WANANCHI WALALAMIKIA KUCHELEWESHEWA KULIPWA FIDIA KUPISHA MRADI WA MAJI MIJI 28

Baadhi ya Nyumba zilizowekwa alama ya kubomolewa kupisha Mradi wa Maji wa Bwawa la Milala eneo la Mtaa wa Mtemi Beda Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi

 Na Walter Mguluchuma,Katavi

Baadhi ya Wananchi wa  Mtaa wa Mtemi  Beda Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoani  Katavi  wameiomba Serikali iweze  kuwalipa fidia zao za  makazi  wanayoishi  baada ya kutakiwa  kupisha ujenzi wa  wa Maji wa Miji 28 katika Manispa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Nelia Nelson mkazi wa mtaa wa Mtemi Beda akiiomba serikali kuwalipafidia ili waweze kupisha maeneo hayo kwaajili ya Mradi wa Maji.

Baadhi ya Wananchi wa  Mtaa wa Mtemi  Beda Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoani  Katavi  wameiomba Serikali iweze  kuwalipa fidia zao za  makazi  wanayoishi  baada ya kutakiwa  kupisha ujenzi wa  wa Maji wa Miji 28 katika Manispa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Wananchi hao wamedai kuwa  toka walipoagizwa  na Serikali ya kuwataka  wananchi hao  waondoke  umbali wa mita 300 kutoka  kwenye bwawa la milala kwa makubaliano ya kulipwa  fidia ya makazi yao wanaoishi  hadi sasa  hawaja lipwa fidia za kuwawezesha wahame kwenye eneo hilo .

Mmoja wa wakazi hao  Gebo  Katagwa  amedai kuwa  wanalia kilio kikubwa  sana  kwa sababu  toka Serikali ya Mkoa wa Katavi ilipotoa agizo  la kuwataka waondoke kwenye maeneo hayo na kuzuiawa kuendeleza majengo yao hawaoni kinachoendelea kwao zaidi ya wao kuwa  hatarini ya kubomokewa na nyumba wanazoishi  .

Baadhi ya Nyumba zilizowekwa alama ya kubomolewa kupisha Mradi wa Maji wa Bwawa la Milala eneo la Mtaa wa Mtemi Beda Kata ya Misunkumilo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi

Ameomba Serikali  iwasaidie walipwe  fedha zao mapema  ili waweze  kahama kwenye maeneo hayo ili  mvua  zisije zikawaua bure  kwani wameisha zuiwa kuendelea na ujenzi hivyo hata kufanya ukarabati wa nyumba zao wanashindwa na kupelekea baadhi yao kuwa wananyeshewa na mvua  .

Amebainisha kuwa toka mwezi wa kumi mwaka huu walivyofanyiwa tathimini  hawajaambiwa lolote mara baada ya kuwa limefanyika zoezi hilo  na kupewa kusaini  fomu za fedha wanazotakiwa kulipwa na kisha kuondoka jumla hivyo wanaiomba Serikali  iwasaidie walipwe   fedha zao wakajenge makazi mengine ya kuishi  ili wasije wakafa bure na mvua amesema Katagwa .

Lucia  Evaristi  amesema Serikali iwalipe mapema  ili na wao wajuwe  sehemu wanayoelekea kwani wanao watoto ambao  wanatakiwa kuanza cheke chea na darasa la kwanza  mpaka sasa hawajuwi wanaelekea wapi kwa kuwa hawajalipwa fidia zao .

Amebainisha kuwa  wameendelea kukaa   ndani na karatasi zao ambazo walifanyiziwa tathimini wanaiomba  Serikali kwa kuwa imeisha amua kuwahamisha kwenye   maeneo hayo basi waweze kuwalipa kwamuda muafaka .

Faridi Paulo  amesema kuwa baada ya kuwa wamefanyiwa tathimi waliambiwa kuwa watalipwa baada ya wiki mbili  na wao kwa sasa wanahari mbaya kwani nyumba zao zinazidi  kuharibika  na kubomoka kwa kuwa wameisha ambiwa wasiendeleze  kitu chochote kilehivyowanashindwa kufanya ukarabati  .

Amemwomba Rais  Samia awasaidie kwa hilo  ili waweze kulipwa  fidia zao hizo kwani hari zao zimekuwa  ngumu kutokana na baadhi ya watu wengine kuamua kuhama   eneo hilo na kwenda kuishi katika nyumba za kupanga na familia zao .

Nelia Nelson  amaesema kuwa  wameshindwa kufanya kitu chochote hata kupanda  mboga wameshindwa   matokeo yake hakuna maendeleo yanayofanyika matokeo yake  ni nyumba  kuanza kubomoka  basi was aid iwe kulipwa fedha mapema ili waondoke .

Ameeleza kama wanaendelea kubaki waluhusiwe kuendelea kufanya maendeleo kama walivyokuwa wakifanya  maendeleo ya  makazi yao na  shughuli nyingine za kujiongezea kipato chao kama hapo awali .

Diwani wa Kata ya  Misunkumilo  Afred  Matondo amesema kuwa ni kweli wananchi hao  wa Mtaa wa Mtemi Beda wapatao zaidi ya 140 wanadai  fidia yao kwa ajiri ya  kupisha eneo la  bwawa la Milala kunakotekelezwa  mradi wa  Miji 28 ambapo  Serikali  bado wapo wanaendelea  na  mchakato wa kuwalipa fidia wananchi hao .

Hivyo hadi sasa  kwenye eneo hilo   la  wananchi wengi wanao lalamika wameisha fanyiwa  tathimini ya malipo yao isipokuwa watu  wachache tuu  ambao ndio  bado kufanyiwa .

Diwani wa Kata ya Misunkumilo Afred Matondo akielezea mchakato wa fidia kwa wananchi hao

Amesema licha ya taratibu  hizo kuwa zinaendelea kumekuwepo kwa baadhi ya changamoto  ya baadhiya wananchi ambao hawajajitokeza  kufanyiwa tathimini  na kusababisha kukamilika kwa zoezi hilo  hata hivyo yeye kama Diwani amepanga kwenda kufanya mkutano na wananchi hao ili awaelimishe kwani ni vigumu watu kulipwa kabla ya kujiridhishs kwanza .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages