo ameeleza katika
msako huo Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mtu mmoja akiwa na dawa za kulevya zidhaniwazo
kuwa mirungi gramu tatu,watu nane wakiwa na dawa za kulevya zidhaniwazo kuwa ni
bhagi kg 4 na kete 90 pamoja na watuhumiwa 17 wakiwa na pombe haramu ya moshi kiasi cha lita 405.
Aidha watu 56 wanaojihusisha na
matukio ya wizi,uporaji,uvunjaji na unyang’anyi
wamekutwa wakiwa na vielelezo za wizi Pikipiki nne MC.456 BCS aina ya
Fekoni,MC 861 DDR aina ya Kinglion, MC 104 DWL aina ya Sanlg na aina ya Sanlg
isiyokuwa na namba “ tumewakamata pia na mbolea za ruzuku mifuko 48.Npk mifuko
29,Can mifuko 11 na Urea mifuko 8” Amesema Urio.
Katika hatua nyingine Jeshi la
Polisi Mkoa wa Katavi limepata mafanikio ya kesi mahakamani ambapo watuhumiwa
108 wamefikishwa mahakamani ikiwa watuhumiwa 28 wamehukumiwa vifungo
gerezani,watuhumiwa 26 wamehukumiwa kulipa faini,watuhumiwa 10 wameachiwa huru
na 44 bado kesi zao zinaendelea
mahakamani.
Vilevile Jeshi la Polisi
linawaomba wananchi wa Mkoa wa Katavi kuongeza ushirikiano katika mapambano
dhidi ya uhalifu kwa kutoa taarifa zitakazo saidia Mkoa kuendelea kuwa salama.